Wanilamba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Wanyiramba)

Wanilamba (au Wanyiramba) ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi mpakani mwa mikoa ya Singida na Shinyanga. Vijiji vya mpakani mwa Tabora wanapopatikana ni: Shelui, Mgongo, Nkonkilangi, Nsunsui, Mingela na Dolomoni.

Lugha yao ni Kinilamba, mojawapo ya lugha za Kibantu.

Historia yao[hariri | hariri chanzo]

Kabla ya Wakoloni kuingia barani Afrika, Makundi mbalimbali jamii ya wabantu walisafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine aidha kutafuta makazi salama au kufanya shughuli zingine za kibinadamu. Wanyiramba walikuwa miongoni ya jamii iliyosafiri kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine na hatimaye kufika walipo sasa.Inasemekana Wanyiramba walitokea Sudani. Walianza safari yao wakielekea Kusini mwa Afrika hadi walipofika Pwani mwa Kenya (Mombasa) ambapo waliweka makazi yao hapo, Shughuli yao kubwa ilikuwa ni kilimo na uvuvi wa Samaki.

Jamii hii iliongezeka kiasi cha kuanza kugombea ardhi na jamii nyingine. Kundi kubwa liliondoka na kuelekea Kusini Magharibi mwa Kenya ambapo walijikuta wamefika Kandokando mwa ziwa Nyanza (kwa sasa Victoria) Mkoa wa Mara (Musoma). Hapo waliwakuta wenyeji wao yaani Wakurya, Wajita, Wakerewe nk. Wanyiramba waliishi hapo na kuanza kuongezeka, wenyeji wao walipoona idadi ya watu inaongezeka, wakahofia kunyang’anywa ardhi yao. Ndipo walipotaka kuanzisha vita baina yao na wageni. Wakiwa kwenye eneo la mapambano, kwa mshangao mkubwa pande zote mbili zilishuhudia radi ikipiga kwa nguvu katikati yao na hali kipindi hicho hakikuwa cha mvua. Baada ya kuona hivyo jamii hizo ziliachana na fikra ya mapigano.

Jamii hizi zilikaa na kutafakari, “kwa nini radi ilipiga hali haikuwa kipindi cha mvua?”, Viongozi wa Kinyiramba na Kikurya walifikiri sana kutokea kwa radi hiyo. Hivyo walishikana mikono na kusema, “sisi tumekuwa ndugu, hivyo hakuna sababu yoyote ya kugombana”. Wakakubaliana upande mmoja wakae wanyiramba na upande wa pili wakae wenyeji. Maisha yaliendelea kwa pande zote, hata hivyo viongozi wa kimila wa kinyiramba walitafakari na kufikiri sana, wakaamua kuwaeleza wenyeji wao kwamba “Sisi na ninyi tumekuwa ndugu hivyo hakuna sababu ya kugombea ardhi , tuacheni tuondoke tukatafute eneo jingine la kuishi. kuishi”.Kundi kubwa liliondoka Musoma na baadhi walibaki hapo na kujichanganya na makabila mengine. Kundi hilo lilielekea Kusini Mashariki mwa Ziwa Nyanza kwa sasa victoria na kujikuta wamefika Milima ya Usambara, wakamua kuishi hapo kwa muda, baada ya hapo waliondoka hadi walipofika eneo la Upareni nako hawakukaa sana bali waliondoka na kuendelea na safari yao hadi walipofika Morogoro, hapo waliishi kwa muda kwani waliamua kuondoka kuendelea na safari yao. Hata hivyo huko nyuma baadhi ya wanyiramba walibaki kuendelea na maisha, ushahidi wa kihistoria na wakisayansi unajitokeza pale majina yenye asili ya kinyiramba kuwepo katika maeneo yote waliopita kwa mfano, Makala, Msengi (msangi), Sha-mwelu (She-muhilu), Kitundu, mbogo nk. Baada ya hapo walielekea Iringa, huko waliwakuta wenyeji wao wakarimu sana walikaribishwa lakini wakaelezwa, kwamba ardhi yote imemilikiwa na wenyeji tena iko chini ya utawali wa kimila. Hivyo waliondoka kuelekea Kaskazini Magharibi mwa Iringa hadi walipotokezea Itigi Mkoani Singida huko waliwakuta Wabarabaig wakijishughulisha na ufugaji wa ng’ombe. Wanyiramba na Wabarabaig walikubaliana kubadilishana mali walizokuwa nazo. Wanyiramba waliwapatia Wabarabaig Mapambo waliyoyapata baharini na Mbegu walizozibeba na Wabarabaigi waliwapatia wanyiramba mifugo. Wanyiramba hawakupendezwa sana kuishi hapo hivyo waliamua kuondoka na kuendelea na safari yao. Katika kuondoka kwao makundi mawili yaligawanyika jingine lilipita mwambao mwa Tabora na hatimaye kufika sehemu iitwayo Lunua (Ushora – Ndago).

