Mkoa wa Katavi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Mkoa wa Katavi
Mahali paMkoa wa Katavi
Mahali paMkoa wa Katavi
Location in Tanzania
Nchi Tanzania
Kanda Nyanda za Juu ua Kusini
Serikali
 - Mkuu wa Mkoa Rajab Mtumwa
Eneo
 - Jumla 45,843 km²
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 1,152,958
EAT (UTC+3)
Msimbo wa posta 50xxx
Kodi ya simu 025
Tovuti:  katavi.go.tz

Mkoa wa Katavi ni mmojawapo kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 50000. Ulianzishwa rasmi mnamo Machi 2012 kwa kumega mkoa wa Rukwa.

Makao makuu yako Mpanda.

Wilaya

Wilaya za mkoa huo ni tano tu: Mlele, Nsimbo, Mpanda mjini, Tanganyika (awali Mpanda vijijini) na wilaya ya Mpimbwe.

Wakazi

Katika sensa ya mwaka 2022 idadi ya wakazi ilihesabiwa kuwa 1,152,958 [1].

Utamaduni

Kabila kubwa ni lile la Wafipa; pia kuna Wabende, Wapimbwe na Wakonongo na dini yao kwa kiasi kikubwa sana ni Ukristo wa madhehebu ya Kanisa Katoliki.

Wapimbwe wanapatikana katika maeneo ya wilaya ya Mpimbwe katika vijiji vya Mamba, Mpimbwe na Majimoto. Katika kijiji cha Mamba kuna kivutio kizuri: bwawa kubwa la asili la maji ya moto ambayo hayapoi muda wote, ni ya moto iwe mchana au usiku.

Pia kuna sehemu za mkoa huu ni wa kihistoria katika baadhi ya maeneo. Mfano mtaa wa Madukani ambao walikua wakiishi Wahindi na Waarabu wa Oman kama Mzee Yusuf Al Salmi.

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

Tazama pia

Marejeo

  1. https://www.nbs.go.tz

Viungo vya nje

Viungo vya nje


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Katavi bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.