Wasafwa
Jump to navigation
Jump to search
Wasafwa ni kabila la watu kutoka eneo la milima ya mkoa wa Mbeya, kusini mwa nchi ya Tanzania.
Wako hasa katika wilaya za Mbeya mjini, Mbeya vijijini, Mbozi na Chunya
Mwaka 1987 idadi ya Wasafwa ilikadiriwa kuwa 158,000 [1].
Rangi kuu ya mavazi yao ni njano.
Dini kuu zilizotawala kati yao ni Ukristo na Uislamu, lakini wengine wamebaki kuamini mila zao.
Uongozi wa kimila[hariri | hariri chanzo]
Kiongozi wa Wasafwa huitwa mwene kwa lugha yao.
Mwene maarufu sana alikuwa Mwene Paul Mwashinga aliyekuwa tajiri na msomi; makao makuu yake yalikuwa Igawilo, Mbeya mjini; naye aliaga dunia mwaka 1987; msiba wake ulihudhuriwa na watu mashuhuri sana.
Mwene mwingine ni Mwene Mwalyego wa Mbalizi.
Tanbihi[hariri | hariri chanzo]
![]() |
Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Wasafwa kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |