Nenda kwa yaliyomo

Eswatini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ufalme wa Eswatini
Umbuso weSwatini (Kiswazi)
Kingdom of Eswatini (Kiingereza)
Kaulimbiu: Siyinqaba (Kiswazi)
"Sisi ni ngome"
Wimbo wa taifa:
Nkulunkulu Mnikati wetibusiso temaSwati
"Mungu, Mpaji wa Baraka kwa Waswati"
Mahali pa Eswatini
Ramani ya Eswatini
Miji mikuuMbabane (serikali)
Lobamba (bunge)
Mji mkubwaMbabane
26°19 S 31°08 E
Lugha rasmiKiswati
Kiingereza
Kabila84 Waswati
10 Wazulu
6 wengine

Eswatini (jina rasmi: Ufalme wa Eswatini, pia Uswazi) ni nchi ndogo isiyo na pwani Kusini mwa Afrika. Imepakana na Afrika Kusini pande zote isipokuwa kaskazini mashariki inapopakana na Msumbiji. Mnamo 2023, Eswatini ilikuwa na idadi ya watu takriban milioni 1.2 na kuwa nchi ya 155 duniani kwa idadi ya watu. Miji mikuu ni Mbabane na Lobamba huku Mbabane ukiwa pia mji mkubwa nchini humo. Kiingereza na Kiswazi ndizo lugha rasmi.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza huaminiwa kuwa wawindaji wa jamii ya Wasani.

Katika karne za kwanza BK walifika wahamiaji Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi.

Waswati walianzisha ufalme wao katikati ya karne ya 18 chini ya Ngwane III; mipaka ya sasa ilikubalika mwaka 1881.

Baada ya vita kati ya Waingereza na Makaburu, Swaziland ilukuwa nchi lindwa ya Uingereza tangu mwaka 1903 hadi 1967.

Chini ya mfalme Sobhuza II aliyetawala kwa muda mrefu sana (1921-1982), Swaziland ilipata uhuru tarehe 6 Septemba 1968.

Eswatini inatawaliwa tangu mwaka 1986 na mfalme Mswati III. Mfalme anapingwa mara nyingi kwa sababu anatumia pesa nyingi kwa ajili yake binafsi ilhali wananchi ni maskini sana. Kwa muda mwingi wa uhuru wa nchi katiba imesimamishwa, na mfalme ametawala peke yake.

Mwanamke kutoka Eswatini akicheza.

Wakazi wengi ni wa kabila la Waswati na kuongea lugha ya Kiswati ambacho ni lugha rasmi pamoja na Kiingereza. Shuleni kinafundishwa pia Kireno.

Upande wa dini, 89.3% ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, hasa Waprotestanti, lakini pia Wakatoliki (5%). Wanaoendelea kufuata dini asilia za Kiafrika ni 0.5% na Waislamu ni 1%.

Eswatini ni kati ya nchi duniani zilizoathiriwa zaidi na Ukimwi; umri wa wastani unafikia miaka 22 pekee kwa sababu ya vifo vingi (64%) vinavyotokana na ugonjwa huo uliopata 26% ya watu wazima wote.

    Tazama pia

    [hariri | hariri chanzo]

    Viungo vya nje

    [hariri | hariri chanzo]
    WikiMedia Commons
    WikiMedia Commons
    Wikimedia Commons ina media kuhusu:


    Nchi za Afrika Bara la Afrika
    Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
    Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
    Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
    Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
    Je unajua kitu kuhusu Eswatini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
    Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
    Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.