Bunge la Tanzania
Bunge la Tanzania ni baraza la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalotunga sheria na kuisimamia serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.
Waliopo bungeni[hariri | hariri chanzo]
Bunge linamjumuisha rais wa Tanzania pamoja na wabunge. Mnamo mwaka 2017 kulikuwa na wabunge 393[1] wanaoingia kwa namna tofauti [2]
- Wabunge 264 waliochaguliwa katika majimbo ya uchaguzi
- Wabunge 113 walioingia kupitia viti maalumu kwa wanawake
- Wabunge 5 walioteuliwa na Baraza la Wawakilishi wa Zanzibar
- Wabunge 10 walioteuliwa na Rais wa Tanzania
- Mwanasheria Mkuu
Mamlaka ya Bunge iko juu ya mambo yote yasiyo ya Zanzibar pekee.
Majimbo ya Uchaguzi wa Bunge[hariri | hariri chanzo]
Kuna majimbo 214 Tanzania Bara na majimbo 50 Zanzibar.
Majimbo yanatofautiana kwa kiasi kikubwa katika idadi ya wakazi. Wastani wa Tanzania bara ni mbunge mmoja kwa wakazi 227,461. [3] Kuna majimbo katika mikoa ambako mbunge mmoja anawakilisha watu wengi zaidi kama vile Dar es Salaam (wakazi 546,542/mbunge 1), Mwanza (346,999) na Kagera (309,953). Kinyume chake kuna majimbo mengine ambako mbunge anawakilisha watu wachache kama vile Pwani (wakazi 133.104/mbunge), Katavi (128.513), Njombe (120.795) au Lindi (112.192).
Tofauti ni kubwa zaidi huko Zanzibar. Kwa mfano Wilaya ya Kaskazini B katika Mkoa wa Unguja Kaskazini ina wakazi 81,675[4] pekee lakini inachagua wabunge 4 katika majimbo ya Bumbwini, Donge, Kiwengwa na Mahonda.
Kamati za Bunge[hariri | hariri chanzo]
Bunge linatekeleza kazi yake kwa kiasi kikubwa kupitia kamati mbalimbali. Kuna aina tofauti za kama kama vile:
Kamati za kudumu zinazohusu uendeshaji wa Bunge:
- Kamati ya Uongozi;
- Kamati ya Kanuni za Bunge
- Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
Kamati za kudumu za Bunge za Kisekta
- Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira
- Kamati ya Katiba na Sheria
- Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama;
- Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa;
- Kamati ya Huduma na Maendeleo ya Jamii
- Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii;
- Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji;
- Kamati ya Miundombinu;
- Kamati ya Nishati na Madini.
Kamati za Sekta Mtambuka:
- Kamati ya Bajeti
- Kamati ya Masuala ya UKIMWI;
- Kamati ya Sheria Ndogo;
- Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma.
Kamati za kudumu za Bunge zinazosimamia matumizi ya fedha za Umma:
- Kamati ya Hesabu za Serikali (Public Accounts Committee PAC)
- Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)
Tazama pia[hariri | hariri chanzo]
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
- ↑ Structure of parliament, tovuti ya bunge, ilitazamiwa Mei 2017
- ↑ Katiba ya Tanzania Archived Mei 16, 2017 at the Wayback Machine., ibara 66, uk. 51
- ↑ Linganisha takwimu hii, hasa Jedwali 1 uk. 2: Makadirio ya idadi ya watu katika majimbo ya uchaguzi Tanzania Bara kwa mwaka 2016; tovuti ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu, iliangaliwa Juni 2017. Wastani unapatikana kwa kugawa idadi ya wakazi jumla kwa idadi ya majimbo
- ↑ Sensa ya 2012, Kaskazini Unguja uk. 226