Wabembe
Wabembe ni kabila la watu ambao wanaishi katika nchi mbalimbali za Maziwa Makuu ya Afrika.
Wanapatikana kwa wingi Fizi, na sehemu nyingine za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, lakini pia: Burundi, Kongo (Brazzaville), Tanzania na Afrika Kusini ambako wanaitwa Amapembe na Amapondo. Wanapatikana kwa wingi kwenye mikoa ya Free State, North West, Eastern Cape na Gauteng. Mwaka wa 2023, walijuana na Wabembe kutoka Kongo na Tanzania. Mwaka huohuo 2023, wakatuma mfalme na mwana-mfalme kutembelea Fizi. Kwa upande wao, walishimika mfalme ambaye atawaongoza wote kuanzia Malawi, Zimbabwe, Namibia, Afrika Kusini, Lesotho na Swaziland. Ufalme wao unahitwa Mpondomise. Kutokana na King Mashiya II, Wazungu waliandika vibaya jina la ukoo wao. Kuliko kuandika Mbondo waliandika Mpondo na kuliko kuandika Mbembe, waliandika Mpembe.
Katika nchi ya Tanzania, wengi wao wanaishi katika kingo za ziwa Tanganyika kutokana na uendeshaji wa shughuli zao. Wabembe ni moja kati ya makabila makubwa yanayopatikana katika Mkoa wa Kigoma, ila baadhi yao wako katika mkoa wa Rukwa. Wanapatikana hasa Ujiji, Buzebazeba, Mwanga, Sigunga, Ilagala, Sinuka, Kalya, Mgambo, Buhingu, Igalula na maeneo mengine. Kwa upande wa mkoa wa Rukwa wengi wanapatikana katika maeneo kama vile Kirando, Ikola, Kalungu, Kipili, Wampembe, Kala n.k.
Lugha yao ni Kibembe na huzungumzwa kila wanapokutana. Kabila la Wabembe limebeba makabila mengi ndani yake ambayo kwa sasa huizungumza lugha hiyo kama lugha yao. Makabila kama Wagoma, Wavinza, Wamanyema na wengineo huzungumza Kibembe kutokana na kupotea kwa lugha zao.
Kwa mujibu wa historia, Wabembe walianza kuingia nchini Tanzania miaka ya 1700 kutokana na kuhamahama, kama ilivyo Kwa makabila mengi ya Wabantu. Kabila hilo lilianza kuingia Tanzania likitokea nchi za Togo na Niger, hadi kufikia Kongo na hatimaye kutawanyika katika nchi nyingine zikiwemo Uganda, Kenya, Burundi na Zambia.
Ndugu zao ni Warega, Wakongo, Wazimba, Wabangubangu, Wazoba, Wavira na Wangala. Pia wana mfanano wa kitamaduni na kihistoria na Wasukuma, Wagoma, Wamanyema n.k
Katika mwaka wa 1991 ilikadiriwa kuwa idadi ya Wabembe ilikuwa 252,000 nchini Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia, ukiachilia mbali wale wa Tanzania na nchi mbalimbali.
Kwa sasa idadi ya Wabembe haijulikani kikamilifu, kufuatana na kusambaa kwa kabila hilo kwenye sehemu mbalimbali za mabara tofauti kama vile: Marekani, Australia, Ulaya ya Magharibi na Ulaya ya Kaskazini. Pia idadi ya Wabembe inaongezeka katika nchi za Afrika Kusini, Kenya, Zimbabwe, Malawi na Zambia.
Wabembe wanajiita taifa teule la Mungu kwa sababu wanadai kufanya miujiza ambayo makabila mengine hawawezi kufanya. Wanasema wakati wa vita vijana wao wanakimbia kuliko gari, wanaangusha ndege za maadui kwa mawe, wanakwenda vitani bila silaha na wanashinda.
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wabembe kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |