Eswatini
| Ufalme wa Eswatini Umbuso weSwatini (Kiswazi) Kingdom of Eswatini (Kiingereza) | |
|---|---|
| Kaulimbiu: Siyinqaba (Kiswazi) "Sisi ni ngome" | |
| Wimbo wa taifa: Nkulunkulu Mnikati wetibusiso temaSwati "Mungu, Mpaji wa Baraka kwa Waswati" | |
| Miji mikuu | Mbabane (serikali) Lobamba (bunge) |
| Mji mkubwa | Mbabane |
| Lugha rasmi | Kiswati Kiingereza |
| Kabila | 84 Waswati 10 Wazulu 6 wengine |
Eswatini (jina rasmi: Ufalme wa Eswatini, pia Uswazi) ni nchi ndogo isiyo na pwani Kusini mwa Afrika. Imepakana na Afrika Kusini pande zote isipokuwa kaskazini mashariki inapopakana na Msumbiji. Mnamo 2023, Eswatini ilikuwa na idadi ya watu takriban milioni 1.2 na kuwa nchi ya 155 duniani kwa idadi ya watu. Miji mikuu ni Mbabane na Lobamba huku Mbabane ukiwa pia mji mkubwa nchini humo. Kiingereza na Kiswazi ndizo lugha rasmi.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.
Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.
Waswati walianzisha ufalme wao katikati ya karne ya 18 chini ya Ngwane III; mipaka ya sasa ilikubalika mwaka 1881.
Baada ya vita kati ya Waingereza na Makaburu, Swaziland ilukuwa nchi lindwa ya Uingereza tangu mwaka 1903 hadi 1967.
Chini ya mfalme Sobhuza II aliyetawala kwa muda mrefu sana (1921-1982), Swaziland ilipata uhuru tarehe 6 Septemba 1968.
Siasa
[hariri | hariri chanzo]Eswatini inatawaliwa tangu mwaka 1986 na mfalme Mswati III. Mfalme anapingwa mara nyingi kwa sababu anatumia pesa nyingi kwa ajili yake binafsi ilhali wananchi ni maskini sana. Kwa muda mwingi wa uhuru wa nchi katiba imesimamishwa, na mfalme ametawala peke yake.
Watu
[hariri | hariri chanzo]
Wakazi wengi ni wa kabila la Waswati na kuongea lugha ya Kiswati ambacho ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza. Shuleni kinafundishwa pia Kireno.
Upande wa dini, 89.3% ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, hasa Waprotestanti, lakini pia Wakatoliki (5%). Wanaoendelea kufuata dini asilia za Kiafrika ni 0.5% na Waislamu ni 1%.
Afya
[hariri | hariri chanzo]Eswatini ni kati ya nchi duniani zilizoathiriwa zaidi na Ukimwi; umri wa wastani unafikia miaka 22 pekee kwa sababu ya vifo vingi (64%) vinavyotokana na ugonjwa huo uliopata 26% ya watu wazima wote.
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Government of Eswatini (Kiingereza)
- The Kingdom of Eswatini – a royal experience, official Eswatini tourism website (richly illustrated) (Kiingereza)
- Eswatini National Trust Commission – Conserving Eswatini's Natural and Cultural Heritage, (very extensive descriptions of history, culture and nature) (Kiingereza)
- The Kingdom of Eswatini's Big Game Parks (website about the three big game parks) (Kiingereza)
- Eswatini entry at World Fact Book (Kiingereza)
- eSwatini country profile from the BBC News (Kiingereza)
- Key Development Forecasts for Eswatini from International Futures (Kiingereza)
- Photographs of Swaziland Wildlife – Hlane Royal National Park, Mkhaya Game Reserve (Kiingereza)
| Nchi za Afrika | |
|---|---|
| Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
| Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
| Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira | |
| Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Eswatini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
