Abakuria

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Wakuria)
Kundi la densi la Wakuria wakiimba na kucheza kule Kenya.

Abakuria (au Wakurya) ni kabila la watu wanaoishi katika wilaya za Rorya, Tarime na Serengeti kwenye mkoa wa Mara, kaskazini mwa Tanzania, na katika kaunti ya Migori katika sehemu ya kusini mashariki ya Kenya.

Mnamo mwaka 2005, idadi ya Abakuria ilikadiriwa kuwa 690,000, ikiwa ni 430,000 wanaoishi nchini Tanzania na 260,000 nchini Kenya.

Lugha yao ni Kikuria.

Abakuria ni wakulima na wafugaji, huku Abakuria wa nchini Kenya wakiegemea sana kwa kilimo nao wa nchini Tanzania wakiegemea sana ufugaji. Hasa Abakuria walio katika wilaya ya Serengeti wanatambulika kama wafugaji.

Kilimo cha asili walikuwa wanalima ulezi mtama na viazi tu kwa ajili ya kutengeneza Togwa (obosara) na Pombe. Mazao mengine yalianza kulimwa miaka ya 1900 baada ya wajerumani kuhimiza kilimo. Wakurya hawapendi kutawaliwa wala kuonewa hivyo walikuwa na saiga lika ya vijana kwa ajili ya ulinzi na usalama hivyo utumwa haukuwaathiri sana. Ila kwa kupenda kwao vita walijiunga sana na jeshi K.A.R (King African Rifle) kupigana vita ya kwanza na ya pili na ya Uganda.[1]

Abakuria wanafanana na Wakisii wa nchini Kenya kwa lugha na umbile. Wanadhaniwa walikuwa kundi moja hadi waliposhambuliwa vikali na Wamasai mnamo karne ya 19 na kusambaratishwa katika maeneo tofautitofauti.

Utengano huo ulisababisha kuweko kwa lahaja mbili ambazo zinaeleweka na kila kundi.

Abakuria wamegawanyika katika "makabila madogo" au koo kumi na sita, nazo ni: Nyabasi, Bakira, Bairege, Bagumbe (wanaoishi Kenya na Tanzania), Batimbaru, Banyamongo, Bakenye, Basimbiti, Basweta, Barenchoka, Baikoma, Bamerani na mengineyo. Makabila haya madogo yote yapo pia katika kabila la Wakisii nchini Kenya.

Wakurya ni kabila ambalo huona vita kama mchezo na kuua ni kama kucheza tu na usiombe ukutane nao wakiwa na hasira. Ila ni watu wema sana wakati wa amani: usipowachokoza hawana ubaya na mtu ila ukiwakosea bila kujua hukusamehe hata kabla hujaomba msamaha ila ukiwakosea makusudi hawana msamaha kabisa. Wakurya ni watu ambao hawasalimu amri ukionesha kuwashinda huenda kujipanga upya na kutafakari ni jinsi gani watashinda na si watu wa kukata tamaa na wakiwa na mori hawaogopi chochote wala lolote wako tayari kukabiliana nalo.

Kabila la Abakuria pia linakaribiana na kabila la Wazanaki katika Mkoa wa Mara nchini Tanzania. Itikadi zao kadhaa zinafanana.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Abakuria kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Makala hii kuhusu utamaduni wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Abakuria kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.