Wilaya ya Same


Wilaya ya Same ni wilaya mojawapo kati ya wilaya 7 za Mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania.
Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 269,807. Katika ile ya mwaka 2022 walihesabiwa 300,303 [1].
Wilaya hii imepakana upande wa kazkazini na Wilaya ya Mwanga na nchi jirani ya Kenya, upande wa kusini na Mkoa wa Tanga na upande wa magharibi na Mkoa wa Manyara. Makao makuu yapo Same Mjini.
Upande wa kusini wa Milima ya Pare upo ndani ya wilaya pamoja na sehemu ya Hifadhi ya Mkomazi.[2]
Njia ya reli ya Usambara inapita wilayani.
Marejeo[hariri | hariri chanzo]
- ↑ https://www.nbs.go.tz
- ↑ (June 2015) Tanzania travel guide, 6, Lonely Planet, 148. ISBN 978-1742207797. Retrieved on 12 January 2016.
Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]
- Same Profile, Kilimanjaro Region website Archived 26 Machi 2016 at the Wayback Machine.
![]() |
Kata za Wilaya ya Same - Mkoa wa Kilimanjaro - Tanzania | ![]() | ||
---|---|---|---|---|
Bangalala | Bendera | Bombo | Bwambo | Chome | Gavao Sawene | Hedaru | Kalemawe | Kihurio | Kirangare | Kisima | Kisiwani | Lugulu | Mabilioni | Makanya | Maore | Mhezi | Mpinji | Mshewa | Msindo | Mtii | Mwembe | Myamba | Ndungu | Njoro | Ruvu | Same Mjini | Stesheni | Suji | Tae | Vudee | Vuje | Vumari | Vunta
|