Australia
Jumuiya ya Australia Commonwealth of Australia | |
---|---|
Wimbo wa taifa: Advance Australia Fair | |
Mji mkuu | Canberra |
Mji mkubwa | Sydney (Jiji) Melbourne (Jiji Kuu) |
Lugha rasmi | Kiingereza (kenyekenye) |
Lugha ya taifa | Kiingereza |
• Mfalme wa Australia | Charles III wa Uingereza |
• Gavana Mkuu | Sam Mostyn |
Uhuru kutoka Uingereza | |
• Katiba ya Australia | 1 Januari 1901 |
• Sanamu ya Westminster | 11 Desemba 1931 |
• Sheria za Australia | 3 Machi 1986 |
Eneo | |
• Jumla | km2 7,617,930 (ya 6) |
• Maji (asilimia) | 1.79% |
• Ardhi | km² 2,969,907 |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2024 | 27,618,900 |
• Msongamano | 3.4/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ![]() |
• Kwa kila mtu | ![]() |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ![]() |
• Kwa kila mtu | ![]() |
HDI (2024) | 0.946 |
Gini (2020) | 32.5 |
Sarafu | Dola ya Australia |
Upande wa magari | Kushoto |
Msimbo wa simu | +61 |
Jina la kikoa | .au |
Australia, rasmi kama Jumuiya ya Australia, ni nchi iliyo katika Oceania, inayojumuisha bara la Australia, kisiwa cha Tasmania, na visiwa vingine vidogo. Inapakana na Bahari ya Hindi magharibi na Kusini, Bahari ya Pasifiki mashariki, na nchi za Indonesia, Timor ya Mashariki, na Papua Guinea Mpya kaskazini. Ina idadi ya watu takriban milioni 27, ikiwa ya 55 duniani. Jiji lake kubwa zaidi ni Sydney na mji mkuu ni Canberra.Australia imegawanyika katika majimbo 6 na maeneo 2 yanayojiendesha.
Inajulikana kwa mazingira yake ya kipekee, ikiwemo Jangwa la Outback, Miamba ya Matumbawe ya Great Barrier Reef, na wanyama wa kipekee kama kangaruu na koala. Vilevile Australia huangaliwa pamoja na visiwa vya Pasifiki katika orodha ya mabara ya dunia kama "Australia na Pasifiki".
Idadi ya wakazi ni 25,970,200 (mwaka 2022).
Demografia
[hariri | hariri chanzo]Australia ina msongamano wa watu wa wastani wa watu 3.4 kwa kila kilomita ya mraba ya eneo lote la ardhi, jambo linaloifanya kuwa moja ya nchi zenye msongamano mdogo zaidi wa watu duniani. Idadi kubwa ya watu inapatikana kwenye pwani ya mashariki, hasa katika eneo la kusini-mashariki kati ya Kusini Mashariki mwa Queensland upande wa kaskazini-mashariki na Adelaide upande wa kusini-magharibi.
Australia pia ina kiwango kikubwa cha miji mikuu, ambapo 67% ya idadi ya watu waliishi katika Maeneo ya Takwimu za Miji Mikuu (maeneo ya miji mikuu ya majimbo na miji mikuu ya wilaya ya bara) mwaka 2018. Maeneo ya miji mikuu yenye zaidi ya wakazi milioni moja ni Sydney, Melbourne, Brisbane, Perth, na Adelaide.
Kama ilivyo kwa nchi nyingi zilizoendelea, Australia inakumbwa na mabadiliko ya idadi ya watu kuelekea kwenye idadi kubwa ya wazee, ikiwa na wastaafu wengi na idadi ndogo ya watu wa umri wa kufanya kazi. Mnamo mwaka 2021, wastani wa umri wa watu ulikuwa miaka 39. Mnamo 2015, 2.15% ya idadi ya watu wa Australia waliishi nje ya nchi, moja ya viwango vya chini zaidi duniani.
Dini
[hariri | hariri chanzo]
Katika sensa ya mwaka 2021, Wakristo walikuwa 43.9% ya wakazi wote, wakiongozwa na Wakatoliki (20%) na Waanglikana (9.8). Waislamu walikuwa 3.2%, Mabanyani 2.7%, Wabuddha 2.4%, Singasinga 0.8%, Wayahudi 0.4% n.k. 38.9% walisema hawana dini yoyote. [1]
Lugha
[hariri | hariri chanzo]Australia haina lugha rasmi, lakini 72% ya wakazi nyumbani wanaongea Kiingereza cha Kiaustralia tu. Lugha nyingine zinazotumika na zaidi ya 1% ya wakazi ni ni Kichina, Kiarabu, Kivietnam, Kipanjabi n.k. Wachache nyumbani wanaongea mojawapo kati ya lugha asili za Australia. Angalia pia Orodha ya lugha za Australia. [2]
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]
Bara la Australia linakaa juu ya sehemu imara ya bamba la Australia bila mipaka ya gandunia na kwa hiyo hakuna volkeno; matetemeko ya ardhi ni madogo tu.
