Papa Silvester I
Mandhari
(Elekezwa kutoka Papa Sylvester I)

Papa Silvester I alikuwa Papa kuanzia tarehe 31 Januari 314 hadi kifo chake tarehe 31 Desemba 335[1].
Alimfuata Papa Miltiades akafuatwa na Papa Marko.
Mtoto wa Rufinus, mkazi wa Roma, hatuna habari nyingi za maisha yake. Ila ni kwamba aliongoza kwa busara Kanisa Katoliki kwa muda mrefu mara baada ya Kaisari Konstantino Mkuu kulipatia uhuru wa dini na kulijengea maabadi mengi, makubwa tena mazuri [2].
Wakati wa utawala wake ulifanyika mtaguso mkuu wa kwanza (Nisea, leo nchini Uturuki, 325) uliomshangilia Kristo kama Mwana wa Mungu. Yeye hakuhudhuria, ila alituma wajumbe wawili akathibitisha maamuzi yaliyofikiwa.
Alizikwa katika katakombu la Prisila [3].
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Maandishi yake
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.html
- ↑ Masomo ya Breviari - Sikukuu za Bwana, za Bikira Maria na za Watakatifu - Ndanda Mission Press 1978, uk 486-488
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/30600
- ↑ Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
Marejeo ya Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]- John Kabeya na wengine - Maisha ya Watakatifu – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1965, 1989, uk. 473-474
- Pd. Leandry Kimario, O.F.M.Cap. - Mfahamu Mtakatifu Somo Wako - Maisha ya Watakatifu wa Kila Siku pamoja na Watakatifu Wafransisko - Toleo la pili - Dar es Salaam 2021, uk. 411-412
- Maurice Soseleje, Kalendari yetu – Maisha ya Watakatifu – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Peramiho 1986 – ISBN 9976-63-112-X, uk. 98
Marejeo ya lugha nyingine
[hariri | hariri chanzo]- Gisela Schmitt (1995). "Pope Sylvester I". In Bautz, Traugott (ed.). Biographisch-Bibliographisches Kirchenlexikon (BBKL) (in German). Vol. 10. Herzberg: Bautz. col. 338–341. ISBN 3-88309-062-X.
- Johann Peter Kirsch (1912). "Pope St. Sylvester I (314–335)". In Herbermann, Charles (ed.). Catholic Encyclopedia. Vol. 14. New York: Robert Appleton Company.
- Francesco Scorza Barcellona: Silvestro I, santo. In: Massimo Bray (ed.): Enciclopedia dei Papi. Rome 2000 (treccani.it)
- H.U. Instinsky: Silvester I. In: Josef Höfer, Karl Rahner (Hrsg.): Lexikon für Theologie und Kirche. 2. Auflage. Band 9. Herder, Freiburg im Breisgau 1964, Sp 757–758.
- Horst Fuhrmann (1991). "Konstantinische Schenkung". Lexikon des Mittelalters, V: Hiera-Mittel bis Lukanien (in German). Stuttgart and Weimar: J. B. Metzler. col. 1385–1387. ISBN 3-7608-8905-0.
- Wilhelm Pohlkamp (1995). "Silvester I., Papst (314–335)". Lexikon des Mittelalters, VII: Planudes bis Stadt (Rus’) (in German). Stuttgart and Weimar: J. B. Metzler. col. 1905–1908. ISBN 3-7608-8907-7.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Kuhusu Papa Silvester I katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki
- Maisha yake Ilihifadhiwa 5 Machi 2016 kwenye Wayback Machine.
- Colonnade Statue in St Peter's Square
- Legenda Aurea
- Akathist to Saint Sylvester
- Canon to Saint Sylvester
| Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Silvester I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |
