Guinea Bisau

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Guinea Bisau


Map of Guinea-Bisau
Map of Guinea-Bisau

Guinea-Bisau (pia: Ginebisau) ni nchi ndogo katika Afrika ya Magharibi.

Iko mwambaoni kwa Bahari Atlantiki ikipakana na Senegal upande wa kaskazini na Guinea upande wa kusini.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Guinea-Bisau ni kati ya nchi ndogo sana za Afrika ikiwa na eneo la kilomita mraba 36,125; takriban 22% ni visiwa na bahari. Sehemu ya bara ni tambarare. Funguvisiwa la Bissagos lenye visiwa 77 liko karibu na pwani.

Miji[hariri | hariri chanzo]

Miji mikubwa zaidi ya Guinea Bisau ni: Bisau (wakazi 492,004), Gabú (wakazi 48,670), Bafatá (wakazi 37,875), Bissorã (wakazi 29,468), Bolama (wakazi 16,216) na Cacheu (14,320).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Zamani ilikuwa koloni la Ureno kwa jina la Guinea ya Kireno.

Baada ya uhuru (1973/1974) jina la mji mkuu wake lilishika nafasi ya nchi tawala kuwa Guinea-Bisau kwa kusudi la kuitofautisha na nchi jirani ya Guinea na ile ya Guinea ya Ikweta.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi walikuwa 1,515,000 mwaka 2010, wakati walikuwa 518,000 tu mwaka 1950.

Makabila[hariri | hariri chanzo]

Waafrika ni 99%: makabila makubwa ni Wabalanta 30%, Wafulbe 30%, Wamanjaca 14%, Wamandinka 13%, Wapapel 7%). Wazungu na machotara ni chini ya 1%.

Lugha[hariri | hariri chanzo]

Pamoja na lugha asilia, 32.1% za wakazi wanasema Kireno ambacho ndicho lugha rasmi na 90.4% wanatumia Krioli maalumu ya Kireno ambayo ni kama lugha ya taifa inayounganisha makabila. Lugha nyingine za kigeni zinazotumika ni Kifaransa (7%), Kiingereza (2.9%) na Kihispania (0.5%)

Dini[hariri | hariri chanzo]

Takriban 46.1% ni Waislamu (hasa Wasuni), 30.6% wafuasi wa dini asilia za Kiafrika, 18.9 % Wakristo (hasa Wakatoliki).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Abdel Malek, K.,"Le processus d'accès à l'indépendance de la Guinée-Bissau.",In : Bulletin de l'Association des Anciens Elèves de l'Institut National de Langues et de Cultures Orientales, N°1, Avril 1998. – pp. 53–60
  • Forrest, Joshua B., Lineages of State Fragility. Rural Civil Society in Guinea-Bissau (Ohio University Press/James Currey Ltd., 2003)
  • Galli, Rosemary E, Guinea Bissau: Politics, Economics and Society, (Pinter Pub Ltd, 1987)
  • Lobban, Jr., Richard Andrew and Mendy, Peter Karibe, Historical Dictionary of the Republic of Guinea-Bissau, third edition (Scarecrow Press, 1997)
  • Vigh, Henrik, Navigating Terrains of War: Youth And Soldiering in Guinea-Bissau, (Berghahn Books, 2006)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Biashara
Habari
Afya
Jiografia


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guinea Bisau kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.