Nenda kwa yaliyomo

Vita ya Maji Maji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Vita vya Maji Maji)
Vita vya Maji Maji
Mchoro wa Mapambano ya Mahenge (1905) uliochorwa na Wilhelm Kuhnert (1927)
Sehemu ya Kinyang'anyiro cha Afrika
TareheJulai 1905Agosti 1907
MahaliAfrika Mashariki ya Ujerumani (sasa ni Tanzania)
MatokeoUshindi wa Ujerumani
Waasi / Pande Zilizopigana
Bendera ya Dola la Ujerumani German Empire
* Afrika Mashariki ya Ujerumani
Tariqa ya Qadiriyya
Kabila za Wamatumbi, Wangindo, Wangoni, Wayao na Watanganyika wengine
Makamanda na Viongozi
* G.A. von Götzen
* Kurt Johannes
* F. W. von Lindeiner-Wildau
* Kinjikitile Ngwale
* Nasr Khalfan
* Hemed Muhammad
Nguvu ya Vikosi
Takriban 2,000 Takriban 90,000
Hasara na Vifo
Wajerumani 15, Askari 73, na Ruga Ruga 316 Watu 75,000 – 300,000 (jumla ya waliofariki kwa njaa, magonjwa, na vita)
Wilhelm Kuhnert, Mapigano huko Mahenge mwaka 1905.

Vita ya Maji Maji ulikuwa upingaji mkali wa Waafrika dhidi ya utawala wa kikoloni wa Ujerumani katika maeneo ya kusini ya koloni la Afrika Mashariki ya Kijerumani. Vita hivyo vilishirikisha baadhi ya makabila ya kusini mwa Tanzania ya leo dhidi ya sera ya Kijerumani iliyoundwa kwa nguvu kuwalazimisha watu wa Tanganyika kulima zao la pamba. Vilidumu kuanzia mwaka 1905 hadi 1907.

Uasi wa Abushiri ibn Salim al-Harthi wa miaka ya 1888–1889 na Uasi wa Wahehe wa miaka ya 1891–1898 vinatazamwa na wanahistoria kama watangulizi wa vita vya Maji Maji.

Chanzo kikuu cha vita hii ni kwamba wanajamii walichoka kunyanyaswa na wakoloni. Baadhi ya manyanyaso hayo wakoloni waliwataka wanajamii kulima mazao ya kibiashara na walikatazwa kulima mazao ya chakula; kwa mantiki hiyo wanajamii walilima mazao ya biashara na kuacha kulima mazao ya chakula kwa lengo la kuwanufaisha wakoloni huku wao wakipata njaa kwa sababu ya kutolima mazao ya chakula kwa ajili ya kuwapatia chakula na huku adhabu kali ikitolewa kwa wale watakaopinga.

Kwa sababu hiyo wananchi walilazimika kufanya kazi huku wakilipwa mshahara mdogo au kutolipwa kabisa. Watu ambao hawakulazimika kufanya kazi ni watoto wadogo na wazee; kwa wale vijana wenye nguvu walifanyishwa kazi ngumu lakini kwa upande wa wasichana na mama wajawazito waliufanya kazi za ndani.

Moja ya changamoto walizozipata kwa upande wa vijana wa kiume ni kudhalilishwa kwa kupigwa mijeledi wakiwa uchi mbele ya wanawake wao na pia walitozwa pesa kubwa ukilinganisha na mshahara wanaopata ni kidogo: hizo ndizo baadhi ya changamoto walizozipata. Hivyo basi waliamua kukataa manyanyaso na masumbuko dhidi ya wakoloni.

Wahusika wakuu ni mtemi wa wanajamii Kinjekitile Ngwale na watemi wa Kijerumani.

Mtemi huyu wa kabila la Wangindo aliamini kwamba maji ndiyo silaha ya kipekee ambayo ingetumika kuwashinda wakoloni hata akawaambia wananchi wake kwamba wakoloni wakirusha silaha waseme "maji" kwa madai ya kuwa silaha itabadilika na kuwa maji.

Wanajamii wake waliamini kusikiliza, kwa hiyo basi vita ilipoanza wakoloni walipoanza kuwashambulia wanajamii walisema, "maji", lakini tunaona kwamba jinsi walivyokuwa wakisema "maji" ndivyo walivyozidi kushambuliwa.

