Japani
Japani 日本国 Nihon-koku au Nippon-koku (Kijapani) | |
---|---|
Wimbo wa taifa: 君が代 Kimigayo ("Utawala wa Mtukufu wa Kifalme") | |
Mji mkuu na mkubwa | Tokyo |
Lugha rasmi | Kijapani |
Lugha ya taifa | Ainu (inayotambuliwa), Kiryukyuan, Hachijō (hazijatambuliwa) |
• Mfalme | Naruhito |
• Waziri Mkuu | Shigeru Ishiba |
Historia | |
• Katiba ya Meiji | 29 Novemba 1890 |
• Katiba ya sasa | 3 Mei 1947 |
Eneo | |
• Jumla | km2 377,975 (ya 62) |
• Maji (asilimia) | 1.4% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2025 | 123,400,000 |
• Msongamano | 330/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ▲ $6.741 trilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $54,678 |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ![]() |
• Kwa kila mtu | ![]() |
HDI (2023) | ▲ 0.925 juu |
Gini (2018) | 33.4 |
Sarafu | Yen ya Kijapani (¥) |
Majira ya saa | UTCUTC+09:00 (JST) |
Upande wa magari | Kushoto |
Msimbo wa simu | +81 |
Jina la kikoa | .jp |
Japani, ni nchi ya visiwa katika Asia ya Mashariki, iliyoko kwenye Bahari ya Pasifiki. Inapakana kwa maji na China, Korea Kusini, Korea Kaskazini, na Urusi. Ina idadi ya watu takriban milioni 123, ikiwa ya 11 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Tokyo, moja ya miji yenye watu wengi zaidi duniani. Japani imegawanyika katika mikoa 47, Inajulikana kwa teknolojia yake ya hali ya juu, utamaduni wake wa kale na wa kisasa kama anime na samurai, pamoja na miundombinu ya kisasa kama treni za mwendo kasi (Shinkansen).
Japani ni mojawapo ya nchi zilizoendelea zaidi kiuchumi duniani, ikiwa na mojawapo ya pato la taifa kubwa zaidi kwa viwango vya kimataifa. Uchumi wake unaegemea hasa katika viwanda vya teknolojia ya hali ya juu, magari, vifaa vya kielektroniki, na roboti. Makampuni makubwa kama Toyota, Sony, na Panasonic yanatoka Japani na yana ushawishi mkubwa duniani. Licha ya rasilimali chache za asili, Japani imefanikiwa kukuza uchumi wake kupitia ubunifu, elimu ya juu, na nidhamu ya kazi miongoni mwa wananchi wake.
Katika historia, Japani iliwahi kuwa milki ya kifalme iliyojitenga na mataifa ya nje kwa karne nyingi, hadi ilipofunguka kwa dunia wakati wa kipindi cha Meiji mnamo karne ya 19. Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia, ambapo ilishambuliwa vikali ikiwemo mabomu ya atomiki mjini Hiroshima na Nagasaki, Japani ilijengwa upya na kuwa taifa la kidemokrasia. Leo, ni mwanachama wa mashirika makubwa kama Umoja wa Mataifa, G7, na G20, na ina ushawishi mkubwa katika siasa, uchumi, na utamaduni wa kimataifa.
Jiografia
Japani ni funguvisiwa lenye visiwa 14,125 mbele ya pwani ya Uchina, Korea na Urusi (Siberia).
Visiwa vikubwa na muhimu zaidi ni vinne tu; ndivyo Honshu, Hokkaido, Shikoku na Kyushu. Safu ya milima inapita visiwa vyote vikubwa na kusababisha msongamano mkubwa wa wakazi katika miji kutokana na uhaba wa ardhi ya kukalia. Hali halisi Japani yote ni safu ya milima tu inayopanda juu kutoka sakafu ya bahari na vilele vya milima yake huonekana juu ya uso wa bahari kama visiwa vikubwa au vidogo.
Kijiolojia eneo hili liko kwenye mstari ambako mabamba ya gandunia ya Ulaya-Asia, Pasifiki na Ufilipino hukutana. Hii ni sababu ya kuwepo kwa volkeno 240 katika Japani na takriban 40 kati ya hizo ni hai pia kutokea kwa matetemeko ya ardhi ya mara kwa mara. Hivyo Japani ni sehemu ya pete ya moto ya Pasifiki inayozunguka bamba la Pasifiki.
Japani inapatwa kila mwaka na dhoruba kali aina ya taifuni. Hata tsunami (ni neno la Kijapani) ni kawaida. Nchi inajikinga na mitambo mengi ya kutoa taarifa ya tsunami kuanza pia mitambo ya kufunga milango ya mabandari.

