Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
4°24′ S 15°24′ E
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (au Kongo-Kinshasa) ni nchi iliyoko Afrika ya Kati; kwa ukubwa wa eneo ni ya pili barani Afrika. Ni tofauti na nchi jirani ya Jamhuri ya Kongo.

Ramani ya Jamhuri.

Jiografia

Nchi imepakana na Jamhuri ya Kongo, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Sudan Kusini, Uganda, Rwanda, Burundi, Tanzania, Zambia na Angola.

Ina sehemu ndogo ya pwani kwenye Bahari ya Atlantiki. Sehemu hiyo inatenganisha eneo la Cabinda kutoka maeneo mengine ya Jamhuri ya Angola.

Eneo lote ni la kilometa mraba 2,345,409 na linafanya Kongo iwe nchi ya 11 duniani kwa ukubwa wa eneo.

Historia

Historia ya kale

Ufalme wa Kongo mnamo mwaka 1700

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani na ya Wabilikimo.

Katika karne za BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.

Jina la Kongo lahusiana na mto Kongo unaopitia nchi yote.

Mnamo karne ya 15, wakati wapelelezi wa kwanza Wareno walipofika kwenye pwani za Afrika, milki kubwa katika nchi ya Kongo ya magharibi pamoja na Angola ya kaskazini ilikuwa Ufalme wa Kongo. Wakati wa uenezaji mkuu ufalme huu ulianza kwenye mwambao wa Atlantiki na kuendelea hadi mto Kwango kwenye mashariki, halafu maeneo kutoka Pointe-Noire (leo: Jamhuri ya Kongo, upande wa kaskazini ya Cabinda) upande wa kaskazini hadi mto Loje (leo: mji wa Ambriz) katika kusini.

Mtawala alikuwa na cheo cha Manikongo na ufalme uligawiwa kwa majimbo sita. Baada ya kufika kwa Wareno wafalme na matabaka ya juu walikuwa Wakristo. Ufalme uliporomoka kutokana na vita vilivyosababishwa na biashara ya watumwa na kuingilia kwa wafanyabiashara ya watumwa katika siasa ya ndani. Hata hivyo, nasaba za watawala waliotumia cheo cha "Awenekongo" waliendelea kukaa katika mji mkuu wa kale M'banza-Kongo (iliyobadilishwa jina kuitwa San Salvador) hadi mwaka 1914 ambako Wareno walifuta mabaki ya uhuru na kufanya eneo lililobaki sehemu kamili ya koloni lao la Angola.

Upande wa kusini, kuanzia karne ya 17, kulikuwa na ufalme ulioitwa Dola la Kazembe.

Koloni binafsi la mfalme kuwa koloni la Ubelgiji

Picha za watoto waliokatwa mikono kama adhabu chini ya Leopold II zilienea na kusababisha madai ya kumwondolea utawala wa Kongo.

Nchi jinsi ilivyo ilianzishwa kama Dola huru la Kongo likiwa mali binafsi ya mfalme Leopold II wa Ubelgiji. Historia yake ni ya aibu na ya ukatili kupindukia.

Utawala wa mfalme ulionekana kuwa wa kinyama na upinzani dhidi yake ulikua katika nchi nyingi za dunia.

Hatimaye alipaswa kukabidhi koloni lake binafsi mikononi mwa serikali ya Ubelgiji iliyomlipa fidia kwa mali aliyoacha.

Kati ya mwaka 1908 hadi 1960 ilikuwa koloni la Ubelgiji kwa jina la Kongo ya Kibelgiji baada ya kuhamishiwa mikononi mwa serikali ya Ubelgiji.

Katika miaka 1925 hadi 1946 maeneo ya Rwanda na Burundi yalitawaliwa kama sehemu za Kongo ya Kibelgiji.

Siasa ya wakoloni

Wabelgiji walijitahidi kuboresha hali ya maisha ya wenyeji baada ya miaka mibaya ya Leopold II. Nia ilichelewa kuonekana hali halisi kwa sababu utaratibu wa kulazimisha Waafrika kufanyia kazi kampuni na shirika kubwa iliendelea hata bila idhini ya serikali mpya ukadai vifo vingi.

Kwenye uwanja wa elimu, matibabu na mawasiliano jitihada za siasa mpya zilionekana zaidi. Kongo ilikuwa kati ya nchi chache ambako lugha za kienyeji zilifundishwa shuleni kwa sababu shule nyingi ziliendshwa na wamisionari.

Kwa upande mwingine ubaguzi wa rangi uliwaruhusu Waafrika wachache sana kufikia ngazi za juu za elimu.

Makampuni makubwa ya migodi kama vile "Société Générale" na "Union Minière du Haut Katanga" yalichimba madini hasa katika jimbo la Katanga. Makampuni haya yalikuwa na athira kubwa.

Katanga ilikuwa maarufu kwa shaba iliyochimbwa huko. halafu pia kwa uranium iliyotumiwa kwa mabomu ya kwanza ya kinyuklia ya Marekani mwaka 1945.