Kundi jingine likaelekea Kaskazini ambapo walikutana na Wanyaturu. Wanyaturu hawakutaka kuwaruhusu wanyiramba kupita hapo,kwa kuwa wanyiramba hawakuwa na nia ya kuishi hapo, waliamua kupambana na wanyaturu kwa mapigano makali.Baada ya kufanikiwa kupita waliendelea na safari kundi dogo liliachwa eneo la Kirumi likaendelea na maisha yao, kundi kubwa lilisonga mbele hadi lilipofika eneo la Kisiriri. Hapo walivutiwa na eneo hilo wakaamua kuweka makazi yao . Kadri walivyoongezeka waliendelea kutawanyika na kwenda sehemu mbalimbali kama vile:- Nduguti, Gumanga, Kinampanda, Ulemo, Iambi, mkalama, Ibaga, kinyangiri na wengine walishuka Shelui(bonde la ufa) wakakutana na wale wa ndago ambapo na wao waliendelea kutawanyika maeneo mbalimbali ya Iramba.Kutokana na mtawanyiko huo lugha ya kinyiramba ilianza kutofautiana kidogo kilahaja, yaani katika matamshi, maumbo na matumizi ya maneno katika lugha yenye asili moja.

Uhusiano kati ya Wanyiramba na Wanyisanzu[hariri | hariri chanzo]

Inasemekana kuna unasaba mkubwa kati ya wanyiramba na wanyisanzu, hii inatokana na ushahidi wa kihistoria na kisayansi kama ifuatavyo: Wanyiramba na Wanyisanzu mila na desturi, sanaa na utamaduni hazitofautiani kwani ni zile zile. Kwa mfano:- Majina ya Ukoo (Nduuli) wanyiramba na wanyisanzu hutumika yaleyale kwa mfano, Mpanda (Wanaume) Tyale (Wanawake), Gyunda (Wanaume) Mwani (wanawake), Mpinga (Wanaume) Kyoga (Wanawake) n.k.Aidha Nyimbo zote zinazoimbwa kwenye ngoma na Burudani huimbwa kwa lugha ya Kinyiramba iwe kwa Wanyiramba ama Wanyisanzu. Ushahidi mwingine ni mfanano na mpangilio wa sentensi na vitenzi kuishia na irabu a.

Kwa mfano, (Kiswahili): Juma anapiga mpira vizuri. (Kinyiramba): Juma ukua mumpila izaa. (Kinyisanzu): Juma ukua mumpila uzaa. (Kinyaturu): Juma ukua mumpila ijaa.

Kwa ujumla Wanyiramba na Wanyisanzu si watani bali ni ndugu, lakini myiramba ni mtani wa Makabila yote ya Musoma wakiongozwa na Wakurya. Watani wengine wa Wanyiramba ni Wanyaturu. Utani wa Mnyaturu na Myiramba ulikuja hasa pale njaa kali ilipoingia turu kiasi cha kupelekea wanyaturu kuhemea chakula kwa Wanyiramba.Koo Za Kinyiramba Wanyiramba wamegawanyika katika Koo ( Nduli) zaidi ya ishirini Koo hizi zimebainisha Mashina, Majina ya ukoo kwa upande wa Wanaume na Wanawake pia eneo lao la asili. Ukoo mkubwa katika kabila la Wanyiramba ni “Anambwa” Ukoo huu una matawi (Milongo) zaidi ya sita. Koo zingine ni “Anishung’u, Anambala, Anikyili, Anampanda, Anankumbi, Ananzoka, Anangili, Analilya, Anangu, Aniyuga, Anambeu, Anishanga, Anakumi, Anankamba, Anankali, Asambaa, Anakilima, Azigo, Anawendo na Anilimu.

