Wairaqw

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwanamume wa Kiiraqw.
‎Nyumba ya wakulima Wairaqw huko mkoa wa Manyara mwaka 2012.

Wairaqw (pia huitwa Wambulu kutokana na jina la mji wa Mbulu) ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika mkoa wa Manyara na mkoa wa Arusha kusini kwa Ngorongoro.

Lugha yao ni Kiiraqw, jamii ya lugha za Kikushi za kusini.

Mwaka 2001 walikuwa 462,000 hivi. Idadi hiyo yaweza kuwa imevuka 1,000,000 kwa sasa.

Asili[hariri | hariri chanzo]

Kihistoria, ni kati ya Wakushi wa kwanza kuhamia eneo la Tanzania ya sasa, ambapo walichanganyikana na Wadatoga na Wabantu, inavyoonekana katika utafiti juu ya DNA. Walitokea Ethiopia katika milenia ya 3 KK na kuelekea kusini kupitia bonde la Ufa.

Nadharia nyingine zinapendekeza kuwa walitokea Mesopotamia ya kale. Hata hivyo hakuna uhusiano dhahiri na nchi ya Irak (au Iraq) iliyopo katika Asia ya Magharibi, isipokuwa jina la kufanana.

Flag of Tanzania.svg Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wairaqw kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.