Wilaya ya Mafia
Mafia ni moja kati ya wilaya 6 za mkoa wa Pwani katika Tanzania yenye postikodi namba 61700[1]. Eneo lake ni hasa Kisiwa cha Mafia na visiwa vidogo karibu nacho. Mji mkuu na makao makuu ya wilaya ni Kilindoni. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, wilaya ilikuwa na wakazi wapatao 46,438 [2] walioishi humo.
Kata za wilaya ya Mafia ni kama zifuatazo[3]:
Shehia | Eneo km² |
Wakazi 2002 |
Vijiji |
---|---|---|---|
Baleni[4] | 132.1 | 9137 | Baleni, Kungwi, Ndagoni[5], Chunguruma |
Jibondo | 21.9 | 3405 | Jibondo, Chole, Juani |
Kanga | 52.7 | 3317 | Kanga, Bweni |
Kilindoni | 36.8 | 11696 | Kilindoni, Dongo |
Kirongwe | 77.0 | 5260 | Kirongwe, Jimbo, Banja, Jojo |
Kiegeani | 40.3 | 3379 | Kiegani, Marimbani |
Miburani | 52.3 | 4363 | Miburani, Mlongo, Chemchem |
Wilaya ya Mafia | 413 | 40801 | 20 villages |
Baleni, Kanga na Kirongwe kwa pamoja ni tarafa ya kaskazini, shehia nyingine ni tarafa za kusini.
Wilaya hii inajumuisha funguvisiwa pamoja na kisiwa cha Mafia ndani yake inayotazama mwambao wa Afrika ya Mashariki 130 km kusini ya Daressalaam karibu na mdomo wa Mto Rufiji. Umbali wake na bara ni 16 km.
Mafia kisiwa kikuu ina urefu wa 50 km na upana wa 8 km; eneo lake ni takriban 400 km². Inajulikana pia kwa jina "Chole shamba" kutokana na mji wa kale wa Chole iliyokuwepo kwenye kisiwa kidogo cha Chole mjini karibu na kisiwa kikuu.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ https://www.tcra.go.tz/images/documents/postcode/pwani.pdf[dead link]
- ↑ Sensa ya 2012, Pwani - Mafia DC. Jalada kutoka ya awali juu ya 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 2016-06-13.
- ↑ [International Resources Group: Strategic Environmental Assessment of Mafia Island, FINAL REPORT, Volume II: Main Report] (PDF)
- ↑ Tangu kupatikana kwa orodha hii Baleni imegagiwa na Ndagoni kuwa kata ya pekee
- ↑ Tangu kupatikana kwa orodha hii Baleni imegagiwa na Ndagoni kuwa kata ya pekee
![]() |
Kata za Wilaya ya Mafia - Mkoa wa Pwani - Tanzania | ![]() |
---|---|---|
Baleni • Jibondo • Kanga • Kiegeani • Kirongwe • Kilindoni • Miburani • Ndagoni |
![]() | Makala hii kuhusu maeneo ya Tanzania bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Mafia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno. |