Umbali kati ya magharibi na mashariki ni km 4,000, na kati ya kaskazini na kusini umbali ni km 3,700.
Australia huzungukwa na bahari ya Hindi, bahari ya Pasifiki na Bahari ya Kusini. Kwa jumla ina pwani yenye urefu wa kilomita 34,218.
Great Barrier Reef mbele ya pwani ya mashariki-kaskazini ni vipwa vya matumbawe vikubwa duniani; ina urefu wa kilomita 2,000.
Sehemu kubwa ya bara ni jangwa au maeneo yabisi sana. Takriban asilimia 40 ya eneo limefunikwa na matuta ya mchanga. Ardhi yenye rutuba iko kusini-mashariki na kona ya kusini-magharibi pamoja na hali ya hewa isiyo na joto kali. Hali ya hewa kaskazini ni ya kitropiki na huko kuna misitu minene pamoja na savana na jangwa.
Sehemu kubwa ya uso wa nchi ni tambarare na majangwa. Kwenye pwani ya mashariki na pia upande wa magharibi kuna safu za milima inayopanda hadi kimo cha mita 2,200. Sehemu ya juu kabisa huitwa milima ya theluji au Alpi za Australia na mlima Kosciuszko unafikia kimo cha mita 2,229. Huko kuna barafuto za kudumu.
Sehemu ya chini iko kwenye beseni la ziwa Eyre iliyopo mita 17 chini ya usawa wa bahari. Tako la beseni hilo mara nyingi ni kavu kabisa, huwa pamejaa maji mara chache tu baada ya mvua kubwa sana.
Mahali pakavu kabisa ni jangwa la Simpson lenye usimbishaji chini ya 200 mm kwa mwaka.
Mito muhimu inaanza katika Alpi za Australia: ni Murray na Darling inayomwagilia beseni la Murray-Darling na hii ni eneo muhimu la kilimo cha Australia.
Mingine ni Mto Snowy na Mto Murrumbidgee, halafu mto Fitzroy (Queensland), mto Ord, mto Swan (Australia ya Magharibi), mto Derwent, mto Tamar (Tasmania) na mto Hawkesbury (New South Wales).
Sehemu kubwa ya bara haina watu. Wakazi wengi pamoja na miji yote wako kwenye pwani ya mashariki na kusini.
Miji mikubwa ni Sydney (wakazi milioni 3.7), Melbourne (wakazi milioni 3.6), Brisbane (wakazi milioni 1.7), Perth (wakazi milioni 1.4) na Adelaide (wakazi milioni 1.1).
Mji mkuu, Canberra (wakazi 308,700), ulijengwa kati ya Sydney na Melbourne kwa sababu miji hiyo miwili ilishindwa kukubaliana ni upi unaostahili kuwa mji mkuu.
Uchumi katika maeneo yabisi ni hasa ufugaji wa kondoo milioni 130 na ng'ombe milioni 25.
Ekolojia
[hariri | hariri chanzo]Australia ilitengana na mabara mengine miaka milioni mingi iliyopita. Kwa sababu hiyo kuna aina nyingi za pekee za mimea na wanyama zisizopatikana penginepo duniani. Wanyama wa pekee ni kwa mfano kanguru na koala. Miti ya Australia kama vile mkalitusi imepelekwa kote duniani katika nchi zenye hali ya hewa ya kufaa.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Watu wa kwanza walifika Australia takriban miaka 65,000 iliyopita[3]. Walitunza utamaduni wa wawindaji-wakusanyaji hadi kufika kwa wakoloni (1606).
Hakuna habari kama watu wa Asia walifikia Australia lakini tangu karne ya 17 BK Waholanzi halafu Waingereza walifika kwa jahazi zao.
Australia ikawa mahali pa koloni la kigereza na wafungwa kutoka Uingereza walipelekwa huko katika karne ya 19. Baadaye walifika pia walowezi huru.
Idadi ya Waustralia asilia imepungua sana kutokana na magonjwa mapya wakiambukizwa na Wazungu, pia walitendewa vibaya na kufukuzwa katika sehemu kubwa ya nchi yao.