Miji
Wajapani wengi hukalia sehemu ndogo ya 10% za nchi. Kuna miji kumi yenye wakazi zaidi ya milioni moja. Miji mikubwa ni Tokyo, Yokohama, Nagoya, Osaka, Kyoto, Kobe, Hiroshima, Fukuoka, Kitakyushu, Sendai na Sapporo. Usafiri ndani ya Japani ni hasa kwa treni, mabasi na ndege. Treni ya Shinkansen visiwani Honshu na Kyushu ni kati ya treni zenye mkasi mkubwa duniani.
Mikoa

Japan ina mikoa arubaini na saba. Kila mkoa unasimamiwa na gavana mmoja, bunge na urasimu utawala. Kila mkoa umegawanyika katika miji na vijiji.
1. Hokkaidō |
2. Aomori |
8. Ibaraki |
15. Niigata |
24. Mie |
31. Tottori |
|
40. Fukuoka |
Kwa sasa manispaa za Japani zinaundwa upya kwa kuunganisha mikoa, miji na baadhi ya vijiji. Mabadiliko hayo yatapunguza idadi ya miji nchini Japani.[1]
Historia
Visiwa vilikaliwa na binadamu tangu miaka 30,000 KK.
Wakazi wa sasa wametokana na mchanganyiko wa makabila asili (kama Waainu) na Wakorea waliovamia visiwa hivyo.
Uchumi
Japani ni nchi ya tatu duniani kwa ukubwa wa uchumi.
Dini
Wajapani wanaweza kushiriki ibada za dini mbalimbali kadiri wanavyojisikia, lakini asilimia 60 hawana dini maalumu. Wabuddha ni asilimia 34, wafuasi wa madhehebu ya Shinto ni asilimia 4, Wakristo sanasana ni asilimia 2.3.
Tazama pia
Tanbihi
- ↑ Mabuchi, Masaru (2001). "Municipal Amalgamation in Japan (PDF)" (PDF). World Bank. Iliwekwa mnamo 2006-12-28.
{{cite web}}
: Unknown parameter|month=
ignored (help)
Marejeo
- Flath (2000). The Japanese Economy. Oxford University Press. ISBN 0-19-877503-2.
- Henshall (2001). A History of Japan. Palgrave Macmillan. ISBN 0-312-23370-1.
- Iwabuchi (2002). Recentering Globalization: Popular Culture and Japanese Transnationalism. Duke University Press. ISBN 0-8223-2891-7.
- Jansen (2000). The Making of Modern Japan. Belknap. ISBN 0-674-00334-9.
- Kato; na wenz. (1997). A History of Japanese Literature: From the Man'Yoshu to Modern Times. Japan Library. ISBN 1-873410-48-4.
{{cite book}}
: Explicit use of et al. in:|author2=
(help); Unknown parameter|displayauthors=
ignored (|display-authors=
suggested) (help) - Pilling, David (2014). Bending Adversity: Japan and the Art of Survival. London: Allen Lane. ISBN 978-1-84614-546-9.
- Samuels (2008). Securing Japan: Tokyo's Grand Strategy and the Future of East Asia. Cornell University Press. ISBN 0-8014-7490-6.
- Silverberg (2007). Erotic Grotesque Nonsense: The Mass Culture of Japanese Modern Times. University of California Press. ISBN 0-520-22273-3.
- Sugimoto; na wenz. (2003). An Introduction to Japanese Society. Cambridge University Press. ISBN 0-521-52925-5.
{{cite book}}
: Explicit use of et al. in:|author2=
(help); Unknown parameter|displayauthors=
ignored (|display-authors=
suggested) (help) - Taggart Murphy, R. (2014). Japan and the Shackles of the Past. Oxford and New York, NY: Oxford University Press. ISBN 978-0-19-984598-9.
- Varley (2000). Japanese Culture. University of Hawaii Press. ISBN 0-8248-2152-1.
Viungo vya nje
- Serikali
- Kantei.go.jp, official site of the Prime Minister of Japan and His Cabinet
- Kunaicho.go.jp, official site of the Imperial House
- National Diet Library
- Public Relations Office
- Utalii
- Taarifa za jumla
- Japan entry at The World Factbook
- Japan Ilihifadhiwa 21 Aprili 2009 kwenye Wayback Machine. from UCB Libraries GovPubs
- Japani katika Open Directory Project
- Japan profile from BBC News
- Energy Profile for Japan from the US Energy Information Administration
- Japan from the OECD
- Key Development Forecasts for the Japan from International Futures
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Japani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Japani kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |