Papa Silvester I
Papa Silvester I alikuwa Papa kuanzia tarehe 31 Januari 314 hadi kifo chake tarehe 31 Desemba 335[1].
Alimfuata Papa Miltiades akafuatwa na Papa Marko.
Mtoto wa Rufinus, mkazi wa Roma, hatuna habari nyingi za maisha yake. Ila ni kwamba aliongoza kwa busara Kanisa Katoliki kwa muda mrefu mara baada ya Kaisari Konstantino Mkuu kulipatia uhuru wa dini na kulijengea maabadi mengi, makubwa tena mazuri.
Wakati wa utawala wake ulifanyika mtaguso mkuu wa kwanza (Nisea, leo nchini Uturuki, 325) uliomshangilia Kristo kama Mwana wa Mungu. Yeye hakuhudhuria, ila alituma wajumbe wawili akathibitisha maamuzi yaliyofikiwa.
Alizikwa katika katakombu la Prisila [2].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[3].
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
- Orodha ya Mapapa
- Mababu wa Kanisa
Maandishi yake
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.html
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/30600
- ↑ Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- Gisela Schmitt (1995). "Pope Sylvester I". In Bautz, Traugott (ed.). Biographisch-Bibliographisches Kirchenlexikon (BBKL) (in German). Vol. 10. Herzberg: Bautz. col. 338–341. ISBN 3-88309-062-X.
- Johann Peter Kirsch (1912). "Pope St. Sylvester I (314–335)". In Herbermann, Charles (ed.). Catholic Encyclopedia. Vol. 14. New York: Robert Appleton Company.
- Francesco Scorza Barcellona: Silvestro I, santo. In: Massimo Bray (ed.): Enciclopedia dei Papi. Rome 2000 (treccani.it)
- H.U. Instinsky: Silvester I. In: Josef Höfer, Karl Rahner (Hrsg.): Lexikon für Theologie und Kirche. 2. Auflage. Band 9. Herder, Freiburg im Breisgau 1964, Sp 757–758.
- Horst Fuhrmann (1991). "Konstantinische Schenkung". Lexikon des Mittelalters, V: Hiera-Mittel bis Lukanien (in German). Stuttgart and Weimar: J. B. Metzler. col. 1385–1387. ISBN 3-7608-8905-0.
- Wilhelm Pohlkamp (1995). "Silvester I., Papst (314–335)". Lexikon des Mittelalters, VII: Planudes bis Stadt (Rus’) (in German). Stuttgart and Weimar: J. B. Metzler. col. 1905–1908. ISBN 3-7608-8907-7.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Kuhusu Papa Silvester I katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki
- Maisha yake Ilihifadhiwa 5 Machi 2016 kwenye Wayback Machine.
- Colonnade Statue in St Peter's Square
- Legenda Aurea
- Akathist to Saint Sylvester
- Canon to Saint Sylvester
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Silvester I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |