Reli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Njia ya reli
Reli ya garimoshi yenyewe
Kituo cha reli mjini Mumbai. Reli ya Uhindi inabeba abiria milioni 17 kila mwaka [1] iko kati ya reli kubwa duniani.[2]

Reli (kutoka Kiing. rail / railroad) ni mfumo wa usafiri wa abiria na mizigo kwa treni zinazotembea juu ya vyuma au pau za feleji. Reli ni sehemu muhimu za miundombinu wa nchi. Kwa maana asilia "reli" ni zile "reli za chuma" au reli za garimoshi ambazo kwa kawaida hutumiwa mbili-mbili kijozi kufanya njia ya reli yenyewe.

Kwa nchi nyingi reli ni mtindo muhimu wa usafiri kwa sababu inarahisisha mwendo wa watu na bidhaa. Ikitumiwa vema gharama zake ni afadhali kuhusu usafiri wa barabarani. Mahitaji ya nishati kwa kiwango cha mzigo ni kidogo kuliko barabarani.[3]

Faida yake ni hasa tabia za njia yake; reli za garimoshi huwa na uso tambarare isiyonyoka kwa hiyo magurudumu ya treni hutembea kwa msuguano mdogo.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. http://news.bbc.co.uk/2/hi/south_asia/6287152.stm
  2. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-02-02. Iliwekwa mnamo 2009-12-03.
  3. Railroad Fuel Efficiency Sets New Record Archived 4 Juni 2008 at the Wayback Machine.- American Association of Railroads
Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Reli kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.