Ufuatao ni ufafanuzi wa koo (nduli za Kinilyamba) kama jedwali linavyoonesha hapa chini: - NA KOO JINSI ASILI (ENEO) UHUSIANISHO ME KE 1 ANAMBWA (a) Anasitwa Kiula Mgalu - Kisiriri - Ndago - Shelui - Ulemo na - Tutu n.k. Mbwa Mwekundu (bI Anansimba Makala Kyunyu - Kisiriri Mbwa Mweusi (c) Anamkato Makala Kyunyu - Kisiriri Mbwa mweupe asiye na doa (d) Anansungui Makala Kyunyu - Kisiriri (e) Ani-tyaa Kilimba Kyunyu - Kimpunda - Tyaa Mbwa aliyejikuja mkia (f( Analunsanga Kitila Kyunyu - Lunsanga Mbwa mwenye mabaka 2 ANISHUNGU Mkumbo Mkumbo Kilie Mwigo -kisharita -munkonze -Galangala Upepo 3 ANAMBALA i) Gyole ii) Lyanga iii) Shani Gyole Gyole Gyole - Kinambala - Kisiriri -korongo(ndege) Kinyiramba(mpuugii) 4 ANIKYELI Msengi Kyeli - Kiomboi - Meli na - Ntwike Simba 5 ANAMPANDA - Mpanda - Shole Tyale Tyale - Kinampanda -punda - nyuki 6 ANANKUMBI Mgelwa Mpuzi - Shelui, - Wembere na - Mkalama -majani ya maboga -sungura 7 ANANZOKA i) Mbogo ii) Shukia Muuza Muuza -Kisiriri (Tyumba) - Gumanga Nyati 8 ANANGILI Shila Mwile - Kinyangiri, - - Kisiriri, - Kimagwe Ngiri 9 ANALILYA i) Shalua ii)Nsunza iii)Shalua Mwelu Mwelu Sagi - Kinalilya Kanga – Ndege 10 ANANGU/ANA MILAMBO i) Nkana ii) Nangu Mbula Nonge - Shelui - Ntwike - Mingela -Ngurumo za mvua -Mvua 11 ANIYUGA Shango Ntoma - Kimpunda - NKango Fisi 12 ANAMBEU Kingu Nzitu - Kinambeu - Mampanta - Kondoo - Paka 13 ANISHANGA Mkoma Nsumbu - Tulya - Migilango - Kisiriri - Nyani - Kuku 14 ANAKUMI Kitundu Msua - Kinakumi Mchwa 15 ANA – NKAMBA Shumbi Ntulu - Msingi - Nduguti - Chachu (me) - Pombe (ke) 16 ANA – NKALI Gunda Mpinga Pyuza Mwani Kyoga Mianzi - Iambi - Mkalama -Isanzu - Chui (me) - Jua 17 ASAMBAA Mgana Mwingo - Mkalama - Iambi -Isanzu -upepo(nzega) 18 ANA – KIZIGO Yindi Jima - Gumanga - Iambi - Mkalama -Ngombe -Maziwa(mtindi) 19 ANA – MWENDO Mwendo Kilima -Iambi -Mkalama -kinakumi -mchwa 20 ANI – LIMU Gwila Sungi -Gumanga -mkalama Kumbuka kwamba, baadhi ya koo zimetokana na koo zingine(matawi) kama ifuatavyo; ukoo wa anakizigo ni tawi la analilya,ukoo wa anamwendo ni tawi la anakumi na ukoo wa asambaa umetokana na ukoo wa anishungu.Wanaume(akina baba) na wanawake(akina mama) kwa heshima huitwa kwa mjina ya baba zao au watoto wao kwa kuanza na sha/shi (kwa wanaume) na na/ni (kwa wanawake). Kwa mfano; sha- makala, shi-shila, sha-kiula, sha-mkumbo, sha-mwile nk, kwa wanawake huitwa, na-mgalu, na-kitundu, ni-lyanga nk.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Utamaduni ni mwenendo wa maisha ya jamii, mtazamo wao wa mambo na taratibu zao za kuendesha maisha zinazowatofautisha wao na jamii nyingine. Utamaduni ndicho kitambulisho kikuu cha taifa na ni kielelezo cha utashi na uhai wa watu wake.Umoja, utulivu na mshikamano ambavyo watanzania tunajivunia vinatokana na utamaduni tuliojijengea.Nguzo za utamaduni ni pamoja na mila na desturi, lugha, sanaa, michezo na historia yetu.

Kwa mfano Wanyiramba wanachukia sana vitendo viovu kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, ubakaji, ulevi, uvivu, uzembe, uzururaji, umalaya, ubaguzi na udhalilishaji wa kijinsia mfano ukeketaji watoto wa kike. Mila na desturi nzuri ni utunzaji wa mali na rasilimali, kuheshimu utu wa watu, tabia ya usafi, uhifadhi na matumizi bora ya rasilimali na mazingira.

