Pembe ya Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Pembe la Afrika)
Pembe ya Afrika ikitazamwa kutoka Space Shuttle ya NASA mnamo Mei 1993. Sehemu kubwa inaonekana ni nusu jangwa.
Picha nyingine ya NASA.
Mataifa ya pembe ya Afrika

Pembe ya Afrika ni jina la sehemu ya mashariki kabisa ya bara la Afrika yenye umbo la pembetatu; ni kama rasi iliyoko kati ya Ghuba ya Aden na Bahari Hindi yenyewe.

Eneo hili linajumuisha nchi za leo za Somalia na Jibuti pamoja na sehemu ya mashariki ya Ethiopia; wakati mwingine Ethiopia yote pamoja na Eritrea huhesabiwa humo. Kwa kutumia wazo la pembe ya Afrika kubwa kuna eneo la km² 1,882,757 linalokaliwa na wakazi milioni 122.6, hasa wa Ethiopia.

Nchani mwa pembe iko Puntland iliyotangaza uhuru wake lakini inahesabiwa na mataifa mengi kama sehemu ya Somalia, jirani yake ni Somaliland ambayo ni pia sehemu ya Somalia iliyotangaza uhuru wake.

Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Pembe ya Afrika kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.