Papa Celestino V

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mt. Selestini V.

Papa Celestino V, O.S.B. (121519 Mei 1296) alikuwa Papa kuanzia tarehe 5 Julai/29 Agosti 1294 hadi 13 Desemba 1294[1]. Alitokea Molise, Italia[2].

Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Pietro Angelerio wa Morrone. Baada yake hakuna tena Papa aliyejichagulia jina la Celestino.

Alimfuata Papa Nikolasi IV baada ya miaka miwili ya pengo[3], akichaguliwa kutokana na umri wake mkubwa na sifa ya utakatifu na utendaji miujiza.

Ni maarufu kwa kuwa mwaka uleule alijiuzulu[4] kwa kujitambua hawezi Upapa [5] ili arudi kuishi maisha ya upwekeni kama mmonaki (mwaka 1244 alikuwa ameanzisha shirika la Waselestini, tawi la Wabenedikto)[6]. Lakini Papa Bonifasi VIII aliyemfuata alimfunga akafuta karibu maamuzi yake yote.

Alitangazwa na Papa Klementi V kuwa mtakatifu tarehe 5 Mei 1313[7].

Sikukuu yake ni tarehe 19 Mei[8].

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. After more than two years, a consensus had still not been reached. Pietro, well known to the cardinals as a Benedictine hermit, sent the cardinals a letter warning them that divine vengeance would fall upon them if they did not quickly elect a pope. Latino Malabranca, the aged and ill dean of the College of Cardinals cried out, "In the name of the Father, the Son, and the Holy Ghost, I elect brother Pietro di Morrone." The cardinals promptly ratified Malabranca's desperate decision. When sent for, Pietro obstinately refused to accept the papacy, and even, as Petrarch says, tried to flee, until he was finally persuaded by a deputation of cardinals accompanied by the king Charles II of Naples and Charles Martel of Anjou, pretender to the throne of Hungary.
  4. Johnston, Bruce. "Cardinal hints that ailing Pope may resign", The Telegraph, 8 February 2005. 
  5. Clement V's bull of canonization noted his "marvelous simplicity and inexperience[] in everything belonging to the rule of the Church" Wood, Charles T. Joan of Arc and Richard III: Sex, Saints, and Government in the Middle Ages. Oxford University Press, 1991, 100.
  6. Loughlin, JF (1908). "Pope St. Celestine V". The Catholic Encyclopedia 3. New York: Robert Appleton Company. 
  7. Ronald C. Finucane (2011). Contested Canonizations: The Last Medieval Saints, 1482–1523. Catholic University of America Press, p. 19.
  8. Martyrologium Romanum

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Papa Celestino V kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.