Bendera ya Tanzania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Tanzania.
Bendera ya Zanzibar baada ya mapinduzi mwaka 1964
iliyotangulia kuundwa kwa bendera ya Tanzania.
Bendera ya Jamhuri ya Tanganyika tangu mwaka 1961 hadi 1964 iliyotangulia kuundwa kwa bendera ya Tanzania.

Bendera ya Tanzania ni ya mstatili unaokatwa pembe kwa pembe na kanda nyeusi yenye milia za njano kandokando[1].

Pembetatu ya juu ina rangi ya majani, pembetatu ya chini ni ya buluu.

Matumizi ya bendera inahifadhiwa chini ya sheria ya "The National Flag and Coat of Arms Act, 15-1971"[2].

Historia ya bendera

Bendera hii imepatikana tangu 30 Juni 1964 kutokana na muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Bendera ya Tanganyika ilikuwa na rangi ya kijani ikiwa na kanda nyeusi katikati yenye milia za njano kando. Buluu imepatikana kutokana na bendera ya Zanzibar ya mwaka 1964 ikimaanisha bahari. Hata hivyo toka mwaka 2005, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ilianza kutumia rasmi bendera ya Zanzibar. Hii ni mara ya kwanza toka kuungana kwa Tanganyika na Zanzibar kwa funguvisiwa la Zanzibar kuwa na bendera yake lenyewe.

Maana ya rangi

Rangi zinasemekana kuwa na maana zifuatazo:

Bendera za kihistoria tangu zamani za ukoloni

Flag Duration Use Description
1856–1963 Bendera ya Usultani wa Zanzibar Kitambaa chekundu
1888–1890 Bendera ya Kampuni ya Kijerumani kwa Afrika ya Mashariki Nyeupe, msalaba mweusi, nyota za Salibu
1893-1919 Bendera ya Mamlaka ya Koloni za Ujerumani Nyeusi-nyeupe – nyekundu kama Dola la Ujerumani, pamoja na ishara ya tai, ilitumiwa katika koloni zote za Ujerumani
1919–1961 Ramani ya eneo la kudhaminiwa Tanganyika Bendera nyekundu yenye rangi za Uingereza kwenye kona na ishara ya twiga
1961–1964 Bendera ya Tanganyika Kijani yenye kanda nyeusi katikati linaloshikwa na milia ya njano-dhahabu
1963–1964 Bendera ya Usultani wa Zanzibar baada ya uhuru Nyekundu, yenye duara ya kibichi inayoonyesha karafuu mbili za rangi ya njano
Januari–Aprili 1964 Bendera ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar hadi maungano Kanda za buluu, nyeusi na kijani.

Marejeo

  1. National Flag Archived 27 Septemba 2018 at the Wayback Machine., tovuti rasmi ya serikali ya Tanzania, iliangaliwa Desemba 2018
  2. Act to prescribe the National Flag and Coat of arms.. Archived 27 Oktoba 2021 at the Wayback Machine., tovuti ya serikali ya Tanzania, iliangaliwa Desemba 2020
  3. http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Serikali-yatoa-maelekezo-matumizi--rangi-ya-bendera/1597296-4893496-f15slnz/index.html
  4. National Flag, "colour specifications", tovuti rasmi ya serikali ya Tanzania
  5. http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Magufuli-afuta-maelekezo-mapya-matumizi-ya-bendera/1597296-4895796-15gjsv1z/index.html