Wanajamii wengi walipoteza maisha kwa hiyo nguvukazi ilipungua kwa kiwango kikubwa, lakini tunaangalia chanzo kikubwa kabisa ni kupinga manyanyaso.

Matokeo ya vita

[hariri | hariri chanzo]

Kukandamizwa kwa watu wa Maji Maji kubadilisha historia ya kusini mwa Tanzania. Makumi, au labda mamia ya maelfu ya watu walifariki au kulazimika kuyahama makazi yao. Baada ya vita hivyo, serikali ya kifalme ilianzisha mageuzi ya kiutawala chini ya ugavana wa Albrecht von Rechenberg.[1] Vita hivyo vilikuwa kitovu katika historia ya eneo hilo. Mwandishi wa habari John Gunther alibainisha mnamo mwaka 1953 kwamba "hata leo, Mkoa wa Kusini wa Tanganyika, 'Mkoa wa Cinderella,' haujapona kabisa kutokana na tishio la Wajerumani la nusu karne iliyopita. Uchumi wa eneo hili haujawahi kujengwa upya kikamilifu."[2] Baadaye, wazalendo wa Tanzania walitumia mfano huo kama ishara ya mwanzo wa utaifa wao, uzoefu wa kuunganisha uliowaleta pamoja watu wote tofauti wa Tanzania chini ya kiongozi mmoja, katika jaribio la kuanzisha taifa huru lisilokuwa na utawala wa kigeni.

Wanahistoria wa baadaye wamepinga mtazamo huo na kudai kuwa uasi huo hauwezi kuonekana kama vuguvugu lililoungana, bali kama mfululizo wa maasi yaliyofanywa kwa sababu mbalimbali, ikiwa ni pamoja na dini. Mchifu wa Kingoni walipewa ubatizo wa Kikristo kabla ya kunyongwa. Watu wengi katika eneo hilo wenyewe walichukulia uasi huo kama sehemu moja ya mfululizo mrefu wa vita vilivyoendelea tangu kabla ya kuwasili kwa Wajerumani katika eneo hilo. Wanataja muungano wa baadhi ya makundi na Wajerumani ili kuendeleza ajenda zao wenyewe.

Mchango wa Uislamu katika uasi huo ni mada inayojadiliwa. Katika tathmini ya hivi karibuni ya ushahidi, Jörg Haustein anahitimisha kuwa hoja kwamba Uislamu ulikuwa sababu "haijaungwa mkono na vyanzo vya kihistoria pamoja na taaluma iliyothibitishwa kuhusu Vita vya Maji Maji."[3]

John Iliffe anatafsiri uasi huo kama "vuguvugu la watu wengi [ambalo] lilianzia kwenye kero za wakulima, kisha likatakaswa na kuenezwa na dini ya kinabii, na hatimaye likasambaratika wakati shida ilipolazimisha kutegemea uaminifu wa msingi wa kijamii na kimbari"[4]. Patrick Redmond anaelezea uasi huo kama "idhihirisho la kuvutia zaidi la Tanzania la kukataa utawala wa kikoloni" lakini ambalo lilikuwa na "nafasi ndogo sana ya kufanikiwa."[5]

  1. Giblin, James Leonard; Monson, Jamie (2010). Maji Maji: Lifting the Fog of War. BRILL. p. 14. ISBN 978-90-04-18342-1.
  2. Gunther, John (1955). Inside Africa. Harper & Brothers. p. 411. ISBN 0836981979.
  3. Haustein, Jörg (2021). "Global Religious History as a Rhizome: Colonial Panics and Political Islam in German East Africa". Method and Theory in the Study of Religion. 33 (3–4): 321–344. doi:10.1163/15700682-12341520.
  4. Iliffe 1969, p. ?.
  5. Redmond, Patrick M. (1975). "Maji Maji in Ungoni: A Reappraisal of Existing Historiography". International Journal of African Historical Studies. 8 (3): 407–424. doi:10.2307/217152. JSTOR 217152.
  • Pugu Hadi Peramiho - kimehaririwa na P. Gerold Rupper, OSB, BPNP, Peramiho 1988, ISBN 9967 67 031 1