Mkoa wa Manyara

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa wa Manyara katika Tanzania
Wilaya za Mkoa wa Manyara

Mkoa wa Manyara ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania wenye postikodi namba 27000. Umepakana na mikoa ya Arusha na Kilimanjaro upande wa kaskazini, Mkoa wa Tanga upande wa mashariki, Mkoa wa Dodoma upande wa kusini na mikoa ya Singida na Shinyanga upande wa magharibi.

Mkoa wa Manyara umetengwa na Mkoa wa Arusha mwaka 2002 kwa azimio la rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ukiwa na eneo la km² 46,359.

Babati ndiyo makao makuu ya mkoa.

Wakazi[hariri | hariri chanzo]

Jumla ya wakazi mkoani ilikuwa 1,892,502 katika sensa ya mwaka 2022 [1].

Idadi hiyo imepatikana katika wilaya 7 zifuatazo (katika mabano idadi ya wakazi mwaka 2022): Babati Vijijini (375,200), Babati Mjini (129,572), Hanang (367,391), Mbulu Vijijini (238,272), Mbulu Mjini (138.593), Simanjiro (291,169) na Kiteto (352,305).

Sensa zinaonyesha kwamba ni kati ya mikoa ya Tanzania yenye ongezeko kubwa la wakazi. Pia ni kati ya mikoa yenye maambukizi machache zaidi ya Ukimwi.

Wenyeji wa mkoa huu ni pamoja na Wairaqw, Wamasai, Wambugwe, Wagorowa na Wabarbaig wakijihusisha na shughuli za kilimo na ufugaji kama njia ya kuingiza kipato chao cha kila siku.

Majimbo ya bunge[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi 7 yafuatayo:

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Manyara bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Manyara kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.