Kaunti ya Nyandarua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kaunti ya Nyandarua
Kaunti
Bendera Nembo ya Serikali
Nyandarua County in Kenya.svg
Kaunti ya Nyandarua katika Kenya
Nchi Kenya
Namba18
IlianzishwaTarehe 4 Machi, 2013
Ilitanguliwa naMkoa wa Kati
Makao MakuuOl Kalou
Miji mingineOl Joro Orok, Kipipiri
GavanaFrancis Thuita Kimemia,EGH, CBS, HSC
Naibu wa GavanaCecilia Wanjiru Mbuthia
SenetaPaul Githiomi Mwangi
Mbunge Mwanamke(Bunge la Taifa)Faith Wairimu Gitau
Bunge la KauntiBunge la Kaunti ya Nyandarua
Wawakilishi wa Bunge la Kaunti waliochaguliwa25
Maeneo bunge/Kaunti ndogo5
Eneo3,285.7 km2 (1,268.6 sq mi)
Idadi ya watu638,289
Wiani wa idadi ya watu194
Kanda mudaSaa za Afrika Mashariki (UTC+3)
Tovutinyandarua.go.ke

Kaunti ya Nyandarua ni mojawapo ya kaunti za Kenya zilizopo baada ya katiba mpya ya Jamhuri ya Kenya kupatikana mwaka 2010.

Wakati wa sensa ya mwaka 2019 wakazi walikuwa 638,289 katika eneo la km2 3,285.7, msongamano ukiwa hivyo wa watu 194 kwa kilometa mraba[1].

Makao makuu ya Kanti ya Nyandarua yako kwenye mji wa Ol Kalou.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Nyandarua imepakana na Nyeri, Murang'a (mashariki), Kiambu (kusini), Nakuru (magharibi) na Laikipia (kaskazini).

Iko mashariki mwa Bonde la Ufa ambalo kuumbwa kwake kulisababisha kuwepo kwa safu ya milima ya Aberdare. Milima ya Nyandarua imezungukwa na Mbuga ya Kitaifa ya Aberdare na Hifadhi ya Msitu wa Aberdare[2]. Msitu huo ndio chanzo cha Mto Malewa, Mto Pesi, Mto Turasha, Mto Chania, Mto Kiburu, Mto Mkungi na Mto Kitir[3].

Nyandarua ina Ziwa Ol Bolossat ambalo ni ziwa la pekee katika ukanda wa kati. Kuwepo kwa ziwa hilo kunatishiwa na shughuli za binadamu k.v. ukulima na uchimbaji mawe[4].

Nyandarua huwa na tabianchi baridi na yenye unyevu. Ina misimu miwili ya mvua, Machi hadi Mei na Septemba hadi Disemba[3].

Utawala[hariri | hariri chanzo]

Kaunti ya Nyandarua imegawanywa katika maeneo bunge yafuatayo[5]:

Eneo bunge Kata
Kinangop Engineer, Gathara, North Kinangop, Murungaru, Njabini/Kibiru, Nyakio, Magumu, Githabai
Kipipiri Wanjohi, Kipipiri, Geta, Githioro
Ol Kalou Karau, Kanjuire Ridge, Milangine, Kaimbaga, Rurii
Ol Jorok Gathanji, Gatimu, Weru, Charagita
Ndaragwa Leshau/Pondo, Kiriita, Central, Shamata

Idadi ya wakazi katika kaunti ndogo (2019) [6][hariri | hariri chanzo]

  • Kinangop 111,410
  • Nyandarua South 93,870
  • Mirangine 67,214
  • Kipipiri 93,855
  • Nyandarua Central 75,262
  • Nyandarua West 97,965
  • Nyandarua North 98,698
    • Aberdare National Park 5

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.
  2. The Aberdare Ranges. Jalada kutoka ya awali juu ya 2020-09-18. Iliwekwa mnamo 2018-04-28.
  3. 3.0 3.1 NYANDARUA COUNTY INTEGRATED DEVELOPMENT PLAN Archived 12 Julai 2018 at the Wayback Machine., Ilipatikana mnamo 28/04/2018
  4. Obura, Fredrick. Region's economy under threat as Central Kenya's Lake Ol Bolossat faces extinction :: Kenya - The Standard. Iliwekwa mnamo 2018-04-29.  
  5. http://countytrak.infotrakresearch.com/Nyandarua-county/
  6. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2019-11-13. Iliwekwa mnamo 2021-05-30.