Afrika ya Kati

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
LocationCentralMiddleAfrica.png

Afrika ya Kati ni kanda la bara la Afrika iliyoko katikati ya bara. Katika hesabu ya Umoja wa Mataifa (UM) nchi 9 zifuatazo huhesabiwa kuwa sehemu zake:

Afrika ya Kati

Jina la nchi au eneo,
bendera
Mji Mkuu
Flag of Angola.svg
Angola
Luanda
Flag of Cameroon.svg
Kamerun
Yaoundé
Flag of the Central African Republic.svg
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Bangui
Flag of Chad.svg
Chadi
N'Djamena
Flag of the Republic of the Congo.svg
Kongo, Jamhuri ya
Brazzaville
Flag of the Democratic Republic of the Congo.svg
Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia
Kinshasa
Flag of Equatorial Guinea.svg
Guinea ya Ikweta
Malabo
Flag of Gabon.svg
Gabon
Libreville
Flag of São Tomé and Príncipe.svg
São Tomé na Príncipe
São Tomé

Afrika ya Kati kwa maana ya mpangilio ya UM ni nchi kusini ya jangwa Sahara, mashariki ya Afrika ya Magharibi na upande wa magharibi wa Bonde la Ufa la Afrika ya Mashariki. Mto mkubwa wa kanda ni mto Kongo.

Mwisho wa ukoloni kati ya 1953-1963 palikuwa na Shirikisho la Afrika ya Kati la nchi za kisasa za Malawi, Zambia na Zimbabwe zinazohesabiwa siku hizi kuwa sehemu za Afrika ya Kusini au Afrika ya Magharibi.