Historia ya Tunisia
Mandhari
Historia ya Tunisia inahusu eneo la Afrika Kaskazini ambalo wakazi wake leo wanaunda Jamhuri ya Tunisia.
Tunisia iliwahi kutawaliwa na Wafinisia kutoka Tiro (Lebanoni ya leo) walioanzisha huko mji wa Karthago.
Baada ya hao kushindwa na Roma ya Kale, ilikuwa jimbo la "Africa" katika Dola la Roma.
Kisha eneo lake likatawaliwa na Wavandali, Waarabu, Wahispania, Waturuki na Wafaransa.
Tarehe 20 Machi 1956 Tunisia ilifanikiwa kupata uhuru wake kutoka kwa Wafaransa.
Mnamo Septemba 2021, Kaïs Saïed alitangaza mageuzi yanayokuja ya Katiba ya 2014 na kuunda serikali mpya.
| Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Tunisia kama enzi zake au matokeo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |