Nenda kwa yaliyomo

Tunisia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Tunisia
الجمهورية التونسية
Wimbo wa taifa: "Humat Al-Hima"
Eneo la Tunisia
Mji mkuu
na mkubwa
Tunis
Lugha rasmiKiarabu
Kabila (2021)98% Waarabu
1% Waberber
1% Wayahudi na wengine
SerikaliJamhuri ya Kidemokrasia ya Kiraia
  Rais
Kais Saied
  Waziri Mkuu
Kamel Madouri
Historia
  Kuanzishwa kwa Karthage
814 KK
  Utawala wa Husainid
15 Julai 1705
  Uhuru kutoka Ufaransa
20 Machi 1956
  Kutangazwa kwa Jamhuri
25 Julai 1957
Eneo
  Jumlakm2 163,610 km² (ya 91)
  Maji (asilimia)5.04%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2020 11,708,370
  Msongamano71.65/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2023
  Jumla $162.097 bilioni (ya 82)
  Kwa kila mtu $13,248(ya 113)
PLT (Kawaida)Kadirio la 2023
  Jumla $51.271 bilioni
  Kwa kila mtu $4,190
HDI (2022)0.732
SarafuDinar ya Tunisia (TND)
Majira ya saaUTC+1 CET
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu+216
Jina la kikoa.tn

Tunisia, rasmi kama Jamhuri ya Tunisia (kwa Kiarabu الجمهرية التونسية, al-Jumhūrīya at-Tūnisīya), ni nchi katika Afrika Kaskazini, inayopakana na Bahari ya Mediteranea kaskazini na mashariki, Aljeria magharibi, na Libya kusini-mashariki. Ina idadi ya watu takriban milioni 12, ikiwa ya 79 duniani. Jiji lake kubwa zaidi ni Tunis, ambalo pia ni mji mkuu. Tunisia imegawanyika katika majimbo 24 yanayosimamia utawala wa ndani. Inajulikana kwa makazi ya ustaarabu wa Karthago.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Tunisia iliwahi kutawaliwa na Wafinikia walioanzisha huko mji wa Karthago.

Baada ya hao kushindwa na Roma ya Kale, ilikuwa jimbo la Afrika katika Dola la Roma.

Kisha eneo lake likatawaliwa kwa awamu na Wavandali, Waarabu, Wahispania, Waturuki na Wafaransa.

Mnamo tarehe 20 Machi 1956 Tunisia ilipewa uhuru wake kutoka kwa Wafaransa.

Wakazi karibu wote (98%) wanajiita Waarabu na hutumia lugha ya Kiarabu ambacho ndicho lugha rasmi. Hata hivyo damu yao ni mchanganyiko hasa wa ile ya Waberber, Waarabu na Waturuki.

Takriban watu 200,000, hasa kusini, wanaendelea kuzungumza Kiberber ambacho ni lugha asili ya wenyeji lakini Waberber wengi wamezoea kutumia Kiarabu.

Katika elimu na biashara Kifaransa kinatumika pia sana.

Upande wa dini, Uislamu unafuatwa na asilimia 99 za wakazi, nao ndio dini rasmi, lakini theluthi moja kati yao, na nusu kati ya vijana, wanajitambulisha kama wasio na dini, kiwango kikubwa kuliko nchi zote za Kiarabu. Waliobaki ni Wakristo, hasa Wakatoliki, na Wayahudi wachache.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Tunisia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.