Utani baina ya koo na kati ya Wanyiramba na makabila mengine[hariri | hariri chanzo]

Kila ukoo katika kabila la wanyiramba wanao watani wao, kwa kinyiramba huitwa anishoi; kuna makundi mawili ya watani katika kabila la wanyiramba kama ifuatavyo; Analelya watani wake ni; anakumi, ananangu/anamilambo, anankamba, anankale, anambeu, ananzo-ka, anamwendo na aniyuga.

Watani wa anambua ni kama ifuatavyo; anishungu, anikyili, anishanga, anambala, anangili, anampanda na Anankumbi.

Kwa upande wa makabila mengine, wanyiramba watani Wao Wa asili ni watu wa Musoma yaani wakurya na wajita,watani wengine ni jirani zao wanyaturu.Utani wao haukuja hivihivi bali ulitokana na matukio mbalimbali katika maisha yao.

Ndoa[hariri | hariri chanzo]

Mtoto wa kiume alipofikia muda wa kuoa, aliomba ridhaa toka kwa wazazi wake,nao wazazi wakisharidhia ombi la mtoto wao walitoa ruksa ama Kumchagulia mke mwenye sifa ya uchapakazi, usafi, ukarimu, mpenda ndugu wa pande zote, nyumbani kwao wasiwe washirikina, maradhi ya ukoma, kifafa na kichaa. Mahari ilitolewa mbuzi 12 na ngombe mmoja, Mama mzaa binti alipewa mbuzi mmoja (mkoa) kutoka familia ya mtoto wa kiume.Naye mtoto wa kiume alipewa mbuzi mmoja na baba yake kama zawadi. Kabla ya harusi binti aliyekuwa anaolewa alikalishwa sehemu maalum na bibi zao kwa lengo la kumfunda ili aweze kuhimili maisha ya ndoa; halikadhalika kwa kijana aliyetarajia kuoa alipatiwa mafunzo toka Kwa wazee (mababu). Siku ya harusi watu waliandaliwa vyakula mbalimbali kama vile: ugali, kande, nyama ya ngombe, mbuzi na vinywaji kama: Togwa (magae ya nkaata) na pombe (magae ya ntulu), sherehe hizo Zilikua zinaambatana michezo na burudani mbalimbali mfano “ngoma ya winga”.

Wanyiramba ni wasanii wazuri katika masuala ya sanaa hususani: ufinyanzi, ususi, uchoraji, uchongaji, ngoma, nyimbo nk. Vile vile Wanyiramba hawapo nyuma katika masuala ya michezo ya jadi kama vile bao, kulenga shabaha, kufukuza kuku, mieleka nk. Wanyiramba hujiburudisha kupitia burudani mbalimbali kama ngoma ya mbutu, ngoma ya Winga ambayo huchezwa kwenye harusi, mpembe ambayo huchezwa wakati wa mavuno, mara nyingi burudani hizi huambatana na vinywaji kama vile: magae mantulu (pombe iliyotengenezwa kwa mtama) na magae ya nkataa (togwa). Kadri muda unavyozidi kwenda mbele, Utamaduni wa Wanyiramba unapungua kidogo kidogo. Hivyo zinatakiwa hatua za maksudi kulinda Mila na desturi.

Kwa upande wa mavazi Wanyiramba walitumia sana kaniki na lubega ingawa kwa siku hizi mavazi haya, hayavaliwi kutokana na utandawazi. Vazi la kaniki na lubega kwa sehemu kubwa huvaliwa wakati wa matambiko, sanaa na burudani.

Hakuna kumbukumbu za kutosha zinazoelezea Utamaduni, Mila na desturi, Rasilima na Utalii wa Wanyiramba na kama zipo hazijatunzwa mahali stahili au eneo muhimu.

Asili[hariri | hariri chanzo]

Kama ilivyo kwa jamii nyingine za Kibantu barani Afrika ambao walihamia Mashariki na Kusini mwa Afrika wakitokea Afrika Magharibi, hususani nchi za Kameruni, Nijeria na Ghana wakipita misitu ya Kongo, Wanyiramba na Wanyisanzu walikuwa katika kundi mojawapo lililoelekea mashariki hadi maeneo ya Ziwa Nyanza (Victoria) hadi katika kisiwa cha Ukerewe kilichopo katika ziwa hilo kubwa zaidi barani Afrika.

