Maji ya chumvi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Watu wanaelea kwenye maji ya chumvi kali ya Bahari ya Chumvi.
Photo of surf
Maji ya bahari katika Mlango wa Malacca.

Maji ya chumvi ni maji yenye kiasi cha myeyusho wa chumvi ndani yake. Kwa kawaida kila aina ya maji huwa na kiwango cha chumvi iliyoyeyushwa. Mwili wa binadamu huwa na kiasi cha chumvi ndani yake kwa hiyo hatusikii chumvi kidogo katika maji au chakula.

Wataalamu mara nyingi hutaja kiwango cha 0.1 % kuwa maji matamu, kiwango juu ya 1% - 1.5% kuwa maji ya chumvi, na hali ya kati kuwa maji ya chumvi kidogo. Maji ya kunywa yasiwe na zaidi ya gramu 1 chumvi kwa kila lita[1].

Asilimia kubwa cha maji duniani inapatikana kwa umbo la maji ya chumvi kwa sababu bahari kuu ya dunia ina karibu maji yote ya duniani. Maji ya bahari huwa na kiwango cha chumvi cha asilimia 3,5 iliyoyeyushwa ndani yake. Kiwango hiki kinatofautiana kidogo na mazingira. Katika tabianchi ya joto uvukizaji ni kubwa zaidi; maji ya uso wa bahari yanavukiza lakini chumvi inabaki hivyo kiwango cha chumvi ni juu kidogo. Karibu na midomo ya mito maji matamu huchanganywa na maji ya bahari kwa hiyo kiwango cha chumvi inaweza kupungua.

Kwa wastani, maji katika bahari ya dunia ina chumvi kwa karibu 3.5% (35 g / L, 599 mM). Hii ina maana kwamba kila kilogramu (takriban sawa na lita moja) cha maji ya bahari ina takriban 35 gramu (1.2 oz) ya chumvi zilizoharibiwa (Zaidi ya sodiamu (Na+) Na kloridi (Cl-) Ions). Wastani wa wiani juu ya uso ni 1.025 kg / L. Maji ya bahari ni denser kuliko maji safi na maji safi yana (wiani 1.0 kg / L saa 4 ° C (39 ° F)) kwa sababu chumvi zilizoharibiwa huongeza wingi kwa kiasi kikubwa. Sehemu ya kufungia ya maji ya bahari inapungua kama ongezeko la chumvi linapo ongezeka. Katika salinity ya kawaida, inafungia saa 2 ° C (28 ° F). Maji ya bahari ya baridi (katika hali ya kioevu) ilikuwa mwaka 2010, katika mkondo chini ya glacier ya Antarctic, na kipimo cha -2.6 ° C (27.3 ° F). Maji ya bahari ya pH ni kawaida kwa kiwango cha kati ya 7.5 na 8.4. Hata hivyo, hakuna kiwango cha pH kinachokubaliwa kwa kiwango kikubwa kwa maji ya bahari na tofauti kati ya vipimo kulingana na mizani tofauti ya kumbukumbu inaweza kuwa hadi vipimo 0.14.

Kuna maziwa kadhaa ambako kiwango cha chumvi kiko juu sana. Mfano mashuhuri ni Bahari ya Chumvi ya Palestina[2] yenye kiwango cha chumvi ya 28%. Maziwa kadhaa huwa na viwango vya juu zaidi.

Matumizi kwa manufaa ya kibinadamu[hariri | hariri chanzo]

Matumizi ya maji ya chumvi ni zaidi ya bahari yaani kwa usafiri wa meli na uvuvi. Matumizi kwenye nchi kavu si kubwa sana. Haifai kwa kilimo kwa sababu mimea ya bara hawezi kumwagiliwa kwa maji ya chumvi. Matumizi ni hasa kusafisha udongo na miamba inayochimbwa kwenye migodi halafu kupoza vituo vya nguvu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maelezo[hariri | hariri chanzo]

  1. Salinity and drinking water , tovuti ya serikali ya Australia Kusini, iliangaliwa Oktoba 2019
  2. Ziwa hili lagawiwa kati ya Yordani, Israeli na mamlaka ya Palestina

Marejeo[hariri | hariri chanzo]