Kaunti ya Machakos
Ili kusoma kuhusu mji, soma Machakos
Kaunti ya Machakos | |||
---|---|---|---|
Kaunti | |||
![]() Ofisi ya gavana wa Machakos | |||
| |||
Machakos County in Kenya.svg![]() Kaunti ya Machakos katika Kenya | |||
Coordinates: 01°14′S 37°23′E / 1.233°S 37.383°E | |||
Nchi | ![]() | ||
Namba | 16 | ||
Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 | ||
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Mashariki | ||
Makao Makuu | Machakos | ||
Miji mingine | Kangudo, Matuu, Kithimani, Athi River | ||
Gavana | Dkt. Alfred Mutua, CBS | ||
Naibu wa Gavana | ENG. Francis Maliti Wambua | ||
Seneta | Boniface Mutinda Kabaka | ||
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa) | Joyce Kamene | ||
Bunge la Kaunti | Bunge la Kaunti ya Machakos | ||
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa | 40 | ||
Maeneo bunge/Kaunti ndogo | 8 | ||
Eneo | 5,952.9 km2 (2,298.4 sq mi) | ||
Idadi ya watu | 1,098,584 | ||
Kanda muda | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) | ||
Tovuti | http://www.machakosgovernment.com/ |
Kaunti ya Machakos ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.
Makao makuu yako Machakos. Inatarajiwa kuwa na mji wa Konza ambao ndio mji wa kwanza wa teknohama katika Afrika Mashariki.
Jiografia[hariri | hariri chanzo]
Kaunti ya Machakos inapakana na Nairobi, Kiambu, Murang'a (magharibi), Embu (Kaskazini), Kitui (mashariki), Makueni na Kajiado(kusini). Tabianchi ya Kaunti ya Machakos ni nusu kavu. Ina mandhari yenye vilima[1]. Udongo katika maeneo mengi ni udongo wa mfinyanzi ulio mwekundu. Hata hivyo, kuna mito ambayo huchimbwa mchanga haramu. Jambo hili huharibu mandhari kwa kukausha mito[2].
Mto Tana na Mto Athi hupitia katika kaunti hii. Bwawa la Masinga liko kaskazini katika mpaka wa Machakos na Embu.
Kiwango cha ardhi kilicho misitu ni 7.6%. Vyanzo vya maji katika kaunti ni Vilima vya Iveti, Muumandu, Kalimanzalu and Kiima Kimwe[2].
Machakos hupata misimu miwili ya mvua, Oktoba hadi Disemba na Machi hadi Mei. Maeneo yaliyo na vilima hupata mvua mingi, kiwango cha mm 1000, kuliko maeneo kavu ambayo hupata mvua ya kiwango cha mm 500. Mwezi wa Julai huwa na baridi zaidi[2].
Utawala[hariri | hariri chanzo]
Kaunti ya Machakos imegawanywa katika maeneo yafuatayo[3]:
Eneo bunge | Wadi |
---|---|
Masinga | Kivaa, Masinga, Central, Ekalakala, Muthesya, ndithini |
Yatta | Ndalani, Matuu, Kithimani, Ikomba, Katangi |
Kangundo | Kangundo North, Kangundo Central, Kangundo East, Kangundo West |
Matungulu | Tala, Matungulu North, Matungulu East, Matungulu West, Kyeleni |
Kathiani | Mitaboni, Kathiani Central, Upper Kaewa/Iveti, Lower Kaewa/Kaani |
Mavoko | Athi River, Kinanie, Muthwani, Syokimau/Mulolongo |
Machakos Town | Kalama, Mua, Mutitini, Machakos Central, Mumbuni North, Muvuti/Kiima-Kimwe, Kola |
Mwala | Mbiuni, Makutano/Mwala, Masii, Muthetheni, Wamunyu, Kibauni |
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Machakos Government - Official Website. Iliwekwa mnamo 2018-04-18.
- ↑ 2.0 2.1 2.2 Machakos County Integrated Development Plan, 2015. Iliwekwa mnamo 2018-04-26.
- ↑ Machakos County. Iliwekwa mnamo 2018-04-18.
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Machakos kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |