Nenda kwa yaliyomo

Kaunti ya Turkana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kaunti ya Turkana
Kaunti
Mto Turkwel ukiwa umekauka wakati wa ukame
Kaulimbiu: ""

Kaunti ya Turkana katika Kenya
Coordinates: 3°09′N 35°21′E / 3.150°N 35.350°E / 3.150; 35.350
Nchi Kenya
Nambari23
IlianzishwaTarehe 4 Machi 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Bonde la Ufa
Mji mkuuLodwar
Miji mingineLokichogio, Kakuma, Lokichar
Serikali
GavanaJeremiah Napotikan
Naibu wa GavanaPeter Lotethiro Emuria
SenetaJames Lomenen
Mwakilishi wa wanawakeJoyce Akai Emanikor
BungeBunge la Kaunti ya Turkana
Wawakilishi Wadi30
Maeneo bunge6
Eneo
Jumlakm2 68 232.9 (sq mi 26 344.9)
Idadi ya Watu
Jumla926,976
Msongamano14 /km²
Majira ya SaaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovuti
turkana.go.ke

Kaunti ya Turkana ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 926,976 katika eneo la km2 68,232.9 msongamano ukiwa hivyo wa watu 14 kwa kilometa mraba[1].

Makao makuu yako Lodwar.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Turkana ndio kaunti kubwa zaidi ikiwa na km2 71 597.8 (sq mi 27 644.1). Imepakana na Uhabeshi, Sudani Kusini (kaskazini), Uganda (magharibi), Pokot Magharibi, Baringo, Samburu (kusini) na Marsabit (mashariki).

Turkana ina safu za milima: Milima Loima, Milima Lorengippi, Milima Mogila, Milima Songot, Milima Kalapata, Milima Loriu, Milima Kailong’kol na Milima Silale. Safu hizo ni vyanzo vya maji. Vilima vya Tepes, Vilima vya Lokwanamoru, Vilima vya Lorionotom, Vilima vya Pelekech na Vilima vya Loima pia hupatikana katika Turkana[2].

Tambarare za kaunti hupatikana katika sehemu kavu za kaunti.

Mto Tarach, Mto Kerio, Mto Kalapata, Mto Malimalite na Mto Turkwel ndio mito mikuu katika kaunti. Mito hii hupungua kiwango cha maji msimu wa kiangazi, na kukauka wakati wa ukame[3]. Ziwa Turkana liko mashariki mwa kaunti. Limegawanywa kati ya Turkana, Marsabit na Uhabeshi. Katika maeneo karibu na ziwa, kuna chemchemi zilizopo. Chemchemi za Eliye ndio chemchemi maarufu na kivutio cha watalii[2].

Hoteli ya Eliye Springs.

Turkana ina tabianchi kavu na nusu kavu. Kaunti hupata misimu miwili ya mvua: Aprili hadi Julai na Oktoba hadi Novemba[2].

Kaunti ya Turkana imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo[4]:

Eneo bunge Kata
Turkana Kaskazini Kaeris, Lake zone, Lapur, Kaaleng/Kaikor, Kibish, Nakalale
Turkana Magharibi Kakuma, Lopur, Letea, Songot, Kalobeyei, Lokichoggio, Nanaam
Turkana Kati Kerio Delta, Kang'atotha, Kalokol, Lodwar Township, Kanamkemer
Loima Kotaruk/Lobei, Turkwel, Loima, Lokiriama/Loren Gippi
Turkana Kusini Kaputir, Katilu, Lobokat, Kalapata, Lokichar
Turkana Mashariki Kapedo/Napeito M, Katilia, Lokori/Kochodin

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [5]

[hariri | hariri chanzo]
  • Kibish 36,769
  • Loima 107,795
  • Turkana Central 185,305
  • Turkana East 138,526
  • Turkana North 65,218
  • Turkana South 153,736
  • Turkana West 239,627

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  2. 2.0 2.1 2.2 "SECOND ANNUAL DEVELOPMENT PLAN" (PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (pdf) mnamo 2018-01-27. Iliwekwa mnamo 2018-05-02.
  3. Cheboit, Emanuel. "Crisis in Turkana as only River dries up - Citizentv.co.ke". Iliwekwa mnamo 2018-05-02.
  4. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-08-14. Iliwekwa mnamo 2021-08-14.
  5. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.