Waturkana

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Turkana
Mzee Mturkana na watoto katika mavazi ya kijadi.
Watu kwa jumla
340,000
Maeneo penye idadi kubwa kiasi
Kaskazini-Magharibi ya Kenya
Lugha

Kiturkana

Dini

dini ya jadi, Ukristo

Makundi yaliyo karibu kiukoo au kiutamaduni

Wamasai

Waturkana ni watu wa jamii ya Waniloti wa Kenya, idadi yao ikiwa karibu 340,000. Ni wakazi wa Kaunti ya Turkana, kaskazini magharibi mwa Kenya, eneo kame na kavu linalopakana na Ziwa Turkana upande wa mashariki.

Kusini kwao wanaishi Wapokot (Wapökoot), Warendille na Wasamburu. Lugha ya Waturkana, lugha yenye asili ya Kiniloti cha Mashariki, hujulikana kama Kiturkana; jina lao kwa lugha hii ni Ng'aturk(w)ana.

Waturkana wanajulikana kwa kufuga ngamia na kushona vikapu. Katika fasihi simulizi zao, hujiita watu wa fahali ya kijivu, kutokana na Zebu, ambaye ukuzaji wake una nafasi muhimu katika historia yao.

Katika miaka ya karibuni, mipango ya misaada ya maendeleo imelenga kuanzisha uvuvi miongoni mwa jamii ya Waturkana (ambao ni mwiko kwao) na imepata mafanikio mbalimbali.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Mifugo[hariri | hariri chanzo]

Waturkana hutegemea mito kadhaa, kama vile Mto Turkwel na Mto Kerio. Mito hiyo inapofurika, mchanga uliobebwa na maji ya mto pamoja na maji hujaza maeneo wazi ya mto na maeneo hayo hulimwa baada ya mvua nzito, ambayo kutokea kwa nadra. Wakati mito inapokauka, visima wazi huchimbwa katika maeneo ya mito na maji yake hutumiwa kwa matumizi ya binadamu na kunywesha mifugo. Kuna visima vizuri vichache, iwapo vipo, kwa ajili ya maji ya matumizi ya jamii na mifugo, na mara nyingi familia hulazimika kusafiri saa kadhaa kutafuta maji kwa ajili yao na ya mifugo.

Mifugo ni kipengele muhimu kwa utamaduni wa Waturkana. Mbuzi, ngamia, punda na ng'ombe wa zebu ndio kundi la msingi la mifugo wanaotumiwa na Waturkana. Katika jamii hii, mifugo si tu kuwapa maziwa na nyama, bali pia kama aina ya sarafu inayotumika kwa ajili ya ulipaji wa mahari. Mara nyingi, kijana atapewa mbuzi mmoja wa kuanzia, na atalimbikiza zaidi kwa ufugaji. Kwa upande mwingine, baada ya kulimbikiza mifugo wa kutosha, mifugo hao watatumika kulipia mahari kwa wake zao. Ni kawaida kwa wanaume wa Kiturkana kuwa na maisha ya ndoa ya bibi wengi, kwani idadi ya mifugo itaashiria idadi ya wake kila mmoja anaweza kulipia na kukimu.

Chakula[hariri | hariri chanzo]

Waturkana hutegemea mifugo wao kwa maziwa, nyama na damu. Zebu huliwa tu wakati wa sikukuu lakini mbuzi huliwa mara kwa mara. Nyama ya ngamia na samaki ni mwiko.

Waturkana mara kwa mara hufanya biashara na Wamasai kwa mahindi na mboga. Waturkana hununua chai kutoka mijini na kutengeneza chai ya maziwa. Asubuhi watu hunywa uji wa mahindi na maziwa, na wakati wa chakula cha mchana na chakula cha jioni, hula ugali wa mahindi kwa kitoweo.

Wanaume mara nyingi huenda uwindaji kushika swala, nguruwe mwitu, kulungu, sungura na wengine zaidi. Baada ya uwindaji, wanaume huenda tena kukusanya asali ambayo ndiyo kitu kitamu zaidi ambacho Waturkana wanacho.

Nyumba[hariri | hariri chanzo]

Nyumba hujengwa kwa kutumia miti na kisha kuvimbwa na nyasi na kisha kufungwa. Nyumba ni kubwa kutosha kwa familia ya watu sita. Kawaida, wakati wa msimu wa mvua nyumba hufanywa kuwa ndefu na hufunikwa kwa samadi. Mifugo huwekwa kwenye zizi la miti.

Mavazi[hariri | hariri chanzo]

Kijadi, wanaume na wanawake wote huvaa mikanda iliyotengenezwa kwa ngozi ya mraba, lakini kila jinsia ya watu hujipamba kwa vitu mbalimbali.

Mara nyingi wanaume huvalia mikanda zao sawa na shuka mara nyingi upande mmoja ukishikana na mwingine kwenye bega lao la kulia, na hubeba visu vya mkononi vilivyotengenezwa kwa chuma na mpini wa ngozi ya mbuzi.

Pia, ni kawaida kwa wanaume kubeba marungu kadhaa; moja hutumiwa kwa kutembea na kusawazisha wakati wa kubeba mizigo, na lingine, kwa kawaida jembamba na refu, hutumika kuwachapia mifugo wakati wa shughuli ya ulindaji.

Wanaume pia hubeba viti vidogo (vinavyojulikana kama ekicholongs) na huvitumia kama viti kuliko kuketi chini kwenye mchanga ulio wa moto wakati wa mchana. Viti hivyo pia hufanya kichwa cha mkaliaji kubaki kama kimeinuka kutoka mchangani na hivyo basi kuzuia mapambo yoyote ya kichwa yasiharibike.

Wanawake kiutamaduni huvaa shanga, na kunyoa nywele zao kabisa ambazo mara nyingi zina shanga zilizofungiwa mwishoni mwa nywele. Wanaume pia hunyoa nywele zao. Wanawake huvalia vipande viwili vya nguo. Kimoja kikiwa kimefungwa kiunoni huku kingine kikisitiri upande wa juu wa mwili.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Angalia pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Pavitt, Nigel (1997) Turkana. London: Harvill Press. ISBN 1-86046-176-X
  • Lamphear, John (1988) 'The people of the grey bull: the origin and expansion of the Turkana', in Journal of African History, 29, 1, 27–39.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu utamaduni wa Kenya bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Waturkana kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.