Nenda kwa yaliyomo

Mikoa ya Tanzania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tanzania imegawiwa katika mikoa 31, ikiwemo 26 upande wa bara na 5 upande wa Zanzibar.

Mikoa ya Tanzania, miji mikuu, eneo na idadi ya wakazi

Mkoa Makao
makuu
Wilaya Eneo
(km2)
Idadi ya
Wakazi[1]
Msimbo wa
posta
Kanda
Arusha Arusha 7 34,516 2,356,255 23xxx Kaskazini
Dar es Salaam Dar es Salaam 5 1,393 5,383,728 11xxx Pwani
Dodoma Dodoma 7 41,311 3,085,625 41xxx Kati
Geita Geita 5 20,054 2,977,608 30xxx Ziwani
Iringa Iringa 5 35,503 1,192,728 51xxx Nyanda za Juu za Kusini
Kagera Bukoba 8 39,627 2,989,299 35xxx Ziwani
Katavi Mpanda 3 45,843 1,152,958 50xxx Nyanda za Juu za Kusini
Kigoma Kigoma 8 45,066 2,470,967 47xxx Kati
Kilimanjaro Moshi 8 13,209 1,861,934 25xxx Kaskazini
Lindi Lindi 6 67,000 1,194,028 65xxx Pwani
Manyara Babati 6 47,913 1,892,502 27xxx Kaskazini
Mara Musoma 7 31,150 2,372,015 31xxx Ziwani
Mbeya Mbeya 7 60,350 2,343,754 53xxx Nyanda za Juu za Kusini
Morogoro Morogoro 7 70,799 3,197,104 67xxx Pwani
Mtwara Mtwara 7 16,707 1,634,947 63xxx Pwani
Mwanza Mwanza 7 9,467 3,699,872 33xxx Ziwani
Njombe Njombe 6 21,347 889,946 59xxx Nyanda za Juu za Kusini
Pemba Kaskazini Wete 2 574 272,091 75xxx Zanzibar
Pemba Kusini Chake Chake 2 332 271,350 74xxx Zanzibar
Pwani Kibaha 7 32,407 2,024,947 61xxx Pwani
Rukwa Sumbawanga 4 22,792 1,540,519 55xxx Nyanda za Juu za Kusini
Ruvuma Songea 5 66,477 1,848,794 57xxx Nyanda za Juu za Kusini
Shinyanga Shinyanga 5 18,901 2,241,299 37xxx Ziwani
Simiyu Bariadi 5 25,212 2,140,497 39xxx Ziwani
Singida Singida 6 49,437 2,008,058 43xxx Kati
Songwe Vwawa 5 1,344,687 Nyanda za Juu za Kusini
Tabora Tabora 7 76,151 3,391,679 45xxx Kati
Tanga Tanga 10 27,348 2,615,597 21xxx Kaskazini
Unguja Kaskazini Mkokotoni 2 470 257,290 73xxx Zanzibar
Unguja Mjini Magharibi Jiji la Zanzibar 2 230 893,169 71xxx Zanzibar
Unguja Kusini Koani 2 854 195,873 72xxx Zanzibar

Mikoa hiyo yote imegawanyika tena kwenye wilaya 169. Wilaya zimeganyika katika kata kibao.

Historia ya mikoa

Ugawaji wa nchi wakati wa ukoloni

Utawala wa Kijerumani

Wakati wa ukoloni wa Kijerumani eneo la Tanzania Bara (=Tanganyika) lilikuwa pamoja na Rwanda na Burundi kama Afrika ya Mashariki ya Kijerumani. Mwaka 1913 eneo lote liligawiwa kwa mikoa 21 na maeneo matatu ya wawakilishi wakazi. Mikoa 19 ilikuwa chini ya wakuu wa mkoa wa kawaida yaani maafisa raia Wajerumani (jer. Bezirksleiter au Bezirkamtsmann) waliyemwakilisha gavana na mikoa miwili ilikuwa chini ya mamlaka ya kijeshi yaani afisa wa jeshi la kikoloni la schutztruppe.

Mikoa ya kawaida ilikuwa:

Na.MkoaNa.Mkoa
1.Wilhelmstal (Lushoto)11.Langenburg (Tukuyu)
2.Tanga12.Bismarckburg (Kasanga)
3.Pangani13.Ujiji
4.Bagamoyo14.Tabora
5.Morogoro15.Dodoma
6.Dar es Salaam16.Kondoa-Irangi
7.Rufiji17.Moshi
8.Kilwa18.Arusha
9.Lindi19.Mwanza
10.Songea

Mikoa miwili ya Iringa na Mahenge ilikuwa "mikoa ya kijeshi" yaani chini ya usimamizi ya maafisa wakuu wa jeshi la Schutztruppe.

Maeneo ya Bukoba (takriban sawa na Mkoa wa Kagera wa leo), Ruanda na Urundi yaliendelea kutawaliwa na watawala wao wa kienyeji wakiangaliwa na mwakilishi mkazi wa Ujerumani aliyekuwa kama balozi, mshauri mkuu na msimamizi wa watawala hao.

