Kaunti ya Kiambu
- Kuhusu mji, soma Kiambu
Kaunti ya Kiambu | |||
---|---|---|---|
Kaunti | |||
![]() | |||
| |||
Kiambu County in Kenya.svg![]() Kaunti ya Kiambu katika Kenya | |||
Nchi | ![]() | ||
Ilianzishwa | Machi 4th 2013 | ||
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Kati | ||
Makao Makuu | Kiambu | ||
Kikao cha Serikali | Thika | ||
Gavana | Ferdinand Waititu | ||
Naibu wa Gavana | Dkt. James Nyoro | ||
Seneta | Kimani Wamatangi | ||
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa) | Gathoni wa Muchomba | ||
Bunge la Kaunti | Bunge la Kaunti ya Kiambu | ||
Spika | Stephen Ndichu[1] | ||
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa | 60[2] | ||
Maeneo bunge/Kaunti ndogo | 12 | ||
Eneo | 2,449.2 km2 (945.6 sq mi) | ||
Idadi ya watu | 1,623,282[3] | ||
Kanda muda | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) | ||
Tovuti | kiambu.go.ke |
Kaunti ya Kiambu ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.
Ilikuwa mojawapo ya wilaya za Kenya katika Mkoa wa Kati baada ya nchi kupata uhuru.
Makao makuu ya kaunti hii ni mji wa Kiambu. Hata hivyo, utendaji wa kaunti hutekeleza majukumu yake kutoka Thika.
Kupakana na Nairobi kumeifanya iwe na idadi ya wakazi wengi mijini, kwa sababu ya maendeleo katika sekta ya mali yasiyohamishika. Sekta za viwanda na ukulima pia zimechangia kukuza kaunti hii kiuchumi.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Kaunti hii imepakana na kaunti za Nairobi (kusini), Machakos (mashariki), Nakuru (magharibi), Nyandarua (kaskazini magharibi) na Murang'a (kaskazini).
Topografia ya kaunti ina nyanda za juu na nyanda za kati.
- Nyanda za juu kabisa zinapatikana katika kata ndogo ya Lari, ambazo ni kuenea kwa Safu za Nyandarua. Sehemu hiyo huwa na vilima vikali na ni chanzo cha maji.
- Nyanda za juu wastani ziko katika Limuru na sehemu za Gatundu Kusini, Gatundu Kaskazini, Githunguri na Kabete. Sehemu hizo zina vilima na tambarare zilizoinuka.
- Nyanda za kati hupatikana katika Juja, Thika na Ruiru. Sehemu hizo huwa kavu kidogo kuliko sehemu zingine za kaunti[4].
Kaunti ina vyanzo kadhaa vya maji.
- Chanzo cha maji cha Nairobi ni chanzo cha Mto Nairobi, Mto Gitaru, Mto Gitahuru, Mto Karura, Mto Ruirwaka, na Mto Gatharaini.
- Chanzo kingine ni chanzo cha Mto Kamiti na Mto Ruiru ambacho huwa na Mto Riara, Mto Kiu, Mto Makuyu, Mto Bathi, Mto Gatamaiyu na Mto Komothai.
- Chanzo cha maji cha tambarare za Aberdare ni chanzo cha Mto Thiririka na Mto Ndarugu.
- Chanzo cha nne ni chanzo cha Mto Chania na matawimto yake: Mto Thika na Mto Kariminu, inayotoka Mlima Kinangop. Mito hii ni matawimto ya Mto Athi.[4]
Kiambu hupata misimu miwili ya mvua: Machi hadi Mei na Septemba hadi Disemba. Miezi kati ya Juni hadi Agosti huwa msimu wa baridi kali. Halijoto hutegemea na eneo. Maeneo ya nyanda za juu hupata baridi zaidi. Kata ndogo za Lari na Limuru na sehemu za magharibi za Gatundu Kusini, Gatundu Kaskazini na Githunguri hupata ukungu mzito na baridi ifikayo 7°c[4].
Serikali na Utawala[hariri | hariri chanzo]
Utendaji[hariri | hariri chanzo]
Gavana, sasa Ferdinand Waititu, ndiye mkuu wa kaunti na serikali. Yeye huchaguliwa kwa muhula wa miaka mitano katika uchaguzi mkuu. Ana nguvu za utendaji na za kuteua wanakamati wa Kamati ya Utendaji ya Kaunti baada ya kuidhinishwa na Bunge la Kaunti. Hata ingawa mji mkuu wa kaunti uko Kiambu, utendaji wa serikali uko mji wa Thika.
Bunge[hariri | hariri chanzo]
Bunge la Kaunti ya Kiambu ni la chumba kimoja. Lina wajumbe 60 waliochaguliwa kutoka wadi sitini za kaunti na wajumbe 27 walioteuliwa[5]. Kila mjumbe anashikilia hatamu ya miaka mitano, inayofanywa upya katika uchaguzi mkuu. Spika wa bunge na naibu wake huchaguliwa na wajumbe. Bunge la Kiambu liko katika mji wa Kiambu.
Mahakama[hariri | hariri chanzo]
Kuna Mahakama Kuu ya Kiambu iliyoanzishwa tarehe 20 Juni 2016. Ina jaji mmoja.[6]
Utawala[hariri | hariri chanzo]
Kamishna wa kaunti huteuliwa na Rais wa Kenya. Yeye ni mwakilishi wa rais kusaidia na mambo ya utawala wa serikali ya kitaifa.
Kaunti ndogo[hariri | hariri chanzo]
Kaunti imegawanywa katika maeneo yafuatayo:
Eneo bunge/kata ndogo | Wadi |
---|---|
Githunguri | Githunguri, Githiga, Ikinu, Ngewa, Komothai 3 |
Kiambaa | Cianda, Karuri, Ndenderu, Muchatha, Kihara |
Kabete | Gitaru, Muguga, Nyathuna, Kabete, Uthiru |
Limuru | Bibirioni, Limuru Kati, Ndeiya, Limuru Mashariki, Ngecha Tigoni |
Lari | Kinale, Kijabe, Nyanduma, Kamburu, Lari/Kirenga |
Gatundu Kaskazini | Gituamba, Githobokoni, Chania, Mang'u |
Gatundu Kusini | Kiamwangi, Kiganjo, Ndarugo, Ng'enda |
Ruiru | Githothua, Biashara, Gatongora, Kahawa Sukari, Kahawa Wendani, Kiuu, Mwiki, Mwihoko 1 |
Kikuyu | Karai, Nachu, Sigona, Kikuyu, Kinoo |
Juja | Murera, Theta, Juja, Witeithie, Kalimoni |
Thika | Township, Kamenu, Hospital, Gatuanyaga |
Kiambu | Ting'ang'a, Ndumberi 3, Riabai, Township |
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ http://www.nation.co.ke/counties/Kiambu/Stephen-Ndichu-Kiambu-Speaker/1183274-4087286-7a5c2kz/index.html
- ↑ http://kiambucountyassembly.go.ke/assembly/about-us.html
- ↑ Kenya Census 2009. scribd.com. Iliwekwa mnamo 20 June 2016.
- ↑ 4.0 4.1 4.2 COUNTY INTEGRATED DEVELOPMENT PLAN 2013 – 2017. Iliwekwa mnamo 2018-05-02.
- ↑ http://kiambucountyassembly.go.ke/assembly/about-us.html
- ↑ http://www.judiciary.go.ke/portal/blog/post/kiambu-gets-high-court
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Kiambu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |