Mto Nairobi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto Nairobi

Mto Nairobi ni mto unaopitia Nairobi, mji mkuu wa Kenya. Ndio mto mkuu katika beseni la mito ya Nairobi, mtandao wa mito kadhaa inayopita sambamba kuelekea mashariki. Mito yote katika beseni hilo hukutana mashariki mwa Nairobi na kuungana na Mto Athi, hatimaye kuelekea Bahari ya Hindi.

Mingi kati ya mito hii ni myembamba na michafu sana. Mito ya Nairobi huchafuliwa na taka kutoka kilimo, makazi duni na viwanda[1].

Mkondo mkuu, Mto Nairobi, umeweka mpaka wa kaskazini mwa jiji. Mto huu umefanywa kanali katika sehemu nyingine.

Mto Nairobi una vijito kadhaa, kama vile (katika utaratibu wa kushuka kutoka kaskazini hadi kusini):

Mto Motoine unafululiza katika Dimbwi la Nairobi, ziwa lililofanywa na wanadamu kutoa maji ya kunywa kwa wakazi wa Nairobi. Mbele zaidi huendelea kama Mto Ngong.

Baadhi ya kingo za mito pia zinajulikana kwa sifa mbaya ya ukosefu wa usalama. Mito hii hugawanya mji kutokana na ukosefu wa mapito yafaayo.

Wakati wa misimu ya mvua maji huongezeka, na kusababisha athari ya mafuriko katika mito yenye kingo zilizo chini.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Ramani[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Biosafety News, Oktoba / Novemba 2002: Uchafuzi wa Mto Nairobi tisho kwa afya Archived 23 Oktoba 2006 at the Wayback Machine.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]