Uaminifu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Katika Biblia, Hosea ni kielelezo cha uaminifu wa mume kwa mke wake. Mchoro mdogo wa mwaka 1340 hivi katika Klosterneuburger Evangelienwerk, fol. 7v.

Uaminifu (kutoka neno la Kiarabu; kwa Kiingereza: faithfulness) ni tabia njema ya mtu inayomfanya akubalike kwa wengine hata wakampatia dhamana ya pesa au mamlaka fulani.

Kwa kawaida unapatikana kwa kuishi sawasawa na maadili ya Mungu, dini au jamii; kwa mfano sheria na taratibu za asasi, kampuni au serikali.