Mkoa wa Dakar
Mandhari

Mkoa wa Dakar (kwa Kifar.: Region de Dakar) ni mkoa mdogo kabisa kati ya mikoa 14 ya Senegal lakini ni mkoa wa mji mkuu na pia mkoa wenye wakazi wengi.
Mkoa huo unajumlisha mji mkuu Dakar, pamoja na miji ya karibu Pikine, Guédiawaye na Rufisque kwenye rasi ya Cap-Vert ambayo ni sehemu ya Afrika bara iliyopo upande wa magharibi zaidi.
Mkoa wa Dakar umegawanywa katika wilaya (departements) nne.
Wilaya | Eneo (km 2 ) | Idadi ya watu Sensa ya 2013 |
---|---|---|
Dakar | 79 | 1,146,053 |
Guédiawaye | 13 | 329,659 |
Pikine | 87 | 1,170,791 |
Rufisque | 372 | 490,694 |
Jumla ya Mkoa wa Dakar | 547 | 3,137,196 |
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- (Kifaransa)Regional Council of Dakar official website Ilihifadhiwa 11 Machi 2005 kwenye Wayback Machine.
- (Kifaransa)Collectivités locales de Dakar from Republic of Senegal Government site, l'Agence de l'informatique de l'État (ADIE). Ilihifadhiwa 8 Februari 2012 kwenye Wayback Machine.
- (Kifaransa)Décret fixant le ressort territorial et le chef lieu des régions et des départements Ilihifadhiwa 12 Mei 2013 kwenye Wayback Machine., décret n°2002-166 du 21 février 2002.
- (Kifaransa)Code des collectivités locales Ilihifadhiwa 11 Mei 2011 kwenye Wayback Machine., Loi n° 96-06 du 22 mars 1996.