Upinzani

Baada ya unyama wa miaka ya Leopold II upinzani dhidi ya utawala wa kikoloni ulikuwa hafifu. Kuanzia miaka ya 1920 Wakongo wengi walionyesha upinzani huo katika mahudhurio katika madhehebu mapya ya wafuasi wa Simon Kimbangu yaliyopigwa marufuku na Wabelgiji kuanzia mwaka 1926.

Tangu mwaka 1950 upinzani uliongezeka na kuonyesha pia uso wa kisiasa.

Wabelgiji ambao hawakujiandaa kwa madai hayo yalipaswa kukubali uchaguzi wa halmashauri za vijiji na miji mwaka 1957.

Mwaka 1958 vyama vya kisiasa vilikubaliwa. Harakati mbili muhimu kati ya hivi zilikuwa Abako (Alliance de Bakongo) chini ya Joseph Kasavubu na MNC (Mouvement National Congolais) chini ya Patrice Lumumba.

Mwaka 1959 mkutano wa wanasiasa Wakongo ulidai uhuru wa nchi.

Mwisho wa koloni na uhuru

Wabelgiji walijaribu kuchelewesha harakati hizo lakini baada ya kutambua matatizo serikali ya Ubelgiji ilitangaza mnamo Januari 1960 kuwa uchaguzi utaendeshwa haraka na baada ya miezi sita Wabelgiji watakabidhi nchi kwa wenyeji.

Chama cha Patrice Lumumba kilishinda kwa kura nyingi naye akawa kiongozi wa kwanza wa nchi huru kama waziri mkuu.

Koloni la Kongo ya Kibelgiji lilipata uhuru tarehe 30 Juni 1960.

Kati ya 27 Oktoba 1971 na 17 Mei 1997, chini ya utawala wa dikteta Mobutu, nchi ilijulikana kwa jina la "Zaire".

Leo hii ni Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mikoa

Mikoa 25 na mji mkuu Kinshasa.


Nchi imegawiwa katika mikoa 26 kadiri ya Katiba mpya (2006) na utekelezaji wake wa mwaka 2015.

Mkoa Mji Mkuu
1. Kinshasa Kinshasa
2. Kongo Kati   Matadi
3. Kwango Kenge
4. Kwilu Kikwit
5. Mai-Ndombe Inongo
6. Kasaï Luebo
7. Lulua Kananga
8. Kasaï Mashariki Mbuji-Mayi
9. Lomami Kabinda
10. Sankuru Lodja
11. Maniema Kindu
12. Kivu Kusini Bukavu
13. Kivu Kaskazini Goma
Mkoa Mji Mkuu
14. Ituri Bunia
15. Wele Juu Isiro
16. Tshopo Kisangani
17. Wele Chini Buta
18. Ubangi Kaskazini Gbadolite
19. Mongala Lisala
20. Ubangi Kusini Gemena
21. Équateur Mbandaka
22. Tshuapa Boende
23. Tanganyika Kalemie
24. Lomami Juu Kamina
25. Lualaba Kolwezi
26. Katanga Juu    Lubumbashi

Watu

Mwaka 2017 wakazi walikuwa 81,339,988: idadi hiyo ni ya 4 kati ya nchi zote za Afrika, baada ya Nigeria, Ethiopia na Misri.

Wakazi asilia ni Wabilikimo, ambao kwa sasa ni 600,000. Kumbe walio wengi ni Wabantu.

Lugha

Maeneo ya lugha kuu za Kongo

Kifaransa ni lugha rasmi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ilikuwa lugha ya utawala ya koloni ikaendelea kutumiwa kama lugha isiyoelekea upande wowote kati ya makabila, lugha na tamaduni za nchi hii.

Lugha ya Kiholanzi iliyotumiwa na Wabelgiji pamoja na Kifaransa katika utawala haitumiki tena.

Kwa jumla kuna takriban lugha 242, hasa lugha za Kibantu, zinazozungumzwa nchini (angalia orodha ya lugha). Kati yake, lugha 4 zinatambuliwa kama lugha za kitaifa, nazo ni: Kikongo (Kituba), Kingala (Kongo), Kiluba (Tshiluba) na Kiswahili. Wakati wa ukoloni lugha hizo nne za kitaifa ziliwahi kutumiwa kieneo katika shule za msingi.

Kingala kilikuwa lugha rasmi ya jeshi la kikoloni lililoitwa "Force Publique" chini ya utawala wa Ubelgiji likaendelea kuwa lugha ya jeshi la jamhuri baada ya uhuru.

Tangu mapinduzi ya 1997 sehemu za jeshi, hasa mashariki, hutumia pia Kiswahili.

Takriban 47% wanatumia Kifaransa kama lugha ya kwanza au lugha ya pili.