Japo haijulikani sababu hasa, kundi moja liliondoka katika kisiwa cha Ukerewe hadi kisiwa cha Uzinza na kutoka huko wakahama hadi maeneo ya Tabora ambako waligawanyika, kundi moja likielekea kusini na inasemekana ndio waliokuja kuwa Wagogo na baadhi ya Wanyaturu (Wanyaturu wa Kibantu, yaani wasio na asili ya Kikushi, maana kuna Wanyaturu wa Kibantu na wale wa asili ya Kikushi wa kutoka Ethiopia), huku kundi lingine likiendelea kuelekea mashariki kupitia mlima Sekenke hadi Kisiriri.

Walipoanza kuitwa Wanyiramba na Wanyisanzu/Waihanzu[hariri | hariri chanzo]

Wakaishi hapo Kisiriri kwa muda mrefu kabla ya kutokea ukame mkubwa sana uliosababisha njaa katika eneo hilo. Ili kukabiliana na tatizo hilo la njaa, watu hao walitumia mboga za majani zaaina ya mlenda uliokaushwa zijulikanazo kama "ndalu" kama chakula kikuu. Kutokana na kula "ndalu" kwa mtindo wa kulamba, watu wa makabila mengine ya kibantu walivyowaona wakawaita "wenye kulamba" na baadaye likabadilika hadi kuwa "wenyilamba" hadi "Wanyiramba". Ikumbukwe kuwa hadi hapo Wanyisanzu na Wanyiramba walikuwa kabila moja na wote walifahamika kama Wanyiramba baada ya njaa hiyo.

Wanyisanzu/Waihanzu wahamia pori la Mkalama[hariri | hariri chanzo]

Kundi moja likaamua kuondoka hapo Kisiriri hadi pori la Mkalama wakiwa na mifugo yao na familia zao na walipofika katika pori hilo ili kujilinda na wanyama wakali wakajenga nyumba na kuzungushia maboma ya miba maarufu kama "masanzu/mahanzu". Baadaye baadhi ya Wanyiramba waliobaki Kisiriri nao waliamua kuondoka hapo na walipofika Mkalama wakawakuta wenzao wamezungushia nyumba zao kwa Maboma ya "masanzu/mahanzu" ndipo walipoanza kuwaita hawa ni wanyisanzu au waihanzu.

Wanyiramba na Wanyisanzu japo wana historia inayofanana na kwa mtu mgeni anaweza kudhani kuwa hakuna tofauti baina yao, lakini ukweli ni kuwa kuna tofauti kubwa sana baina yao.

Koo zao na wanapopatikana[hariri | hariri chanzo]

Wanyiramba: Hizi ni koo tano za Wanyiramba na wanapopatikana

  • Kinampanda: Wanaishi sehemu za milimani hasa huko Kinampanda
  • Anagimbu: Wapo Iramba Mashariki
  • Waiambi/waiyambi: Wanaishi Nkungi na Iambi
  • Anishai: Wanapatikana Kinandili na
  • Akimbu: Hawa wapo mpakani mwa Iramba na Tabora

Kwa upande wa Wanyisanzu, wao wana koo nne tu

  • Mnyakilumi: Wapo maeneo ya Kilumi/Kirumi
  • Mnyatumbili: Wanaishi Ikolo
  • Mnyadintima: Hawa wanapatikana Mwangeza na
  • Mnyasoha: Waishio Mkalama

Vyakula wanavyopenda Wanyiramba[hariri | hariri chanzo]

Wanyiramba wanavyo vyakula vya asili ambavyo huvitumia, vyakula hivyo ni: ugali wa mtama, uwele na mahindi; mahindi ya kupikwa na kuchoma, maboga.

Mboga ni kyuluga (mlenda), nsonga, ndalu (mlenda uliokaushwa na kusagwa), nsansa (majani ya kunde yaliyopikwa na kukaushwa), akwepa, kukulu, kyumbo, muzuo, matembele, mung'ang'i, kinsagi, ulyoze, nyama/nama, majokolo nk.

Vyakula vingine ni indoolo (viazi) na mihogo.

Aidha kuna matunda ya asili nayo ni; matogo, nsisai, mbilo, nsingila, mapama, ntundua, mbula, ntunguza, numpilo, nsansampeke, mpumambuli, maungo, mpulu, mbwembwe nk.

Vinywaji ni togwaa, pombe/magai mantulu.

Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wanilamba kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.