Papa Urban I

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Urbano I

Papa Urban I alikuwa Papa kuanzia tarehe 14 Oktoba 222 hadi kifo chake tarehe 23 Mei 230[1]. Alitokea Roma, Italia.

Alimfuata Papa Kalisto I akafuatwa na Papa Ponsyano.

Urban I ni Papa wa kwanza ambaye tarehe zake zina hakika ya kihistoria[2]. Inaonekana hakukuwa na dhuluma za serikali wakati wa Upapa wake, lakini alipaswa bado kupambana na farakano la Hipoliti wa Roma[3] pamoja na kuongoza kwa uaminifu Kanisa la Roma miaka minane.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu, hasa tarehe 19 Mei, sikukuu yake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. Kung, Hans. The Catholic Church: A Short History. New York; The Modern Library, 2003, p. 41
  3. "Pope Urban I". Catholic Encyclopedia. New York: Robert Appleton Company. 1913. http://www.newadvent.org/cathen/15209a.htm.
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Urban I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.