Papa Agapeto I
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Papa Agapeto I alikuwa papa kuanzia mwezi wa Mei au Juni 535 hadi kifo chake tarehe 22 Aprili, 536. Alimfuata Papa Yohane II. Muda sio mrefu baada ya kifo chake alianza kuangaliwa kuwa mtakatifu. Sikukuu yake ni 20 Septemba, tarehe alipomwondosha madarakani Anthimus, askofu mkuu wa Trebizond kwa ajili ya mafunzo yake ya Kiariani yaliyoangaliwa kuwa ya uwongo.
[hariri] Viungo vya nje
Kuhusu Papa Agapeto I katika Kamusi Elezo ya Kikatoliki

