Milima Aberdare

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Milima Aberdare.

Milima ya Aberdare (ambayo zamani ilikuwa inajulikana kama Milima ya Sattima, kwa Kikuyu: Nyandarua) ni safu ya milima yenye urefu wa kilomita 160 katika upande wa kaskazini wa mji mkuu wa Kenya ambao ni Nairobi na yenye wastani wa kimo wa mita 3.350 (futi 11,000) juu ya usawa wa bahari. Milima hiyo inapatikana katika sehemu ya magharibi ya kati ya Kenya, kaskazini mashariki ya Naivasha na Gilgil na kusini mwa ikweta. Milima hii hufomu sehemu ya mashariki ya Bonde la Ufa la Afrika Mashariki inayoteremka kutoka kwa tambarare ya Kinangop hadi kwa ngome ya Laikipia ambayo iko kaskazini ukielekea kusini. Upande wa mashariki, mtiririko wa maji wa milima hii huteremka ndani ya Bonde la Ufa na unaweza kuona Ziwa Naivasha na ngome ya Mau kwa mbali.

Safu ya milima ya Aberdare.

Milima ya Aberdare ina msitu mzito. Wingi wa msitu umelindwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Aberdare tangu ianzishwe mwaka wa 1950. Anuwai hii huvutia idadi kubwa ya wapenzi wa kutembea na wapandaji milima, wanaoendesha shughuli zao nje ya miji ya Naivasha na Gilgil. Mteremko wa chini hutumiwa kwa ukulima huku maeneo ya juu yanajulikana sana kwa wanyamapori. Tukio la The Rhino Charge ni tukio la kila mwaka linaloendeshwa na wahafidhina nchini Kenya wanaolipa kuweka ua katika mbuga ya kitaifa ya Aberdare kama njia ya kulinda msitu mkubwa kabisa katika eneo la Afrika Mashariki kutoka kwa uharibifu.

Jina la zamani la milima hii bado linatumiwa katika sehemu ya Oldoinyo la Satima ("mlima wa ng'ombe dume mdogo"); ifikapo mita 4,001 wa milima (futi 13.120), ndicho kilele cha juu kabisa katika Milima ya Aberdare. Mlima Kenya (mita 5.199, futi 17,057), mlima wa pili mkubwa barani Afrika (baada ya Mlima Kilimanjaro), unapatikana kilomita kadhaa mashariki mwa Milima ya Aberdare.

Eneo hili linajulikana sana kama makao makuu ya Dedan Kimathi, kiongozi wa kundi la Mau Mau lililoanzishwa mwaka 1950. Pia, Malkia Elizabeth akawa Malkia wa Uingereza wakati alikuwa amekufa kutembea katika Milima hii ya Aberdares. Eneo hili pia lilikuwa eneo ambalo JA Hunter alimwua tembo katika msitu wa Aberdare.

Jiolojia[hariri | hariri chanzo]

Aberdare iko katika sehemu ya vyanzo vya maji kwa mabwawa ya Sasumua na Ndakaini, ambazo hutoa zaidi ya maji kwa wakazi wa mji mkuu wa Kenya, Nairobi. Maeneo ya Msitu wa Mlima ni vyanzo vya Mto Tana, mto mkubwa zaidi nchini Kenya, ambayo husambaza maji kwa “Seven Fork hydropower plants” zinaotengeneza zaidi ya asilimia 55 ya jumla ya umeme nchini Kenya.

Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Mazingira kuu ndani ya milima hii ya Aberdare ni pamoja na Msitu ya mvua ambayo ina misitu ya mianzi na kisha moorland. Pembe za magharibi ya mwinuko wa kilima haina wanyamapori wengi ikilinganishwa na miteremko wa misitu upande wa mashariki ambayo ni makazi kwa wanyamapori mbalimbali kwa upana. Kuna umati wa tembo, nyati, Nguruwe wa msitu na vilevile kifaru ambaye yuko hatarini. Aina za paka wanaweza kuonekana pamoja kama vile chui na paka wa dhahabu wa Kiafrika ambaye ni nadra. Wanyamapori wengine ambao wako hatarini ni pamoja na nguchiro wa aina ya Jackson. Tumbili wa rangi Nyeusi na nyeupe ambaye anajulikana sana kama Colobus na tumbili wa aina ya Sykes ni wengi katika sehemu hii, na vilevile ni ndogoro, forhi, mindi, paka wa aina ya serval na pongo.

Aberdare ina mimea mbalimbali tajiri. Kuna spishi za mimea 778i, spishi zingine ambazo zinapatikana katika Mbuga ya Kitaifa ya Aberdare, kutokana na mvua na kimo cha mbuga hii. Aina ya miti ni pamoja na mkulo, mtarakwa, mpodo na mlozilozi.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Coordinates: 0°25′S 36°38′E / 0.417°S 36.633°E / -0.417; 36.633