Wampoto

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wampoto ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Ruvuma, Wilaya ya Mbinga. Eneo lao ni mwambao wa ziwa Nyasa (kuanzia Hinga, Mbuli, Ngumbo, Ndingine, Mkili, Yola, Nindai, Tawi, Njambe, Mango, Tumbi, Ngehe na sehemu ndogo ya Puulu na Liuli ambako wamechangamana na Wanyasa).

Wanapakana na Wanyasa (kusini), Wamanda (kaskazini) na Wamatengo (mashariki). Wanahusiana zaidi na majirani wao Wamatengo na Wanyasa.

Lugha yao ni Kimpoto, lugha ya Kibantu ambayo mwaka wa 1977 idadi ya wasemaji wake ilihesabiwa kuwa watu 80,000. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kimpoto iko katika kundi la N10. [1]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wampoto kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.