Kaunti ya Elgeyo-Marakwet

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani ya Kaunti ya Elgeyo-Marakwet,Kenya

Kaunti ya Elgeyo-Marakwet ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 454,480 katika eneo la km2 3,032, msongamano ukiwa hivyo wa watu 150 kwa kilometa mraba[1].

Wakimbiaji wengi mashuhuri hutoka Marakwet ni pamoja na Moses Kiptanui, Evans Rutto, Reuben Kosgei, Ezekiel Kemboi, Brigid Kosgei, Ishmael Kirui, Timothy Kitum, Sally Kirui, Abraham Chebii na Richard Chelimo. Shaif Shaheen aliyejulikana mwanzoni kama Stephen Cherono wa Qatar, Edna Kiplagat wa Uholanzi, Geoffrey Kamworor na Raymond Yator wanatoka upande wa Keiyo.

Makao makuu yako Iten.

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Elgeyo-Marakwet ina maeneo bunge yafuatayo[2]:

Eeneo bunge Kata
Marakwet Mashariki Kapyego, Sambirir, Endo, Embobut/Embulot
Marakwet Magharibi Lelan, Sengwer, Cherang'any/Chebororwa, Moiben/Kuserwo, Kapsowar, Arror
Keiyo Kaskazini Kamariny, Emsoo, Tambach, Kapchemutwa
Keiyo Kusini Kaptarakwa, Chepkorio, Soy North, Soy South, Kamiebit, Metkei

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [3][hariri | hariri chanzo]

  • Keiyo North 99,176
  • Keiyo South 120,750
  • Marakwet East 97,041
  • Marakwet West 137,513

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  2. http://countytrak.infotrakresearch.com/Elgeyo-Marakwet-county/
  3. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.