Papa Miltiades

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Miltiades.

Papa Miltiades alikuwa Papa kuanzia tarehe 2 Julai 311 hadi kifo chake tarehe 10 Januari 314[1]. Kadiri ya Liber Pontificalis, Miltiades alikuwa na asili ya Afrika[2], ingawa aliweza pia kuwa mtu wa Roma.[3]

Alimfuata Papa Eusebius akafuatwa na Papa Silvester I. Alifurahia amani ambayo Kanisa lilirudishiwa na kaisari Konstantino Mkuu, na ingawa alipingwa sana na Wadonati, alishughulikia kwa busara upatanisho[4].

Wakati wa Upapa wake Hati ya Milano iliwapa wananchi uhuru wa dini (313) na Kanisa lilirudishiwa mali yake iliyotaifishwa.

Alipinga fundisho la Donatus wa Carthago la kwamba mapadri na maaskofu walioasi wabatizwe tena. Uaumuzi huo wa Sinodi ya Laterano (313) haukumaliza uenezi wa farakano la Donato katika Afrika Kaskazini.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[5].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://dacb.org/stories/tunisia/militiades/
  3. Richard P. McBrien, Lives of the Popes, (HarperCollins, 2000), 56.
  4. Martyrologium Romanum
  5. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Burris, Ronald D. (2012). Where Is the Church?: Martyrdom, Persecution, and Baptism in North Africa from the Second to the Fifth Century. Eugene, OR: Wipf and Stock Publishers. ISBN 9781608998081. 
  • Calendarium Romanum. Vatican: Libreria Editrice Vaticana. 1969. 
  • De Clerq, Victor Cyril (1954). Ossius of Cordova: A Contribution to the History of the Constantinian Period. Washington, D.C.: Catholic University of America Press. 
  • Finn, Thomas M. (2004). Quodvultdeus of Carthage: The Creedal Homilies. Mahwah, New Jersey: The Newman Press. ISBN 9780809105724. 
  • Gibbon, Edward (2008). The History of the Decline and Fall of the Roman Empire. New York City: Cosimo, Inc. ISBN 9781605201221. 
  • Green, Bernard (2010). Christianity in Ancient Rome: The First Three Centuries. London: T&T Clark International. ISBN 9780567032508. 
  • Kirsch, Johann Peter (1909). "Eusebius, Pope St.". In Herbermann, Charles G.; Pace, Edward A.; Pallen, Condé B.; Shahan, Thomas J.; Wyne, John J. The Catholic Encyclopedia 5. New York: Encyclopedia Press, Inc. 
  • Kirsch, Johann Peter (1912). "Marcellinus, Pope St.". In Herbermann, Charles G.; Pace, Edward A.; Pallen, Condé B.; Shahan, Thomas J.; Wyne, John J. The Catholic Encyclopedia 9. New York: Encyclopedia Press, Inc. 
  • Kirsch, Johann Peter (1913). "Miltiades, Pope St.". In Herbermann, Charles G.; Pace, Edward A.; Pallen, Condé B.; Shahan, Thomas J.; Wyne, John J. The Catholic Encyclopedia 10. New York: Encyclopedia Press, Inc. 
  • Lenski, Noel Emmanuel (2012). The Cambridge Companion to the Age of Constantine. Cambridge: Cambridge University Press. ISBN 9781107013407. 
  • Levillain, Philippe, ed. (2002). The Papacy: an Encyclopedia 2. New York City: Routledge. 
  • Malveaux, Ethan (2015). The Color Line: A History. Bloomington, IN: Xlibris Corporation. ISBN 9781503527591. 
  • Martyrologium Romanum. Vatican: Libreria Editrice Vaticana. 2001. ISBN 978-8820972103. 
  • McBrien, Richard P. (2000). Lives of the Popes. New York, NY: HarperCollins. ISBN 9780060653040.  Unknown parameter |url-access= ignored (help)
  • O'Malley, John (2009). A History of the Popes: From Peter to the Present. Lanham, MD: Government Institutes. ISBN 9781580512299. 
  • Serralda, Vincent; Huard, André (1984). Le Berbère – lumière de l'Occident [The Berbers – the Light of the West] (in French). Paris: Nouvelles Editions Latines. ISBN 9782723302395. 
  • White, Cynthia (2007). The Emergence of Christianity. Westport, CT: Greenwood Press. ISBN 9780313327995. 

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Miltiades kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.