Mikoa ya Senegal

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mikoa ya Senegal

Mikoa ya Senegal ni ngazi ya kwanza ya ugatuzi nchini Senegal katika Afrika ya Magharibi. Senegal imegawanywa katika mikoa 14 (kwa Kifaransa: régions). Kila mkoa unasimamiwa na halmashauri yake (Conseil Régional) ambayo wajumbe wake wanachaguliwa na wananchi kwenye ngazi ya tarafa.

Ngazi ya pili ya ugatuzi ni wilaya (departements) 45, tarafa (arrondissements) 103 (ambazo hazina kazi ya kiutawala) na maeneo ya jumuiya za kieneo (collectivités locales) ambazo huchagua maafisa wa utawala.

Orodha ifuatayo inaonyesha mikoa ya Senegal pamoja na idadi ya wakazi kufuatana na sensa ya mwaka 2013.[1]

Mkoa Makao makuu Eneo
(km²)
Wakazi
(sensa 2013)
Dakar Dakar 547 3,137,196
Ziguinchor Ziguinchor 7,352 549,151
Diourbel Diourbel 4,824 1,497,455
Saint-Louis Saint-Louis 19,241 908,942
Tambacounda Tambacounda 42,364 681,310
Kaolack Kaolack   5,357 960,875
Thiès Thiès 6,670 1,788,864
Louga Louga 24,889 874,193
Fatick Fatick 6,849 835,352
Kolda Kolda 13,771 714,392
Matam Matam 29,445 562,539
Kaffrine Kaffrine 11,262 566,992
Kédougou Kédougou 16,800 152,357
Sédhiou Sédhiou 7,341 452,944
Jengo la Halmashauri ya Mkoa huko Ziguinchor. Mikoa huwa na madaraka ya kikatiba nchini Senegal, tofauti na wilaya na tarafa.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Senegal: Administrative Division, tovuti ya Citypopulation.de, iliangaliwa Januari 2022