Papa Caio

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Kayo

Papa Caio alikuwa Papa kuanzia tarehe 17 Desemba 283 hadi kifo chake tarehe 22 Aprili 296[1]. Alitokea Dalmatia, leo nchini Korasya[2].

Alimfuata Papa Eutychian akafuatwa na Papa Marcellinus.

Wakati wa Upapa wake, chokochoko dhidi ya Wakristo zilianza kuongezeka tena, ingawa waliweza kujenga makanisa na kupanua mashamba ya Mungu. Alidai muumini asipewe uaskofu bila kupitia kwanza daraja zote za chini[3]. Alikwepa dhuluma ya kaisari Dioklesyano, anayesemekana alikuwa na undugu naye.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake[4].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Maandishi yake[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. http://www.santiebeati.it/dettaglio/50400 (Kiitalia)
  3. Saint of the Day, April 22: Caius Archived 28 Oktoba 2013 at the Wayback Machine SaintPatrickDC.org. Retrieved 4 March 2012.
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Caio kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.