Kampuni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kampuni (kutoka Kiingereza "company") ni asasi au shirika linalotambuliwa kisheria ambalo limeundwa kwa ajili ya kuunda au kuuza bidhaa na / au huduma kwa wateja[1] na linashughulika na aina yoyote ya biashara.

Ufafanuzi wa neno na taratibu za sheria hutofautiana nchi kwa nchi. Kwa ujumla, kampuni shirika la biashara linalotengeneza bidhaa kwa namna iliyopangwa na kuziuza kwa umma ili kupata faida.

Kampuni inaweza kuajiri watu kuwa wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Kampuni zinapatikana sana katika uchumi wa kibepari, nyingi zikiwa zinamilikiwa na watu binafsi kwa ajili ya kupata faida ambayo itaongeza mali ya wamiliki wake na kuikuza biashara yenyewe. Wamiliki na wahudumu wa biashara huwa na lengo mojawapo kuu kama kupata mapato ya kifedha kutokana na kazi wanayoifanya napia kwa sababu ya kukubali kujiingiza kwenye hatari ya kufanya biashara. Baadhi ya kampuni ambazo malengo yake siyo kama yale yaliyosemwa hapo juu ni kama vyama vya ushirika na kampuni zinazomilikiwa na serikali.

Biashara pia inaweza kuanzishwa bila kusudi la kupata faida au biashara inayomilikiwa na serikali.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Sullivan, arthur; Steven M. Sheffrin (2003). Economics: Principles in action. Upper Saddle River, New Jersey 07458: Prentice Hall. p. 29. ISBN 0-13-063085-3. Archived from the original on 2016-12-20. Retrieved 2021-02-24. 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kampuni kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.