Utawala wa Kiingereza

Tangu mwaka 1918/1919 eneo la Tanganyika lilikuwa eneo la kudhaminiwa kwa Uingereza bila maeneo ya Rwanda (Ruanda) na Burundi (Urundi). Tanganyika ikigawiwa mwaka 1922 kuwa na mikoa ileile ilhali majina ya Kijerumani yalibadilishwa kuwa majina ya kienyeji kama vile [2]:

Arusha, Bagamoyo, Bukoba, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa (si tena mkoa wa kijeshi), Kilwa, Kondoa-Irangi, Lindi, Mahenge (si tena mkoa wa kijeshi), Morogoro, Moshi, Mwanza, Pangani, Rufiji, Rungwe, Songea, Tabora, Tanga, Ufipa (badala ya Bismarckburg), Ujiji na Usambara (badala ya Wilhelmstal).

Katika miaka iliyofuata mfumo huo wa kiutawala ukabadilishwa. Mnamo mwaka 1948 Waingereza walikuwa na majimbo ("provinces") yafuatayo[3]:

Na. Jimbo Idadi ya wakazi
1. Central (Kati) 821,147
2. Eastern (Mashariki) 933,120
3. Lake (Ziwani) 1,853,719
4. Northern (Kaskazini) 592,300
5. Southern (Kusini) 917,648
6. Southern Highlands

(Nyanda za Juu za Kusini)

849,995
7. Tanga 557,245
8. Western (Magharibi) 952,503
Tanganyika yote 7,477,677

Mwaka 1961 Jimbo la Mashariki likagawiwa na Dar es Salaam kuwa jimbo la pekee. Ziwa Magharibi ikatengwa na Mkoa wa Ziwani.

Nyakati za uhuru

Majimbo hayo 10 yalirithiwa na nchi huru ya Tanganyika.

Tarehe 26 Aprili 1964 Tanganyika na Zanzibar zikaungana. Tanzania sasa ilikuwa na majimbo 12. Majimbo hayo yalibadilishwa mnamo 1966 kuwa mikoa 20.

Na.JimboIdadi ya WakaziEneo (km²)Makao makuuMikoa ya baadaye
1.Kati886,96294,301DodomaDodoma, Singida
2.Mashariki955,828107,630Dar es SalaamPwani (kisehemu), Morogoro
3.Dar es Salaam128,7421,393Dar es SalaamPwani (kisehemu)
4.Ziwani1,731,794107,711MwanzaMara, Mwanza, Shinyanga (kisehemu)
5.Ziwa Magharibi514,43128,388BukobaZiwa Magharibi
6.Kaskazini772,43485,374ArushaArusha, Kilimanjaro (kisehemu)
7.Kusini1,014,265143,027MtwaraMtwara, Ruvuma
8.Nyanda za Juu za Kusini1,030,269119,253MbeyaIringa, Mbeya (kisehemu)
9.Tanga688,29035,750TangaKilimanjaro (kisehemu), Tanga
10.Magharibi1,062,598203,068TaboraKigoma, Mbeya (kisehemu), Shinyanga (kisehemu), Tabora
11.Zanzibar165,2531,658ZanzibarZanzibar Shambani, Zanzibar Magharibi
12.Pemba133,858984Chake ChakePemba
Majimbo yote9,084,724928,537
  • Mwaka 1967 Zanzibar Shambani (Rural) ikagawiwa kuwa Zanzibar Shambani Kaskazini na Zanzibar Shambani Kusini. Mikoa hiyo iliitwa baadaye Kaskazini Zanzibar na Kusini Zanzibar.
  • 1971 Mkoa wa Rukwa ulianzishwa kutokana na maeneo ya Mbeya na Tabora.
  • 1972 Mkoa wa Lindi ukatengwa na Mtwara.
  • 1974 Mkoa wa Dar es Salaam ukatengwa na Mkoa wa Pwani
  • 1982 Mkoa wa Pemba ukagawiwa kuwa Kaskazini Pemba na Kusini Pemba
  • 1984 Jina la Mkoa wa Ziwa Magharibi likabadilishwa kuwa Mkoa wa Kagera
  • 2002 Mkoa wa Manyara ukatengwa na Arusha,
  • Mwaka 2012 mikoa minne mipya ilianzishwa ambayo ni
    • Mkoa wa Geita, kutoka maeneo ya mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Kagera
    • Mkoa wa Katavi, awali ilikuwa Wilaya ya Mpanda katika Mkoa wa Rukwa
    • Mkoa wa Njombe, kutoka maeneo ya Mkoa wa Iringa (wilaya za Ludewa, Makete na Njombe)
    • Mkoa wa Simiyu, kutoka maeneo ya mikoa ya Shinyanga (Bariadi, Meatu na Maswa) na Mwanza (Busega).
  • Mwaka 2016 ulianzishwa mkoa wa Songwe kwa kumega mkoa wa Mbeya upande wa magharibi.

Tazama pia

Marejeo

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-11-07. Iliwekwa mnamo 2022-11-07.
  2. http://www.statoids.com/utz.html
  3. http://www.statoids.com/utz.html
Tanzania

Makala hii imepangwa kwa mfululizo:
Siasa na serikali ya
Tanzania



Zanzibar

Nchi zingine · Atlasi

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu: