Kaunti ya Nyandarua
Kaunti ya Nyandarua | |||||
---|---|---|---|---|---|
Kaunti | |||||
![]() | |||||
| |||||
Nyandarua County in Kenya.svg![]() Kaunti ya Nyandarua katika Kenya | |||||
Nchi | ![]() | ||||
Namba | 18 | ||||
Ilianzishwa | Tarehe 4 Machi, 2013 | ||||
Ilitanguliwa na | Mkoa wa Kati | ||||
Makao Makuu | Ol Kalou | ||||
Miji mingine | Ol Joro Orok, Kipipiri | ||||
Gavana | Francis Thuita Kimemia,EGH, CBS, HSC | ||||
Naibu wa Gavana | Cecilia Wanjiru Mbuthia | ||||
Seneta | Paul Githiomi Mwangi | ||||
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa) | Faith Wairimu Gitau | ||||
Bunge la Kaunti | Bunge la Kaunti ya Nyandarua | ||||
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa | 25 | ||||
Maeneo bunge/Kaunti ndogo | 5 | ||||
Eneo | km2 3 285.7 (sq mi 1 268.6) | ||||
Idadi ya watu | 638,289 | ||||
Wiani wa idadi ya watu | 194 | ||||
Kanda muda | Saa za Afrika Mashariki (UTC+3) | ||||
Tovuti | nyandarua.go.ke |
Kaunti ya Nyandarua ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.
Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 638,289 katika eneo la km2 3,285.7, msongamano ukiwa hivyo wa watu 194 kwa kilometa mraba[1].
Makao makuu ya Kanti ya Nyandarua yako kwenye mji wa Ol Kalou.
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]Kaunti ya Nyandarua imepakana na Nyeri, Murang'a (mashariki), Kiambu (kusini), Nakuru (magharibi) na Laikipia (kaskazini).
Iko mashariki mwa Bonde la Ufa ambalo kuumbwa kwake kulisababisha kuwepo kwa safu ya milima ya Aberdare. Milima ya Nyandarua imezungukwa na Mbuga ya Kitaifa ya Aberdare na Hifadhi ya Msitu wa Aberdare[2]. Msitu huo ndio chanzo cha Mto Malewa, Mto Pesi, Mto Turasha, Mto Chania, Mto Kiburu, Mto Mkungi na Mto Kitir[3].
Nyandarua ina Ziwa Ol Bolossat ambalo ni ziwa la pekee katika ukanda wa kati. Kuwepo kwa ziwa hilo kunatishiwa na shughuli za binadamu k.v. ukulima na uchimbaji mawe[4].
Nyandarua huwa na tabianchi baridi na yenye unyevu. Ina misimu miwili ya mvua, Machi hadi Mei na Septemba hadi Disemba[3].
Utawala
[hariri | hariri chanzo]Kaunti ya Nyandarua imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo[5]:
Eneo bunge | Kata |
---|---|
Kinangop | Engineer, Gathara, North Kinangop, Murungaru, Njabini/Kibiru, Nyakio, Magumu, Githabai |
Kipipiri | Wanjohi, Kipipiri, Geta, Githioro |
Ol Kalou | Karau, Kanjuire Ridge, Milangine, Kaimbaga, Rurii |
Ol Jorok | Gathanji, Gatimu, Weru, Charagita |
Ndaragwa | Leshau/Pondo, Kiriita, Central, Shamata |
Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [6]
[hariri | hariri chanzo]- Kinangop 111,410
- Nyandarua South 93,870
- Mirangine 67,214
- Kipipiri 93,855
- Nyandarua Central 75,262
- Nyandarua West 97,965
- Nyandarua North 98,698
- Aberdare National Park 5
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
- ↑ "The Aberdare Ranges". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2020-09-18. Iliwekwa mnamo 2018-04-28.
- ↑ 3.0 3.1 NYANDARUA COUNTY INTEGRATED DEVELOPMENT PLAN Ilihifadhiwa 12 Julai 2018 kwenye Wayback Machine., Ilipatikana mnamo 28/04/2018
- ↑ Obura, Fredrick. "Region's economy under threat as Central Kenya's Lake Ol Bolossat faces extinction :: Kenya - The Standard". Iliwekwa mnamo 2018-04-29.
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2021-09-04. Iliwekwa mnamo 2021-09-04.
- ↑ "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Kenya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kaunti ya Nyandarua kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |