Mkoa wa Kilimanjaro
Mkoa wa Kilimanjaro |
|
![]() |
|
Majiranukta: 3°20′S 37°20′E / 3.333°S 37.333°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Wilaya | 7 |
Mji mkuu | Moshi |
Serikali | |
- Mkuu wa Mkoa | |
Eneo | |
- Jumla | 13,209 km² |
Idadi ya wakazi (2022) | |
- Wakazi kwa ujumla | 1,861,934 |
Tovuti: http://www.kilimanjaro.go.tz/ |
Mkoa wa Kilimanjaro ni mojawapo ya mikoa 31 ya Tanzania, uliopo kaskazini-mashariki mwa nchi. Unapakana na Kenya upande wa kaskazini, Mkoa wa Arusha magharibi, na Mkoa wa Tanga upande wa kusini. Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2022, mkoa una wakazi 1,861,934. Makao makuu ya mkoa huo yako Moshi mjini. Mkoa huo unajulikana zaidi kwa kuwa na Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu zaidi barani Afrika, ambao pia ni kivutio kikuu cha utalii kutoka dunia nzima. Mkoa huu una historia tajiri ya biashara, na kilimo, hasa cha kahawa, na unajulikana kwa kiwango cha juu cha maendeleo ya kijamii na kiuchumi ukilinganisha na mikoa mingine ya Tanzania, ingawa teknolojia ya utandawazi katika eneo kubwa haijashamiri.
Wakazi
[hariri | hariri chanzo]Mkoani Kilimanjaro kuna wakazi wapatao 1,861,934 (sensa ya mwaka 2022[1].).
Makabila makubwa mkoani humo ni Wachagga, Wagweno na Wapare, ambapo pia kuna makabila mengine madogomadogo kama Wamasai na Wakamba.
Wilaya
[hariri | hariri chanzo]Mkoa wa Kilimanjaro una wilaya 7 ambazo ni: Hai, Mwanga, Moshi mjini, Moshi vijijini, Rombo na Same na ile mpya ya Siha.
Ramani | Wilaya au manisipaa | Wakazi (2022) | Tarafa | Kata | Kijiji | Eneo km² |
---|---|---|---|---|---|---|
![]() |
Wilaya ya Hai | 240,999 | 17 | 1,217 | ||
Wilaya ya Moshi Vijijini | 535,803 | 32 | 1,300 | |||
Wilaya ya Moshi Mjini | 331,733 | 21 | 63 | |||
Wilaya ya Mwanga | 148,763 | 20 | 1,831 | |||
Wilaya ya Rombo | 275,314 | 28 | 1,471 | |||
Wilaya ya Same | 300,303 | 34 | 6,221 | |||
Wilaya ya Siha | 139,019 | 17 | 1,217 | |||
Jumla | 1,861,934 | 152 | 13,209 | |||
Wilaya ya Siha hii ilianzishwa mwaka 2007 kutokana na maeneo ya wilaya ya Hai. | ||||||
Marejeo: Mkoa wa Kilimanjaro |
Majimbo ya bunge
[hariri | hariri chanzo]Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Hai
- Siha
- Moshi Mjini
- Mwanga
- Same Mashiriki
- Same Magharibi
- Moshi Vijijini
- Vunjo
- Rombo
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]
![]() | |
---|---|
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Songwe | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Kilimanjaro kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
|