Nenda kwa yaliyomo

Mkoa wa Pwani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Barabara ya Pwani
Mkoa wa Pwani katika Tanzania

Mkoa wa Pwani ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepakana upande wa Kaskazini na mkoa wa Tanga, upande wa mashariki na Dar-es-Salaam na Bahari Hindi, upande wa kusini na mkoa wa Lindi na upande wa magharibi na mkoa wa Morogoro. Mkoa huo una eneo la km² 32,407, na idadi ya wakazi wapatao 2,024,947 kadiri ya sensa ya mwaka 2022 [1] kutoka 1,098,668 (2012). Mkoa huo ni maarufu kwa shughuli za utalii hususani katika mji wa Bagamoyo, kisiwa cha Mafia na Hifadhi ya Taifa ya Saadani. Makao makuu ya mkoa yako Kibaha.

Una postikodi namba 61000.

Wilaya na wakazi

Wilaya za Mkoa wa Pwani

Mkoa wa Pwani una wilaya nane (katika mabano idadi ya wakazi wakati wa sensa ya mwaka 2022 [2]):

Mkoa huo wenyeji wake ni watu wa makabila ya Wakwere, Wazaramo, Wandengereko, Wadoe, Wazigua na Wanyagatwa.

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huo ulikuwa na majimbo ya uchaguzi tisa yafuatayo [3]:

Tazama pia

Tanbihi

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-11-07. Iliwekwa mnamo 2022-11-14.
  2. https://www.nbs.go.tz
  3. Kuhusu makadirio ya idadi ya watu katika majimbo ya uchaguzi Tanzania Bara kwa mwaka 2016: [http://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/majimbo/MAJIMBOApril_Kisw.pdf

Viungo vya nje