Papa Fransisko

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Fransisko siku alipotangaza watakatifu watangulizi wake Yohane XXIII na Yohane Paulo II (2014). Amevaa kanzu nyeupe kama inavyotumiwa na maaskofu wa Roma tangu karne ya 16.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Kardinali Jorge Bergoglio akiongea na rais wa Argentina, Cristina Fernández de Kirchner.

Papa Fransisko, S.I. (kwa Kilatini Franciscus, jina la awali Jorge Mario Bergoglio) ni askofu wa Roma, na hivyo pia Papa wa Kanisa Katoliki duniani kote, tangu tarehe 13 Machi 2013.

Amemfuata Papa Benedikto XVI akiwa wa 266 katika orodha ya mapapa.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Umati wa watu milioni 6 wakishiriki Misa iliyongozwa na Papa Fransisko huko Rizal Park, Manila, Ufilipino, tarehe 18 Januari 2015.

Alizaliwa tarehe 17 Desemba 1936 huko Buenos Aires, mji mkuu wa Argentina, hivyo ni papa wa kwanza kutokea bara la Amerika. Pia ni wa kwanza kutoka Shirika la Yesu.

Baada ya masomo ya kemia na kipindi kifupi cha kazi, tarehe 11 Machi 1958 aliitikia wito wa kitawa na wa kipadri, akaweka nadhiri za muda tarehe 12 Machi 1960, akapata upadrisho tarehe 13 Desemba 1969.

Tarehe 22 Aprili 1973 aliweka nadhiri za daima.

Kati ya miaka 1973 na 1979 alikuwa mkuu wa shirika nchini Argentina.

Mwaka 1992 alichaguliwa kuwa askofu msaidizi wa Buenos Aires akapewa daraja hiyo tarehe 27 Juni mwaka huo, halafu akawa askofu mkuu wa Buenos Aires tarehe 28 Februari 1998, pia askofu wa Wakatoliki wa Mashariki wa Argentina wasio na askofu wa kwao tarehe 6 Novemba 1998, akateuliwa kuwa kardinali tarehe 21 Februari 2001.

Kati ya miaka 2005 na 2011 alikuwa rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki la Argentina.

Alichaguliwa Papa tarehe 13 Machi 2013, wiki mbili baada ya mtangulizi wake kung'atuka.

Tofauti na kawaida, alijichagulia jina lisilowahi kutumiwa na mapapa waliomtangulia. Chaguo hilo linaelekeza nia ya kufuata kwa namna fulani roho ya Fransisko wa Asizi.

Hata kabla ya kuchaguliwa alijulikana kwa unyenyekevu na ufukara wake, pamoja na juhudi za kutetea haki za wanyonge, imani sahihi na maadili ya Kanisa.

Tabia hizo alizileta katika ngazi ya juu ya Kanisa Katoliki, akijivutia mioyo ya watu wengi.

Tarehe 13 Aprili 2013 alichagua Jopo la Makardinali 8 kutoka mabara yote limsaidie kuongoza Kanisa na kurekebisha idara na ofisi zake huko Vatikano.

Tarehe 29 Juni 2013, Papa Fransisko alitoa waraka wake wa kwanza, "Lumen Fidei", kuhusu imani; huo ulifuatwa tarehe 24 Novemba 2013 na "Evangelii Gaudium" kuhusu uinjilishaji.

Tarehe 18 Juni 2015, alitoa barua ensiklika kwa watu wote "Laudato si'" kuhusu mazingira, mabadiliko ya hali ya hewa na maendeleo ya kufaa. Barua hiyo ilipokewa vizuri na wengi.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi[hariri | hariri chanzo]

Vitabu[hariri | hariri chanzo]

  • Bergoglio, Jorge (1982). Meditaciones para religiosos [Meditations for the Religious] (in Spanish). Buenos Aires: Diego de Torres. OCLC 644781822. 
  • Bergoglio, Jorge (1992). Reflexiones en esperanza [Reflections of Hope] (in Spanish). Buenos Aires: Ediciones Universidad del Salvador. OCLC 36380521. 
  • Bergoglio, Jorge (2003). Educar: exigencia y pasión: desafíos para educadores cristianos [To Educate: Exactingness and Passion: Challenges for Christian Educators] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 9789505124572. 
  • Bergoglio, Jorge (2003). Ponerse la patria al hombro: memoria y camino de esperanza [Putting the Motherland on One's Shoulders: Memoir and Path of Hope] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 9789505125111. 
  • Bergoglio, Jorge (2005). La nación por construir: utopía, pensamiento y compromiso: VIII Jornada de Pastoral Social [The Nation to Be Built: Utopia, Thought, and Commitment] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 9789505125463. 
  • Bergoglio, Jorge (2006). Corrupción y pecado: algunas reflexiones en torno al tema de la corrupción [Corruption and Sin: Some Thoughts on Corruption] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 9789505125722. 
  • Bergoglio, Jorge (2006). Sobre la acusación de sí mismo [On Self-Accusation, (or from the Italian, Humility: The Road towards God)] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 978-950-512-549-4. 
  • Bergoglio, Jorge (2007). El verdadero poder es el servicio [True Power Is Service] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. OCLC 688511686. 
  • Bergoglio, Jorge (2009). Seminario: las deudas sociales de nuestro tiempo: la deuda social según la doctrina de la iglesia [Seminar: the Social Debts of Our Time: Social Debt According to Church Doctrine] (in Spanish). Buenos Aires: EPOCA-USAL. ISBN 9788493741235. 
  • Bergoglio, Jorge; Skorka, Abraham (2010). Sobre el cielo y la tierra [On Heaven and Earth] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Sudamericana. ISBN 9789500732932. 
  • Bergoglio, Jorge (2010). Seminario Internacional: consenso para el desarrollo: reflexiones sobre solidaridad y desarrollo [International seminar: Consensus about Development: Reflexions on Solidarity and development] (in Spanish). Buenos Aires: EPOCA. ISBN 9789875073524. 
  • Bergoglio, Jorge (2011). Nosotros como ciudadanos, nosotros como pueblo: hacia un bicentenario en justicia y solidaridad [Ourselves as Citizens, Ourselves as a People: towards a Bicentenary in Justice and Solidarity] (in Spanish). Buenos Aires: Editorial Claretiana. ISBN 9789505127443. 

Mengine[hariri | hariri chanzo]

  • Bergoglio, Jorge (1995). La vida sagrada y su misión en la Iglesia y en el mundo (in Spanish). Argentina Catholic University: Faculty of Theology. OCLC 806712655. 
  • Egan, Edward Michael; Bergoglio, Jorge (2001). "Episcopus minister Evangelii Iesu Christi propter spem mundi: relatio post disceptationem". The Catholic Church. The Synod of Bishops. Ordinary General Assembly. E Civitate Vaticana. OCLC 749998123
      .

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons