Papa Stefano I

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Papa Stefano I alikuwa Papa kuanzia tarehe 12 Machi 254 hadi kifodini chake tarehe 2 Agosti 257[1][2]. Alitokea Roma, Italia, ingawa aliweza kuwa na asili ya Ugiriki.

Alimfuata Papa Lucius I akafuatwa na Papa Sisto II.

Alifundisha kwamba waliobatizwa na madhehebu yaliyojitenga na Kanisa Katoliki hawahitaji kubatizwa tena, tofauti na walivyodai baadhi ya maaskofu, hasa wa Afrika Kaskazini. Baadaye msimamo wake ulienea kote katika Kanisa la Kilatini.

Inasimuliwa kwamba aliuawa na maaskari wa Kaisari Valerian wakati wa Misa[3] .

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu, pengine mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 2 Agosti [4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Mann, Horace (1912). "Pope St. Stephen I" in The Catholic Encyclopedia. Vol. 14. New York: Robert Appleton Company.
  3. The golden legend: readings on the saints By Jacobus de Voragine, William Granger Ryan
  4. "Martyrologium Romanum" (Libreria Editrice Vaticana, 2001 ISBN 88-209-7210-7)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Stefano I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.