Australia ilipata uhuru wake mwaka 1901 lakini inaendelea kumkubali malkia ya Uingereza kama Mkuu wa Dola akiwasilishwa na Gavana Mkuu. Mamlaka imo mikononi mwa waziri mkuu na serikali yake.
Serikali
[hariri | hariri chanzo]Muundo wa utawala ni wa shirikisho. Kuna majimbo 6 ya kujitawala pamoja na maeneo ambayo yako moja kwa moja chini ya serikali ya shirikisho.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Australia Bureau Of Statistics. "Religious affiliation in Australia". Iliwekwa mnamo 2025-02-10.
- ↑ Australian bureau of Statistics. "Languages of Australia". Iliwekwa mnamo 2025-02-10.
- ↑ Clarkson, Chris; Jacobs, Zenobia; Marwick, Ben; Fullagar, Richard; Wallis, Lynley; Smith, Mike; Roberts, Richard G.; Hayes, Elspeth; Lowe, Kelsey; Carah, Xavier; Florin, S. Anna; McNeil, Jessica; Cox, Delyth; Arnold, Lee J.; Hua, Quan; Huntley, Jillian; Brand, Helen E. A.; Manne, Tiina; Fairbairn, Andrew; Shulmeister, James; Lyle, Lindsey; Salinas, Makiah; Page, Mara; Connell, Kate; Park, Gayoung; Norman, Kasih; Murphy, Tessa; Pardoe, Colin (2017). "Human occupation of northern Australia by 65,000 years ago". Nature. 547 (7663): 306–310. Bibcode:2017Natur.547..306C. doi:10.1038/nature22968. hdl:2440/107043. ISSN 0028-0836. PMID 28726833.
- Davison, Graeme; Hirst, John; Macintyre, Stuart (1999). The Oxford Companion to Australian History. Melbourne, Vic.: Oxford University Press. ISBN 0-19-553597-9.
{{cite book}}
: CS1 maint: multiple names: authors list (link) - Jupp, James (2001). The Australian people: an encyclopedia of the nation, its people, and their origins. Cambridge University Press. ISBN 0-521-80789-1.
- Smith, Bernard; Smith, Terry (1991). Australian painting 1788–1990. Melbourne, Vic.: Oxford University Press. ISBN 0-19-554901-5.
{{cite book}}
: CS1 maint: multiple names: authors list (link) - Teo, Hsu-Ming; White, Richard (2003). Cultural history in Australia. University of New South Wales Press. ISBN 0-86840-589-2.
{{cite book}}
: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
Marejeo mengine
[hariri | hariri chanzo]- Denoon, Donald, et al. (2000). A History of Australia, New Zealand, and the Pacific. Oxford: Blackwell. ISBN 0-631-17962-3
- Goad, Philip and Julie Willis (eds) (2011). The Encyclopedia of Australian Architecture Cambridge University Press, Port Melbourne, Victoria. ISBN 978-0-521-88857-8
- Hughes, Robert (1986). The Fatal Shore: The Epic of Australia's Founding. Knopf. ISBN 0-394-50668-5.
- Powell JM (1988). An Historical Geography of Modern Australia: The Restive Fringe. Cambridge, U.K.: Cambridge University Press. ISBN 0-521-25619-4
- Robinson GM, Loughran RJ, and Tranter PJ (2000) Australia and New Zealand: economy, society and environment. London: Arnold; NY: OUP; 0340720336 paper 0-340720328 hard.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- About Australia Ilihifadhiwa 31 Desemba 2014 kwenye Wayback Machine. from the Department of Foreign Affairs and Trade website
- Governments of Australia website (federal, states and territories)
- Australian Government website
- Australian Bureau of Statistics
- Community organisations portal Ilihifadhiwa 2 Mei 2010 kwenye Wayback Machine.
- Tourism Australia
- Australia entry at The World Factbook
- Australia Ilihifadhiwa 16 Novemba 2009 kwenye Wayback Machine. at UCB Libraries GovPubs
- Australia katika Open Directory Project
Nchi_na maeneo ya Australia na Pasifiki |
Australia | Fiji | Guam | Hawaii | Kaledonia Mpya | Kiribati | Kisiwa cha Pasaka | Mikronesia | Nauru | Nyuzilandi | Niue | Pitcairn | Polinesia ya Kifaransa | Palau | Papua Guinea Mpya | Samoa | Samoa ya Marekani | Visiwa vya Cook | Visiwa vya Mariana ya Kaskazini | Visiwa vya Marshall | Visiwa vya Solomon | Tonga | Tuvalu | Vanuatu | Wallis na Futuna |
![]() |
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|