Nenda kwa yaliyomo

Kireno

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kireno
Português (pt)
Lugha
Asili Ureno
Brazili
Angola
Msumbiji
Guinea-Bissau
Timor ya Mashariki
Cabo Verde
São Tomé na Príncipe
Wasemaji

L1 : 230 Milioni
L2: 17 Milioni

Jumla: 267 Milioni
Familia za lugha Kihindi-Kiulaya
Kiitalia
Kilatini
Kirumi
Kirumi Magharibi
Kirumi Kusini
Kireno-Galicia
Aina za Awali Kilatini cha Kale
Kilatini halisin
Kireno-Galicia
Mfumo wa kuandika Kilatini
Lugha Rasmi
Lugha rasmi kwa Ureno
Brazili
Angola
Msumbiji
Guinea-Bissau
Timor ya Mashariki
Cabo Verde
São Tomé na Príncipe
Nambari za Msimbo
ISO 639-1 pt
ISO 639-2 por
Glottolog port1283

Wasemaji wa Kireno duniani

Kireno (Português - tamka "purtuGESH") ni lugha ya Kirumi inayozungumzwa hasa nchini Ureno na Brazil, lakini pia Kusini mwa Afrika, Asia Kusini na Asia Kusini-Mashariki.

Imekuwa lugha ya kimataifa kutokana na historia ya ukoloni ya Ureno ikiwa na wasemaji wa lugha ya kwanza milioni 210-215; pamoja na wasemaji wa lugha ya pili kuna watu milioni 270 duniani wanaoelewana kwa Kireno, hivyo ni lugha ya 5 au ya 6 ulimwenguni.

Kutokana na historia ya ukoloni Kireno kimepatikana katika nchi zifuatazo:

Kireno kama lugha rasmi

[hariri | hariri chanzo]

Lugha ya kieneo

[hariri | hariri chanzo]

Historia ya lugha

[hariri | hariri chanzo]

Kireno ni moja kati ya lugha za Kirumi maana yake kimetokana na Kilatini cha Dola la Roma lililotawala eneo la Ureno kwa karne nyingi.

Ni karibu hasa na Kigalicia kinachozungumzwa katika Hispania ya Kaskazini.

Wareno waliacha lugha yao katika makoloni yao. Leo hii idadi ya wasemaji katika Ureno ni milioni 10 tu - idadi kubwa kabisa wako nje ya Ureno, hasa Brazil.

Kireno kilisambaa zaidi katika karne ya 20 kwa sababu Wareno waliondoka Ureno kutafuta kazi katika nchi nyingi za Ulaya. Vilevile kuna Wabrazil na Waangola waliotoka kwao kuhamia penginepo wakienda na lugha yao.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kireno kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.