Nenda kwa yaliyomo

Mkoa wa Kilimanjaro

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa wa Kilimanjaro
Mahali paMkoa wa Kilimanjaro
Mahali paMkoa wa Kilimanjaro
Mahali pa Mkoa wa Kilimanjaro katika nchi ya Tanzania
Majiranukta: 3°20′S 37°20′E / 3.333°S 37.333°E / -3.333; 37.333
Nchi Tanzania
Wilaya 7
Mji mkuu Moshi
Serikali
 - Mkuu wa Mkoa
Eneo
 - Jumla 13,209 km²
Idadi ya wakazi (2022)
 - Wakazi kwa ujumla 1,861,934
Tovuti:  http://www.kilimanjaro.go.tz/

Mkoa wa Kilimanjaro ni mojawapo ya mikoa 31 ya Tanzania, uliopo kaskazini-mashariki mwa nchi. Unapakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Arusha magharibi, na Mkoa wa Tanga upande wa kusini. Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022, mkoa una wakazi 1,861,934. Makao makuu ya mkoa huo yako Moshi mjini. Mkoa huo unajulikana zaidi kwa kuwa na Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu zaidi barani Afrika, ambao pia ni kivutio kikuu cha utalii kutoka dunia nzima. Mkoa huu una historia tajiri ya biashara, na kilimo, hasa cha kahawa, na unajulikana kwa kiwango cha juu cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi ukilinganisha na mikoa mingine ya Tanzania, ingawa teknolojia ya utandawazi katika eneo kubwa haijashamiri.

Mkoani Kilimanjaro kuna wakazi wapatao 1,861,934 (sensa ya mwaka 2022[1].).

Makabila makubwa mkoani humo ni Wachagga, Wagweno na Wapare, ambapo pia kuna makabila mengine madogomadogo kama Wamasai na Wakamba.

Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 7 ambazo ni: Hai, Mwanga, Moshi mjini, Moshi vijijini, Rombo na Same na ile mpya ya Siha.

Ramani Wilaya au manisipaa Wakazi (2022) Tarafa Kata Kijiji Eneo km²
Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro
Wilaya za Mkoa wa Kilimanjaro
Wilaya ya Hai 240,999 17 1,217
Wilaya ya Moshi Vijijini 535,803 32 1,300
Wilaya ya Moshi Mjini 331,733 21 63
Wilaya ya Mwanga 148,763 20 1,831
Wilaya ya Rombo 275,314 28 1,471
Wilaya ya Same 300,303 34 6,221
Wilaya ya Siha 139,019 17 1,217
Jumla 1,861,934 152 13,209
Wilaya ya Siha hii ilianzishwa mwaka 2007 kutokana na maeneo ya wilaya ya Hai.
Marejeo: Mkoa wa Kilimanjaro

Majimbo ya bunge

[hariri | hariri chanzo]

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

  • Hai
  • Siha
  • Moshi Mjini
  • Mwanga
  • Same Mashiriki
  • Same Magharibi
  • Moshi Vijijini
  • Vunjo
  • Rombo

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Kilimanjaro kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Isipokuwa usitaje majina ya viongozi waliopo sasa maana wanabadilika haraka mno.