Dini

Wananchi wengi (zaidi ya 90%) wanajihesabu Wakristo wa madhehebu mbalimbali; kati yao asilimia 29.7 ni Wakatoliki. Waislamu ni asilimia 10-12. Wafuasi wa dini asilia za Kiafrika ni 3%.

Tazama pia

Marejeo

  • Clark, John F., The African Stakes of the Congo War, 2004.
  • Devlin, Larry (2007). Chief of Station, Congo: A Memoir of 1960–67. New York: PublicAffairs. ISBN 978-1-58648-405-7. .
  • Drummond, Bill and Manning, Mark, The Wild Highway, 2005.
  • Edgerton, Robert, The Troubled Heart of Africa: A History of the Congo. St. Martin's Press, December 2002.
  • Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. The Dark Side of Globalization. The Vicious Cycle of Exploitation from World Market Integration: Lesson from the Congo, Working Papers in Economics and Statistics 31, University Innsbruck 2007.
  • Exenberger, Andreas/Hartmann, Simon. Doomed to Disaster? Long-term Trajectories of Exploitation in the Congo Archived 1 Septemba 2011 at the Wayback Machine., Paper to be presented at the Workshop "Colonial Extraction in the Netherlands Indies and Belgian Congo: Institutions, Institutional Change and Long Term Consequences", Utrecht 3–4 December 2010.
  • Gondola, Ch. Didier, "The History of Congo", Westport: Greenwood Press, 2002.
  • Joris, Lieve, translated by Waters, Liz, The Rebels' Hour, Atlantic, 2008.
  • Justenhoven, Heinz-Gerhard; Ehrhart, Hans Georg. Intervention im Kongo: eine kritische Analyse der Befriedungspolitik von UN und EU. Stuttgart: Kohlhammer, 2008. (In German) ISBN 978-3-17-020781-3.
  • Kingsolver, Barbara. The Poisonwood Bible HarperCollins, 1998.
  • Larémont, Ricardo René, ed. 2005. Borders, nationalism and the African state. Boulder, Colorado and London: Lynne Rienner Publishers.
  • Lemarchand, Reni and Hamilton, Lee; Burundi: Ethnic Conflict and Genocide. Woodrow Wilson Center Press, 1994.
  • Mealer, Bryan: "All Things Must Fight To Live", 2008. ISBN 1-59691-345-2.
  • Melvern, Linda, Conspiracy to Murder: The Rwandan Genocide and the International Community. Verso, 2004.
  • Miller, Eric: "The Inability of Peacekeeping to Address the Security Dilemma", 2010. ISBN 978-3-8383-4027-2.
  • Mwakikagile, Godfrey, Nyerere and Africa: End of an Era, Third Edition, New Africa Press, 2006, "Chapter Six: Congo in The Sixties: The Bleeding Heart of Africa", pp. 147 – 205, ISBN 978-0-9802534-1-2; Mwakikagile, Godfrey, Africa and America in The Sixties: A Decade That Changed The Nation and The Destiny of A Continent, First Edition, New Africa Press, 2006, ISBN 978-0-9802534-2-9.
  • Nzongola-Ntalaja, Georges, The Congo from Leopold to Kabila: A People's History, 2002.
  • O'Hanlon, Redmond, Congo Journey, 1996.
  • O'Hanlon, Redmond, No Mercy: A Journey into the Heart of the Congo, 1998.
  • Prunier, Gérard, Africa's World War: Congo, the Rwandan Genocide, and the Making of a Continental Catastrophe, 2011 (also published as From Genocide to Continental War: The Congolese Conflict and the Crisis of Contemporary Africa: The Congo Conflict and the Crisis of Contemporary Africa).
  • Renton, David; Seddon, David; Zeilig, Leo. The Congo: Plunder and Resistance, 2007. ISBN 978-1-84277-485-4.
  • Reyntjens, Filip, The Great African War: Congo and Regional Geopolitics, 1996–2006 , 2009.
  • Rorison, Sean, Bradt Travel Guide: Congo  — Democratic Republic/Republic, 2008.
  • Schulz, Manfred. Entwicklungsträger in der DR Kongo: Entwicklungen in Politik, Wirtschaft, Religion, Zivilgesellschaft und Kultur, Berlin: Lit, 2008, (in German) ISBN 978-3-8258-0425-1.
  • Stearns, Jason: Dancing in the Glory of Monsters: the Collapse of the Congo and the Great War of Africa, Public Affairs, 2011.
  • Tayler, Jeffrey, Facing the Congo, 2001.
  • Turner, Thomas, The Congo Wars: Conflict, Myth and Reality, 2007.
  • Van Reybrouck, David, Congo: The Epic History of a People, 2014
  • Wrong, Michela, In the Footsteps of Mr. Kurtz: Living on the Brink of Disaster in Mobutu's Congo.
  • Osman, Mohamed Omer Guudle(November,2011) Africa: A rich Continent where poorest people live, The Case of DR Congo and the exploitation of the World Market

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.