Jibuti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Jibuti (Kiswahili)
Jamhuuriyadda Jabuuti (Kisomali)
Gabuutih Ummuuno (Kiafar)
Bendera ya Jibuti Nembo ya Jibuti
(Bendera ya Jibuti) (Nembo ya Jibuti)
Lugha rasmi Kifaransa
Mji Mkuu Jibuti
Mji Mkubwa Jibuti
Serikali Jamhuri
Rais Ismaïl Omar Guelleh
Eneo km² 23,200
Idadi ya wakazi 957,273 (2022)
Wakazi kwa km² 37.2
Uchumi nominal Bilioni $2.187
Uchumi kwa kipimo cha umma $2,084
Pesa CFA frank (XFA) (Frank ya Afrika ya Kati)
Kaulimbiu "Inkittiino, Qeedala, Wagar" (Umoja, Usawa, Amani)
Wimbo wa Taifa Jibuti
Jibuti katika Afrika
Saa za Eneo UTC +3 (Wakati wa Afrika Mashariki)
Mtandao .dj
Kodi ya Simu +253

Jibuti (kwa Kifaransa: Djibouti, kwa Kiarabu: جيبوتي) ni nchi ndogo ya Afrika ya Mashariki kwenye Pembe la Afrika.

Imepakana na Eritrea, Ethiopia na Somalia upande wa bara. Kuna pwani ya Bahari ya Shamu na Ghuba ya Aden. Ng'ambo ya bahari iko nchi ya Yemen katika umbali wa km 20 pekee.

Jina la nchi linatokana na lile la mji mkuu, Jibuti.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Hali ya nchi inalingana kwa karibu na ile ya mataifa mengine katika Mashariki mwa Afrika, Jibuti ilipo, ikipakana na Ghuba ya Aden na Bahari ya Shamu, katikati ya Eritrea, Ethiopia na Somalia.

Eneo[hariri | hariri chanzo]

Kwa kilomita 13 Jibuti inapakana na Eritrea, huku kukiwa na urefu wa kilomita 337 za mpaka kati ya Jibuti na Ethiopia, na mpaka wa km 58 na Somalia. Kwa jumla ina mpaka wa km 506. Pia ina pwani ya urefu wa km 314.

Jibuti inakaa kaika eneo la kufana, ikiwa karibu na leni zenye shughuli nyingi zaidi duniani la meli na pia karibu na mahali pa uchimbaji mafuta nchini Saudi Arabia.

Jibuti pia ni kituo cha reli ya Ethiopia-Jibuti.

Hali ya hewa[hariri | hariri chanzo]

Hali yake ya hewa ni ya joto kiasi, na pia haina mvua (ni jangwa).

Miinuko[hariri | hariri chanzo]

Milima iliyopo katikati ya nchi hugawa tambarare za pwani kutoka plateau. Eneo la chini zaidi ni Ziwa Assal mita 155 chini ya usawa wa bahari na la juu zaidi ni volikano Moussa Ali yenye kimo cha mita 2028. Hakuna shamba la ukulima, unyunyizaji maji, mimea iliyojimeza huko (msitu upo tu katika milima ya Goda, hasa mbuga ya Day Forest). Takribani asilimia 9 ya nchi ni malisho yeliyojimeza (1993 mashariki). Kwa hiyo Jibuti inahesabiwa kuwa sehemu ya nyasi ya Ethiopia, isipokuwa kijisehemu kinachopakana na Bahari ya Shamu ambacho ni baadhi ya Jangwa la Pwani ya Eritrea ambayo inajulikana kuwa njia nzuri ya uhamiaji wa ndege ambao wanaweza kuwindwa[1].

Mazingira[hariri | hariri chanzo]

Matukio ya kimaumbile ni pamoja na Matetemeko ya ardhi, kiangazi, mawimbi kutoka Bahari ya Hindi ambayo husababisha mafuriko na mvua kubwa. Malighafi ni pamoja na umeme kutoka ardhini (geothermal energy). Eneo hili limekumbwa na uhaba wa maji salama ya kunywa na pia kugeuka kwa eneo hilo kuwa jangwa.

Jibuti ni mwanachama wa makubaliano ya kimataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, ueneaji wa jangwa, viumbehai vilivyo hatarini, sheria ya bahari, kulinda ukanda wa ozoni na uharibifu wa mazingira na meli.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Nchi ilikuwa koloni la Ufaransa kwa jina la Somalia ya Kifaransa, halafu (1967) Eneo la Kifaransa la Waafar na la Waisa, kutokana na majina ya makabila mawili makubwa zaidi ya eneo hilo.

Sababu ya kuanzishwa kwa koloni ilikuwa nia ya Ufaransa ya kuwa na bandari ya mji wa Jibuti karibu na Bab el Mandeb inayotawala mawasiliano kati ya Bahari Hindi na Bahari ya Shamu kuelekea Mfereji wa Suez.

Nchi ilipata uhuru tarehe 27 Juni 1977.

Hadi leo umuhimu na uchumi wake unategemea bandari, ambapo zinapitia asilimia 95 za bidhaa zinazoingizwa Ethiopia. Nchi hiyo imeunganishwa na Jibuti kwa reli, moja ya zamani, na nyingine mpya iliyokamilika mwaka 2016.

Ramani ya Jibuti

Watu[hariri | hariri chanzo]

Siku hizi wakazi wengi (60%) ni Wasomali, hasa wa kabila la Waisa, halafu Waafar (35%). Asilimia 5 zilizobaki ni Waarabu, Waethiopia na Wazungu (hasa Wafaransa na Waitalia).

Lugha rasmi ni Kifaransa na Kiarabu. Kisomali na Kiafar ni lugha za taifa.

Upande wa dini, Uislamu unafuatwa na 94% za wakazi na ndio dini rasmi pekee. Asilimia 6 wanafuata Ukristo katika madhehebu mbalimbali, hasa Waorthodoksi wa Mashariki kutoka Ethiopia (3.2%), halafu Wakatoliki (1.4%) na Waprotestanti (chini ya 1%).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Ismaaciil Cumar Geelle.
Bunge.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla
Mengineyo


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Jibuti kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. http://www.worldwildlife.org/wildworld/profiles/terrestrial/at/at1304_full.html